Ya Pili kwa Wakorinto 5:1-21
5 Kwa maana tunajua kwamba ikiwa nyumba yetu ya kidunia, hema hii, inabomolewa,*+ tutapata jengo kutoka kwa Mungu, nyumba yenye haikujengwa kwa mikono,+ nyumba ya milele mbinguni.
2 Kwa maana tunalia kwa maumivu kwelikweli katika nyumba hii,* na tunatamani sana kuvaa ile yetu* ya kutoka mbinguni,*+
3 ili wakati tutaivaa, tusipatikane tukiwa uchi.
4 Kwa kweli, sisi wenye tuko katika hema hii tunalia kwa maumivu, na tunalemewa, kwa sababu hatutaki kuvua hema hii, lakini tunataka kuvaa ile ingine,+ ili uzima umeze kile chenye kinaweza kufa.+
5 Sasa ule mwenye alitutayarisha kwa ajili ya jambo hili ni Mungu,+ mwenye alitupatia roho kama alama yenye kuhakikisha kile chenye kitakuja.*+
6 Basi sikuzote tuko na uhakika kabisa na tunajua kama wakati tungali na makao yetu katika mwili, hatuko mahali Bwana iko,*+
7 kwa maana tunatembea kwa imani, hapana kwa kuona.
8 Lakini tuko hakika kabisa na tungependa zaidi tusikuwe katika mwili na tufanye makao yetu pamoja na Bwana.+
9 Basi ikuwe tuko nyumbani pamoja naye ao hatuko pamoja naye, tunafanya kusudi letu likuwe kukubaliwa naye.
10 Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama* mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mumoja apate malipo kulingana na mambo yenye alitenda wakati alikuwa katika mwili, yakuwe ya muzuri ao ya mubaya.*+
11 Kwa hiyo, kwa kuwa tunajua kumuogopa Bwana, tunaendelea kushawishi watu, lakini tunajulikana muzuri* kwa Mungu. Hata hivyo, ninatumaini kama tunajulikana pia muzuri* kwa zamiri zenu.
12 Hatujipendekeze wenyewe tena kwenu, lakini tunawachochea ninyi kujisifu juu yetu, ili muweze kujibu wale wenye wanajisifu juu ya namna wanaonekana kwa inje+ lakini hapana juu ya mambo yenye kuwa katika moyo.
13 Kwa maana kama tulikuwa tumepoteza akili,+ ilikuwa kwa ajili ya Mungu; kama tuko na akili ya muzuri, ni kwa ajili yenu.
14 Kwa maana upendo wenye Kristo iko* nao unatulazimisha, kwa sababu tumefikia uamuzi huu, kwamba mutu mumoja alikufa kwa ajili ya watu wote;+ kwa hiyo basi, watu wote walikuwa wamekufa.
15 Na alikufa kwa ajili ya watu wote ili wale wenye wanaishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe,+ lakini kwa ajili ya ule mwenye alikufa kwa ajili yao na akafufuliwa.
16 Basi tangu sasa na kuendelea hatumujue mutu yeyote kulingana na mawazo ya kimwili.+ Hata kama wakati fulani tulimujua Kristo kulingana na mwili, kwa hakika hatumujue tena kwa njia hiyo.+
17 Kwa hiyo, kama mutu yeyote iko* katika umoja na Kristo, yeye ni kiumbe kipya;+ mambo ya zamani yalipita; angalia! mambo ya mupya yamekuja kuwa.
18 Lakini mambo yote yametoka kwa Mungu, mwenye alitupatanisha naye mwenyewe kupitia Kristo+ na kutupatia utumishi wa upatanisho,+
19 ni kusema, kwamba Mungu kupitia Kristo alikuwa anapatanisha ulimwengu kwake yeye mwenyewe,+ bila kuwahesabia makosa yao,+ na alitupatia ujumbe wa upatanisho.+
20 Kwa hiyo sisi ni mabalozi*+ pa nafasi ya Kristo,+ kama vile Mungu alikuwa anaomba kupitia sisi. Kama wenye kuwa pa nafasi ya Kristo, tunaomba: “Mupatanishwe pamoja na Mungu.”
21 Ule mwenye hakujua zambi+ alimufanya kuwa zambi* kwa ajili yetu, ili kupitia yeye tukuwe haki ya Mungu.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “inavunjwa.”
^ Ao “makao haya.”
^ Ao “kuvaa makao yetu yenye ni ya.”
^ Ao “makao yetu ya mbinguni.”
^ Ao “malipo ya kwanza; uhakikisho wa kile chenye kitakuja.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “kuonekana.”
^ Ao “maovu.”
^ Ao “tunaonekana.”
^ Ao “tunaonekana pia.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “ambassadeurs.”
^ Ao “toleo la zambi.”