Mika 4:1-13
4 Katika kipindi cha mwisho cha zile siku,*Mulima wa nyumba ya Yehova+Utawekwa imara kabisa kwenye kichwa cha milima,Na utainuliwa juu ya vilima,Na vikundi vya watu vitamiminika kule.+
2 Na mataifa mengi yataenda na kusema:
“Mukuje, tupande kwenye mulima wa YehovaNa kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+
Atatufundisha njia zake,Na tutatembea katika njia zake.”
Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.
3 Atafanya hukumu kati ya vikundi vingi vya watu+Na kunyoosha* mambo kuhusu mataifa yenye nguvu yenye kuwa mbali.
Watafua panga zao kuwa majembeNa mikuki yao kuwa miundu.*+
Taifa halitainua upanga juu ya taifa,Wala hawatajifunza vita tena.+
4 Watakaa,* kila mutu chini ya muzabibu wake na chini ya muti wake wa tini,+Na hakuna mutu mwenye atawaogopesha,+Kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema.
5 Kwa maana vikundi vya watu vitatembea, kila mutu katika jina la mungu wake,Lakini sisi tutatembea katika jina la Yehova Mungu wetu+ milele na milele.
6 “Katika siku hiyo,” ni vile Yehova anasema,“Nitakusanya ule mwenye alikuwa anatembea kwa kukokota muguu,*Na kukusanya mwenye kutawanyika,+Pamoja na wale wenye nilitendea kwa ukali.
7 Ule mwenye alikuwa anatembea kwa kukokota muguu* nitamufanya kuwa baki,+Na ule mwenye alikuwa amepelekwa mbali nitamufanya kuwa taifa lenye nguvu;+Na Yehova atakuwa mufalme juu yao kwenye Mulima Sayuni,Kuanzia sasa na milele.
8 Sasa wewe, Ee munara wa kundi,Kilima cha binti ya Sayuni,+Utakuja kwako, ndiyo, utawala wa kwanza* utakuja kwako,+Ufalme wa binti ya Yerusalemu.+
9 Sasa sababu gani unalalamika kwa sauti kubwa?
Je, hauna mufalme,Ao mushauri wako ameangamia,Na hivyo maumivu yamekushika kama mwanamuke mwenye kuzaa?+
10 Ukuwe katika maumivu makali na ulie kwa maumivu, Ee binti ya Sayuni,Kama mwanamuke mwenye kuzaa,Kwa kuwa sasa utatoka katika muji na kukaa katika mashamba.
Utaenda mupaka Babiloni,+Na utakombolewa kule;+Kule Yehova atakununua tena kutoka katika mukono wa maadui wako.+
11 Sasa mataifa mengi yatakusanyika ili kukushambulia;Yatasema, ‘Muache achafuliwe,Na muache macho yetu yaone namna jambo hili litapata Sayuni.’
12 Lakini hawajue mawazo ya Yehova,Hawaelewe kusudi* lake;Kwa maana atawakusanya kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka kama nafaka yenye imetoka kuvunwa.
13 Simama na upige-pige nafaka, Ee binti ya Sayuni;+Kwa maana nitabadilisha pembe zako kuwa chuma,Na nitabadilisha kwato* zako kuwa shaba,Na utaponda-ponda vikundi vingi vya watu.+
Utamutolea Yehova faida yao yenye haiko ya haki,Na mali zao utazipatia Bwana wa kweli wa dunia yote.”+

