Ya Pili kwa Wakorinto 6:1-18
6 Kwa kuwa tunafanya kazi pamoja naye,+ tunawaomba ninyi pia musikubali fazili zenye hazistahiliwe za Mungu kisha mukose kusudi lake.+
2 Kwa maana anasema: “Katika wakati wenye kukubalika nilikusikia, na katika siku ya wokovu nilikusaidia.”+ Angalia! Sasa ndio wakati wenye kukubalika kabisa. Angalia! Sasa ndiyo siku ya wokovu.
3 Hatutoe sababu yoyote ya kukwaza kwa njia yoyote, ili kosa lolote lisipatikane katika utumishi wetu;+
4 lakini katika kila njia tunajipendekeza sisi wenyewe kuwa watumishi wa Mungu,+ kwa kuvumilia mambo mengi, kwa taabu, kwa nyakati za uhitaji, kwa magumu,+
5 kwa kupigwa, kwa kufungwa katika gereza,+ kwa machafuko, kwa kazi ya nguvu, kwa kukosa usingizi usiku, kwa nyakati za kukosa chakula;+
6 kwa utakaso, kwa ujuzi, kwa uvumilivu,+ kwa fazili,+ kwa roho takatifu, kwa upendo wenye hauna unafiki,+
7 kwa kusema maneno ya kweli, kwa nguvu za Mungu;+ kupitia silaha za haki+ katika mukono wa kuume* na wa kushoto,*
8 kupitia utukufu na haya, kupitia habari ya mubaya na habari ya muzuri. Tunaonwa kuwa wenye kudanganya lakini tunasema kweli,
9 kama wenye hawajulikane lakini tunatambuliwa, kama wenye kufa* lakini angalia! tunaishi,+ kama wenye kupewa azabu* lakini hatujatolewa kwenye kifo,+
10 kama wenye kuwa na huzuni lakini wenye kufurahi sikuzote, kama maskini lakini wenye kufanya watu wengi kuwa matajiri, kama wenye hawana kitu chochote na bado wenye kuwa na vitu vyote.+
11 Tumefungua kinywa chetu ili kusema* na ninyi, ninyi Wakorinto, na tumefungua wazi moyo wetu.
12 Hatufinywe katika* upendo wetu kuwaelekea ninyi,+ lakini ninyi mumefinywa katika upendo wenu wenye upole* kutuelekea sisi.
13 Kwa hiyo, kwa kujibu—ninasema kama na watoto wangu—ninyi pia mufungue mioyo yenu wazi.*+
14 Musifungwe nira yenye haiko sawa pamoja* na watu wenye hawako waamini.+ Kwa maana kuko uhusiano gani kati ya haki na uvunjaji wa sheria?+ Ao mwangaza uko na upatano gani na giza?+
15 Zaidi ya hayo, kuko upatano gani kati ya Kristo na Beliali?*+ Ao muamini* iko* na ushirika gani* na mutu mwenye haiko muamini?+
16 Na hekalu la Mungu liko na makubaliano gani na sanamu?+ Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu mwenye kuishi;+ kama vile Mungu alisema: “Mimi nitakaa katikati yao na kutembea katikati yao,+ na nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”+
17 “‘Kwa hiyo, mutoke katikati yao na mujitenge,’ ni vile Yehova* anasema, ‘na muache kugusa kitu kichafu’”;+ “‘na mimi nitawakaribisha ninyi ndani.’”+
18 “‘Na nitakuwa baba kwenu,+ na ninyi mutakuwa wana na mabinti kwangu,’+ ni vile Yehova,* Mweza-Yote anasema.”
Maelezo ya Chini
^ Pengine kwa ajili ya kujilinda.
^ Pengine kwa ajili ya kushambulia.
^ Ao “tunaonwa kuwa tunastahili kifo.”
^ Ao “wenye kutiwa nizamu.”
^ Ao “Tumesema waziwazi.”
^ Ao “upendo wenu mwororo.”
^ Ao “Hatukose nafasi kwa ajili ya.”
^ Ao “ninyi pia mupanuke.”
^ Ao “Musiunganishwe.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “muamini iko na fungu gani.”
^ Ao “mutu muaminifu.”
^ Linatokana na neno la Kiebrania lenye kumaanisha “Mutu Bure.” Linatumiwa ili kumutaja Shetani.
^ Angalia Nyongeza A5.
^ Angalia Nyongeza A5.

