Mika 3:1-12
3 Nikasema: “Tafazali, musikie ninyi vichwa vya YakoboNa ninyi makamanda wa nyumba ya Israeli.+
Munapaswa kujua yenye kuwa haki, haiko vile?
2 Lakini munachukia mambo ya muzuri+ na munapenda mambo ya mubaya;+Munachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao.+
3 Pia munakula nyama ya watu wangu+Na kuwachuna ngozi,Munavunja mifupa yao, na kuiponda-ponda,+Kama kitu chenye kupikwa ndani ya chungu,* kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.
4 Wakati huo watamuita Yehova awasaidie,Lakini hatawajibu.
Ataficha uso wake wakati huo,+Kwa sababu ya matendo yao maovu.+
5 Yehova anasema hivi juu ya manabii wenye kupotosha watu wake,+Wenye kutangaza ‘Amani!’+ wakati wanatafuna kwa meno yao,+Lakini wenye kutangaza* vita juu ya mutu yeyote mwenye hatie kitu katika vinywa vyao:
6 ‘Mutakuwa na usiku;+ hakutakuwa maono;+Mutakuwa na giza tu, hamutafanya uaguzi.
Jua litashuka juu ya manabii,Na muchana utageuka kuwa giza kwao.+
7 Watu wenye kuona maono watapatishwa haya,+Na waaguzi watakatishwa tumaini.
Wote watafunika masharubu yao,*Kwa maana hakuna jibu kutoka kwa Mungu.’”
8 Lakini mimi, ninajaa nguvu kupitia roho ya Yehova,Na haki na uwezo,Ili nimuambie Yakobo uasi wake na Israeli zambi yake.
9 Tafazali musikie jambo hili, ninyi vichwa vya nyumba ya YakoboNa ninyi makamanda wa nyumba ya Israeli,+Wenye kuchukia haki na kupotosha mambo yote yenye kunyooka,+
10 Wenye kujenga Sayuni kwa kumwanga damu na Yerusalemu kwa ukosefu wa haki.+
11 Viongozi wake* wanapokea rushwa* ili kuhukumu,+Makuhani wake wanafundisha ili wapate malipo,+Na manabii wake wanafanya uaguzi ili wapate feza.+
Na hata hivyo wanamutegemea Yehova,* kwa kusema:
“Je, Yehova haiko pamoja na sisi?+
Hakuna musiba wenye utatupata.”+
12 Basi kwa sababu yenu,Sayuni italimwa kama shamba,Yerusalemu itakuwa marundo ya mabomoko,+Na mulima wa Nyumba* utakuwa kama mahali pa juu katika pori.*+
Maelezo ya Chini
^ Ao “chungu cha kupikia chenye mudomo mukubwa.”
^ Tnn., “kutakasa.”
^ Ao “watafunga vinywa vyao.” Masharubu ni nywele zenye kuota kwenye mudomo wa juu.
^ Tnn., “Vichwa vyake.”
^ Ao “kata-midomo.”
^ Ao “wanasema kama wanamutegemea Yehova.”
^ Ao “mulima wa hekalu.”
^ Ao “kilima chenye miti.”

