Mika 3:1-12

  • Viongozi na manabii wanalaumiwa (1-12)

    • Mika anapata nguvu kwa sababu ya roho ya Yehova (8)

    • Makuhani wanafundisha ili wapate feza (11)

    • Yerusalemu itakuwa marundo ya mabomoko (12)

3  Nikasema: “Tafazali, musikie ninyi vichwa vya YakoboNa ninyi makamanda wa nyumba ya Israeli.+ Munapaswa kujua yenye kuwa haki, haiko vile?  2  Lakini munachukia mambo ya muzuri+ na munapenda mambo ya mubaya;+Munachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao.+  3  Pia munakula nyama ya watu wangu+Na kuwachuna ngozi,Munavunja mifupa yao, na kuiponda-ponda,+Kama kitu chenye kupikwa ndani ya chungu,* kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.  4  Wakati huo watamuita Yehova awasaidie,Lakini hatawajibu. Ataficha uso wake wakati huo,+Kwa sababu ya matendo yao maovu.+  5  Yehova anasema hivi juu ya manabii wenye kupotosha watu wake,+Wenye kutangaza ‘Amani!’+ wakati wanatafuna kwa meno yao,+Lakini wenye kutangaza* vita juu ya mutu yeyote mwenye hatie kitu katika vinywa vyao:  6  ‘Mutakuwa na usiku;+ hakutakuwa maono;+Mutakuwa na giza tu, hamutafanya uaguzi. Jua litashuka juu ya manabii,Na muchana utageuka kuwa giza kwao.+  7  Watu wenye kuona maono watapatishwa haya,+Na waaguzi watakatishwa tumaini. Wote watafunika masharubu yao,*Kwa maana hakuna jibu kutoka kwa Mungu.’”  8  Lakini mimi, ninajaa nguvu kupitia roho ya Yehova,Na haki na uwezo,Ili nimuambie Yakobo uasi wake na Israeli zambi yake.  9  Tafazali musikie jambo hili, ninyi vichwa vya nyumba ya YakoboNa ninyi makamanda wa nyumba ya Israeli,+Wenye kuchukia haki na kupotosha mambo yote yenye kunyooka,+ 10  Wenye kujenga Sayuni kwa kumwanga damu na Yerusalemu kwa ukosefu wa haki.+ 11  Viongozi wake* wanapokea rushwa* ili kuhukumu,+Makuhani wake wanafundisha ili wapate malipo,+Na manabii wake wanafanya uaguzi ili wapate feza.+ Na hata hivyo wanamutegemea Yehova,* kwa kusema: “Je, Yehova haiko pamoja na sisi?+ Hakuna musiba wenye utatupata.”+ 12  Basi kwa sababu yenu,Sayuni italimwa kama shamba,Yerusalemu itakuwa marundo ya mabomoko,+Na mulima wa Nyumba* utakuwa kama mahali pa juu katika pori.*+

Maelezo ya Chini

Ao “chungu cha kupikia chenye mudomo mukubwa.”
Tnn., “kutakasa.”
Ao “watafunga vinywa vyao.” Masharubu ni nywele zenye kuota kwenye mudomo wa juu.
Tnn., “Vichwa vyake.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “wanasema kama wanamutegemea Yehova.”
Ao “mulima wa hekalu.”
Ao “kilima chenye miti.”