Malaki 4:1-6

  • Kuja kwa Eliya mbele ya siku ya Yehova kufika (1-6)

    • “Jua la haki litaangaza” (2)

4  “Kwa maana angalia! siku inakuja, yenye kuwaka kama tanuru,+ na wale wote wenye kimbelembele na wote wenye kutenda uovu watakuwa kama majani yenye kukauka. Siku hiyo yenye kuja itawameza,” ni vile Yehova wa majeshi anasema, “na haitawaachia muzizi wala tawi. 2  Lakini ninyi wenye kuheshimia* jina langu, jua la haki litaangaza, litakuwa na uponyeshaji katika miali* yake; na mutaruka-ruka kama vitoto-dume vya ngombe vyenye kunenepa.” 3  “Na mutakanyangia waovu chini, kwa sababu watakuwa kama mavumbi chini ya vikanyangio vya miguu yenu siku yenye nitatenda,” ni vile Yehova wa majeshi anasema. 4  “Mukumbuke Sheria ya Musa mutumishi wangu, masharti na hukumu zenye niliamuru kwenye Mulima Horebu ili Israeli wote watii.+ 5  “Angalia! Ninatuma kwenu nabii Eliya+ mbele ya kuja kwa siku kubwa ya Yehova na yenye kuogopesha sana.+ 6  Na atarudisha mioyo ya baba kwa wana,+ na mioyo ya wana kwa baba, ili nisikuje kupiga dunia na kuiharibu.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “kuogopa.”
Tnn., “mabawa.”