Mika 6:1-16

  • Kesi ya hukumu ya Mungu pamoja na Israeli (1-5)

  • Yehova anataka mutu afanye nini? (6-8)

    • Haki, ushikamanifu, kiasi (8)

  • Hatia na azabu ya Israeli (9-16)

6  Tafazali, musikie jambo lenye Yehova anasema. Musimame, mupeleke kesi ya hukumu mbele ya milima,Na vilima visikie sauti yenu.+  2  Musikie kesi ya hukumu ya Yehova, Enyi milima,Ninyi misingi imara ya dunia,+Kwa maana Yehova iko* na kesi ya hukumu pamoja na watu wake;Atabishana na Israeli:+  3  “Watu wangu, nimewafanya nini? Nimewachokesha namna gani?+ Mushuhudie juu yangu.  4  Kwa maana niliwatosha katika inchi ya Misri,+Niliwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa;+Nilituma Musa, Haruni, na Miriamu mbele yenu.+  5  Watu wangu, tafazali, mukumbuke jambo lenye Mufalme Balaki wa Moabu alipendekeza,+Na jambo lenye Balaamu mwana wa Beori alimujibu+—⁠Mambo yenye yalitokea kuanzia Shitimu+ mupaka Gilgali+Ili mujue matendo yenye haki ya Yehova.”  6  Nitakuja na nini mbele ya Yehova? Nitainama na nini mbele ya Mungu mwenye kuwa juu? Je, nikuje mbele yake na matoleo mazima ya kuteketezwa,Na vitoto-dume vya ngombe vya mwaka mumoja?+  7  Je, Yehova atafurahia maelfu ya kondoo-dume,Na makumi ya maelfu ya mito ya mafuta?+ Je, nitoe mwana wangu muzaliwa wa kwanza kwa ajili ya uasi wangu,Uzao wa tumbo langu kwa ajili ya zambi yangu?*+  8  Ee mwanadamu, amekuambia mambo mema. Na Yehova anataka* ufanye nini? Anataka tu utende haki,*+ upende ushikamanifu,*+Na utembee kwa kiasi+ pamoja na Mungu wako!+  9  Sauti ya Yehova inaita muji;Watu wenye kuwa na hekima yenye kutenda wataogopa jina lako. Musikilize fimbo na mwenye aliiweka.+ 10  Je, hazina za uovu zingali katika nyumba ya muovuNa kipimo cha efa* chenye hakienee chenye kuchukiza? 11  Je, ninaweza kuwa na mwenendo safi* kama niko na mizani* ya uovu,Na mufuko wa majiwe ya kupimia ya udanganyifu?+ 12  Kwa maana matajiri wake wamejaa jeuri,Na wakaaji wake wanasema uongo;+Ulimi wao unasema udanganyifu katika kinywa chao.+ 13  “Kwa sababu hiyo, nitakuumiza kwa kukupiga,+Na kukufanya kuwa ukiwa kwa sababu ya zambi zako. 14  Utakula lakini hautashiba;Utakuwa bila kitu ndani yako.+ Vitu vyenye utaondoa, hautavibeba kwa usalama,Na vyenye unabeba, nitavitoa kwa upanga. 15  Utapanda mbegu, lakini hautavuna. Utakanyanga zeituni, lakini hautatumia hayo mafuta;Na utatengeneza divai mupya, lakini hautaikunywa.+ 16  Kwa sababu unafuata maagizo ya Omri na kazi yote ya nyumba ya Ahabu,+Na unafuata mashauri yao. Ndiyo sababu nitakufanya kuwa kitu cha kuogopesha sanaNa wakaaji wake watakuwa kitu cha kupigia muluzi;+Na utabeba zarau ya vikundi vya watu.”+

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “zambi ya nafsi yangu?”
Ao “ukuwe mwenye fazili na mushikamanifu katika upendo wako.” Tnn., “upende upendo mushikamanifu.”
Ao “ukuwe mwenye haki; bila upendeleo.”
Ao “anaomba.”
Ao “Je, ninaweza kuwa bila kosa.”
Ao “kilo.”