Mika 7:1-20
7 Ole wangu! Mimi ni kama mutu mwenye,Kisha kukusanya matunda ya kipindi cha jotoNa masalio kisha mavuno ya zabibu,Hapate kishada cha zabibu za kula,Wala tini ya kwanza-kwanza yenye ninatamani sana.*
2 Mushikamanifu amekosekana katika dunia;Hakuna munyoofu kati ya wanadamu.+
Wote wanavizia ili kumwanga damu.+
Kila mumoja anawinda ndugu yake kwa wavu wa* kukokotwa.
3 Mikono yao inajua kabisa kufanya mambo ya mubaya;+Mukubwa anaomba mambo fulani,Muamuzi anaomba zawabu,+Mutu wa maana anaonyesha wazi tamaa yake,*+Na wanafanya mupango mubaya pamoja.*
4 Mutu mwema zaidi kati yao ni kama miiba,Na mutu munyoofu zaidi kati yao ni mubaya zaidi kuliko ukuta wa miiba.
Siku ya walinzi wenu na ya ninyi kutoa hesabu itakuja.+
Sasa watahangaika sana.+
5 Usiamini mwenzakoAo kutumainia rafiki yako wa karibu.+
Ukuwe muangalifu juu ya mambo yenye unaambia mwenye kulala kwenye kifua chako.
6 Kwa maana mwana anazarau baba yake,Binti anasimama kupingana na mama yake,+Na binti-mukwe anapinga mama-mukwe wake;+Maadui wa mutu ni watu wa nyumba yake.+
7 Lakini mimi, nitaendelea kumungojea Yehova.+
Nitaonyesha mutazamo wa kumungojea* Mungu wa wokovu wangu.+
Mungu wangu atanisikia.+
8 Usishangilie juu yangu, Ee adui* yangu.
Hata kama nimeanguka, nitasimama;Hata kama ninakaa katika giza, Yehova atakuwa mwangaza wangu.
9 Nitavumilia kasirani kali ya Yehova—Kwa maana nimemutendea zambi+—Mupaka wakati atatetea kesi yangu ya hukumu na kufanya nitendewe haki.
Atanileta inje kwenye mwangaza;Nitaangalia uadilifu* wake.
10 Adui yangu pia ataona,Haya itamufunika mwenye aliniambia:
“Yehova Mungu wako iko* wapi?”+
Macho yangu yatamuangalia adui yangu.
Sasa atakanyangwa kama matope katika barabara.
11 Itakuwa siku ya kujenga kuta zako za majiwe;Siku hiyo mipaka yako itapanuliwa.*
12 Siku hiyo watu watakuja kwakoKutoka Ashuru na miji ya Misri,Na kutoka Misri mupaka kwenye ule Muto;*Kutoka bahari mupaka bahari na kutoka mulima mupaka mulima.+
13 Na inchi itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakaaji wake,Kwa sababu ya mambo yenye wamefanya.*
14 Chunga watu wako kwa fimbo yako, kundi la uriti wako,+Mwenye alikuwa anaishi peke yake katika pori—katikati ya shamba la matunda.
Uwaache wakule katika Bashani na Gileadi+ kama vile katika siku za zamani.
15 “Kama vile katika siku zenye ulitoka katika inchi ya Misri,Nitamuonyesha mambo ya ajabu.+
16 Mataifa yataona na kusikia haya hata kama yako na nguvu nyingi.+
Watatia mikono yao juu ya vinywa vyao;Masikio yao yatakuwa kama ya viziwi.
17 Watalambula mavumbi kama nyoka;+Kama wanyama wa dunia wenye kutambaa watatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Watakuja kwa Yehova Mungu wetu wakiwa na woga,Na watakuogopa.”+
18 Ni Mungu gani mwenye kuwa kama wewe,Mwenye kusamehe makosa na mwenye haangalie makosa+ ya mabaki ya uriti wake?+
Hataendelea kuwa na kasirani milele,Kwa maana anafurahia upendo mushikamanifu.+
19 Atatuonyesha tena rehema;+ atashinda* makosa yetu.
Utatupa zambi zao zote katika sehemu za chini kabisa za bahari.+
20 Utaonyesha uaminifu kwa Yakobo,Upendo mushikamanifu kwa Abrahamu,Kama vile uliapia mababu zetu tangu siku za zamani.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “nafsi yangu inatamani sana.”
^ Ao “makila ya.”
^ Ao “tamaa ya nafsi yake.”
^ Tnn., “wanausuka pamoja.”
^ Ao “Nitamungojea kwa uvumilivu.”
^ Katika Kiebrania, neno lenye kutafsiriwa “adui” liko katika jinsia ya kike.
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “eko.”
^ Ao pengine, “amri itakuwa mbali sana.”
^ Ni kusema, Efrati.
^ Tnn., “Kwa sababu ya matunda ya matendo yao.”
^ Ao “atakanyangia chini, atatiisha.”

