Ya Pili kwa Wakorinto 6:1-18

  • Fazili za Mungu hazipaswe kutumiwa mubaya (1, 2)

  • Utumishi wa Paulo unaelezwa (3-13)

  • Musifungwe nira yenye haiko sawa (14-18)

6  Kwa kuwa tunafanya kazi pamoja naye,+ tunawaomba ninyi pia musikubali fazili zenye hazistahiliwe za Mungu kisha mukose kusudi lake.+ 2  Kwa maana anasema: “Katika wakati wenye kukubalika nilikusikia, na katika siku ya wokovu nilikusaidia.”+ Angalia! Sasa ndio wakati wenye kukubalika kabisa. Angalia! Sasa ndiyo siku ya wokovu. 3  Hatutoe sababu yoyote ya kukwaza kwa njia yoyote, ili kosa lolote lisipatikane katika utumishi wetu;+ 4  lakini katika kila njia tunajipendekeza sisi wenyewe kuwa watumishi wa Mungu,+ kwa kuvumilia mambo mengi, kwa taabu, kwa nyakati za uhitaji, kwa magumu,+ 5  kwa kupigwa, kwa kufungwa katika gereza,+ kwa machafuko, kwa kazi ya nguvu, kwa kukosa usingizi usiku, kwa nyakati za kukosa chakula;+ 6  kwa utakaso, kwa ujuzi, kwa uvumilivu,+ kwa fazili,+ kwa roho takatifu, kwa upendo wenye hauna unafiki,+ 7  kwa kusema maneno ya kweli, kwa nguvu za Mungu;+ kupitia silaha za haki+ katika mukono wa kuume* na wa kushoto,* 8  kupitia utukufu na haya, kupitia habari ya mubaya na habari ya muzuri. Tunaonwa kuwa wenye kudanganya lakini tunasema kweli, 9  kama wenye hawajulikane lakini tunatambuliwa, kama wenye kufa* lakini angalia! tunaishi,+ kama wenye kupewa azabu* lakini hatujatolewa kwenye kifo,+ 10  kama wenye kuwa na huzuni lakini wenye kufurahi sikuzote, kama maskini lakini wenye kufanya watu wengi kuwa matajiri, kama wenye hawana kitu chochote na bado wenye kuwa na vitu vyote.+ 11  Tumefungua kinywa chetu ili kusema* na ninyi, ninyi Wakorinto, na tumefungua wazi moyo wetu. 12  Hatufinywe katika* upendo wetu kuwaelekea ninyi,+ lakini ninyi mumefinywa katika upendo wenu wenye upole* kutuelekea sisi. 13  Kwa hiyo, kwa kujibu⁠—⁠ninasema kama na watoto wangu⁠—⁠ninyi pia mufungue mioyo yenu wazi.*+ 14  Musifungwe nira yenye haiko sawa pamoja* na watu wenye hawako waamini.+ Kwa maana kuko uhusiano gani kati ya haki na uvunjaji wa sheria?+ Ao mwangaza uko na upatano gani na giza?+ 15  Zaidi ya hayo, kuko upatano gani kati ya Kristo na Beliali?*+ Ao muamini* iko* na ushirika gani* na mutu mwenye haiko muamini?+ 16  Na hekalu la Mungu liko na makubaliano gani na sanamu?+ Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu mwenye kuishi;+ kama vile Mungu alisema: “Mimi nitakaa katikati yao na kutembea katikati yao,+ na nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”+ 17  “‘Kwa hiyo, mutoke katikati yao na mujitenge,’ ni vile Yehova* anasema, ‘na muache kugusa kitu kichafu’”;+ “‘na mimi nitawakaribisha ninyi ndani.’”+ 18  “‘Na nitakuwa baba kwenu,+ na ninyi mutakuwa wana na mabinti kwangu,’+ ni vile Yehova,* Mweza-Yote anasema.”

Maelezo ya Chini

Pengine kwa ajili ya kujilinda.
Pengine kwa ajili ya kushambulia.
Ao “tunaonwa kuwa tunastahili kifo.”
Ao “wenye kutiwa nizamu.”
Ao “Tumesema waziwazi.”
Ao “upendo wenu mwororo.”
Ao “Hatukose nafasi kwa ajili ya.”
Ao “ninyi pia mupanuke.”
Ao “Musiunganishwe.”
Ao “eko.”
Ao “muamini iko na fungu gani.”
Ao “mutu muaminifu.”
Linatokana na neno la Kiebrania lenye kumaanisha “Mutu Bure.” Linatumiwa ili kumutaja Shetani.