Mika 2:1-13

  • Ole wao wakandamizaji! (1-11)

  • Waisraeli wanakusanywa tena katika umoja (12, 13)

    • Inchi itajaa makelele ya watu (12)

2  “Ole wao wenye kupanga mambo yenye kuumiza,Wale wenye kupanga maovu katika vitanda vyao! Na wakati mwangaza wa asubui unatokea wanayatimiza,Kwa sababu wako na uwezo wa kufanya vile.+  2  Wanatamani mashamba na kuyanyanganya;+Pia nyumba, na kuzikamata;Na wanamunyanganya mutu nyumba yake kwa udanganyifu,+Na uriti wake.  3  Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninapanga kuletea familia hii musiba+ wenye hamutaepuka.*+ Hamutatembea tena kwa kiburi,+ kwa sababu ni wakati wa musiba.+  4  Siku hiyo watu watasema mezali juu yako,Na wataomboleza sana kwa ajili yako.+ Watasema: “Tumeharibiwa kabisa!+ Alifanya sehemu ya watu wangu iende katika mikono ya watu wengine—ona namna anaiondoa kwangu!+ Anagawia mashamba yetu mutu mwenye haiko muaminifu.”  5  Kwa hiyo hakuna mwenye atanyoosha kamba ya kupimia,Na kutugawia inchi kwa kura katika kutaniko la Yehova.  6  “Muache kuhubiri!” ni vile wanahubiri,“Hawapaswe kuhubiri mambo haya;Hatutafezeheshwa!”  7  Watu wanasema, Ee nyumba ya Yakobo: “Roho ya Yehova imeshindwa kuvumilia? Haya ndiyo matendo yake?” Je, maneno yangu hayaletee faida wenye kutembea kwa unyoofu?  8  Lakini hivi karibuni watu wangu wamesimama kama adui. Munaondoa waziwazi mapambo yenye kupendeza pamoja na* nguo,Juu ya watu wenye kupita bila wasiwasi, kama wale wenye kutoka kwenye vita.  9  Munaondoa wanamuke wa watu wangu katika nyumba zao za muzuri;Munakamata utukufu wangu kutoka kwa watoto wao milele. 10  Musimame na muende zenu, kwa sababu hapa haiko mahali pa kupumuzikia. Kwa sababu ya uchafu,+ kutakuwa uharibifu, uharibifu mukubwa.+ 11  Kama mutu anafuata upepo na udanganyifu, na kusema uongo huu: “Nitawahubiria juu ya divai na pombe,”Basi angekuwa tu muhubiri wa watu hawa!+ 12  Kwa kweli nitawakusanya ninyi wote, Ee Yakobo;Kwa kweli nitakusanya pamoja Waisraeli wote wenye kubakia.+ Nitawaunganisha, kama kondoo katika zizi,*Kama kundi katika malisho yake;+Kutakuwa makelele ya watu.’+ 13  Mwenye kutoboa tundu ataenda mbele yao;Na watatoboa tundu na kupita katika mulango mukubwa na kuenda inje kupitia mulango huo.+ Mufalme wao atapita mbele yao,Na Yehova atawaongoza.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “hamutaondoa shingo zenu.”
Ao pengine, “kutoka kwenye.”
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.