Mika 6:1-16
6 Tafazali, musikie jambo lenye Yehova anasema.
Musimame, mupeleke kesi ya hukumu mbele ya milima,Na vilima visikie sauti yenu.+
2 Musikie kesi ya hukumu ya Yehova, Enyi milima,Ninyi misingi imara ya dunia,+Kwa maana Yehova iko* na kesi ya hukumu pamoja na watu wake;Atabishana na Israeli:+
3 “Watu wangu, nimewafanya nini?
Nimewachokesha namna gani?+
Mushuhudie juu yangu.
4 Kwa maana niliwatosha katika inchi ya Misri,+Niliwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa;+Nilituma Musa, Haruni, na Miriamu mbele yenu.+
5 Watu wangu, tafazali, mukumbuke jambo lenye Mufalme Balaki wa Moabu alipendekeza,+Na jambo lenye Balaamu mwana wa Beori alimujibu+—Mambo yenye yalitokea kuanzia Shitimu+ mupaka Gilgali+—Ili mujue matendo yenye haki ya Yehova.”
6 Nitakuja na nini mbele ya Yehova?
Nitainama na nini mbele ya Mungu mwenye kuwa juu?
Je, nikuje mbele yake na matoleo mazima ya kuteketezwa,Na vitoto-dume vya ngombe vya mwaka mumoja?+
7 Je, Yehova atafurahia maelfu ya kondoo-dume,Na makumi ya maelfu ya mito ya mafuta?+
Je, nitoe mwana wangu muzaliwa wa kwanza kwa ajili ya uasi wangu,Uzao wa tumbo langu kwa ajili ya zambi yangu?*+
8 Ee mwanadamu, amekuambia mambo mema.
Na Yehova anataka* ufanye nini?
Anataka tu utende haki,*+ upende ushikamanifu,*+Na utembee kwa kiasi+ pamoja na Mungu wako!+
9 Sauti ya Yehova inaita muji;Watu wenye kuwa na hekima yenye kutenda wataogopa jina lako.
Musikilize fimbo na mwenye aliiweka.+
10 Je, hazina za uovu zingali katika nyumba ya muovuNa kipimo cha efa* chenye hakienee chenye kuchukiza?
11 Je, ninaweza kuwa na mwenendo safi* kama niko na mizani* ya uovu,Na mufuko wa majiwe ya kupimia ya udanganyifu?+
12 Kwa maana matajiri wake wamejaa jeuri,Na wakaaji wake wanasema uongo;+Ulimi wao unasema udanganyifu katika kinywa chao.+
13 “Kwa sababu hiyo, nitakuumiza kwa kukupiga,+Na kukufanya kuwa ukiwa kwa sababu ya zambi zako.
14 Utakula lakini hautashiba;Utakuwa bila kitu ndani yako.+
Vitu vyenye utaondoa, hautavibeba kwa usalama,Na vyenye unabeba, nitavitoa kwa upanga.
15 Utapanda mbegu, lakini hautavuna.
Utakanyanga zeituni, lakini hautatumia hayo mafuta;Na utatengeneza divai mupya, lakini hautaikunywa.+
16 Kwa sababu unafuata maagizo ya Omri na kazi yote ya nyumba ya Ahabu,+Na unafuata mashauri yao.
Ndiyo sababu nitakufanya kuwa kitu cha kuogopesha sanaNa wakaaji wake watakuwa kitu cha kupigia muluzi;+Na utabeba zarau ya vikundi vya watu.”+

