Danieli 10:1-21

  • Danieli anatembelewa na mujumbe wa Mungu (1-21)

    • Mikaeli anamusaidia malaika (13)

10  Katika mwaka wa tatu (3) wa utawala wa Koreshi+ mufalme wa Uajemi, ufunuo ulitolewa kwa Danieli, mwenye aliitwa kwa jina Belteshaza;+ na ujumbe ulikuwa wa kweli, na ulihusu ugomvi mukubwa. Na akaelewa ujumbe huo na akapewa uelewaji juu ya mambo yenye alikuwa ameona. 2  Katika siku hizo, mimi Danieli, nilikuwa nimeomboleza+ kwa majuma tatu (3) kamili. 3  Sikukula chakula kizuri, na hakuna nyama wala divai yenye iliingia katika kinywa changu, na sikujipakaa mafuta kwa majuma tatu (3) kamili. 4  Katika siku ya makumi mbili na ine (24) ya mwezi wa kwanza, wakati nilikuwa pembeni ya ule muto mukubwa, Tigri,*+ 5  niliinua macho na nikaona mwanaume mwenye kuvaa nguo ya kitani,+ na kuzunguka kiuno chake kulikuwa mukaba* wa zahabu ya Ufazi. 6  Mwili wake ulikuwa kama krisolito,+ uso wake ulikuwa kama umeme wa radi, macho yake yalikuwa kama mienge yenye kuwaka moto, mikono yake na miguu yake ilionekana kama shaba yenye kungarishwa,+ na sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya watu wengi. 7  Mimi tu, Danieli, ndiye niliona maono hayo; watu wenye walikuwa pamoja na mimi hawakuona maono hayo.+ Lakini walishikwa na mutetemeko mukubwa, na wakakimbia na kujificha. 8  Kisha niliachwa peke yangu, na wakati niliona maono hayo makubwa, hakuna nguvu zenye zilibakia ndani yangu na sura yangu yenye kuheshimika ikaniacha na nguvu zote zikanitoka.+ 9  Kisha nikasikia sauti yake akisema; lakini wakati nilimusikia akisema, nilipatwa na usingizi muzito nikiwa nimelala uso chini.+ 10  Lakini kisha pale mukono ukanigusa,+ na ukanitikisa ili niinuke kwa mikono na magoti yangu. 11  Kisha akaniambia: “Ee Danieli, wewe mutu mwenye samani sana,*+ kaza uangalifu juu ya maneno yenye ninataka kukuambia. Sasa, simama mahali pako, kwa maana nimetumwa kwako.” Wakati aliniambia vile, nikasimama, nilikuwa ninatetemeka. 12  Kisha akaniambia: “Usiogope,+ Ee Danieli. Maneno yako yalisikiwa tangu siku ya kwanza yenye ulielekeza moyo wako kwenye uelewaji na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wako, na nimekuja kwa sababu ya maneno yako.+ 13  Lakini mukubwa+ wa ufalme wa Uajemi alisimama ili kunipinga kwa siku makumi mbili na moja (21). Lakini kisha pale Mikaeli,*+ mumoja kati ya wakubwa wa mbele,* alikuja kunisaidia; na nilibakia pale karibu na wafalme wa Uajemi. 14  Nimekuja ili kukufanya uelewe mambo yenye yatapata watu wako katika kipindi cha mwisho cha zile siku,+ kwa sababu hayo bado ni maono kwa ajili ya siku zenye zitakuja.”+ 15  Sasa wakati aliniambia maneno hayo, niliinamisha uso wangu chini na nikakuwa bubu. 16  Kisha mumoja mwenye kuonekana kama mwanadamu akagusa midomo yangu,+ na nikafungua kinywa changu na kumuambia ule mwenye alikuwa amesimama mbele yangu: “Bwana wangu, ninatetemeka kwa woga kwa sababu ya maono hayo, na sina nguvu.+ 17  Basi namna gani mutumishi wa bwana wangu anaweza kusema na bwana wangu?+ Kwa maana sasa sina nguvu, na hakuna pumuzi yenye kubakia ndani yangu.”+ 18  Ule mwenye kuonekana kama mwanadamu akanigusa tena na kunitia nguvu.+ 19  Kisha akasema: “Usiogope,+ Ee mutu mwenye samani sana.*+ Ukuwe na amani.+ Ukuwe na nguvu, ndiyo, ukuwe na nguvu.” Wakati alisema na mimi nilitiwa nguvu na nikasema: “Bwana wangu aseme, kwa maana umenitia nguvu.” 20  Kisha akasema: “Je, unajua sababu gani nimekuja kwako? Sasa nitarudia kupigana na mukubwa wa Uajemi.+ Wakati nitaondoka, mukubwa wa Ugiriki atakuja. 21  Hata hivyo, nitakuambia mambo yenye yameandikwa katika maandishi ya kweli. Hakuna mwenye iko* ananitegemeza kwa nguvu katika mambo haya isipokuwa Mikaeli,+ mukubwa wako.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Hidekeli.”
Ao “mushipi.”
Ao “mwenye kutamanika sana; mwenye kuheshimika sana.”
Ao “mukubwa wa cheo cha kwanza.”
Maana yake, “Ni Nani Mwenye Kuwa Kama Mungu?”
Ao “mwenye kutamanika sana; mwenye kuheshimika sana.”
Ao “eko.”