Mambo ya Walawi 21:1-24

21  Na Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Ongea na makuhani, wana wa Haruni, nawe uwaambie, ‘Kwa ajili ya nafsi iliyokufa, mtu yeyote asijitie unajisi katikati ya watu wake.+  Lakini kwa ajili ya mtu mwenye uhusiano wa damu aliye karibu naye, kwa ajili ya mama yake na kwa ajili ya baba yake na kwa ajili ya mwana wake na kwa ajili ya binti yake na kwa ajili ya ndugu yake  na kwa ajili ya dada yake, bikira aliye karibu naye, ambaye hajawa wa mwanamume, kwa ajili yake anaweza kujitia unajisi.  Hatajitia unajisi kwa ajili ya mwanamke mwenye mume katikati ya watu wake ili kujitia unajisi.  Hawataweka upara juu ya vichwa+ vyao, na ncha ya ndevu zao hawatanyoa,+ na katika mwili wao hawatafanya mkato.+  Watakuwa watakatifu kwa Mungu wao,+ nao hawatalitia unajisi jina la Mungu wao,+ kwa sababu wao ndio wanaotoa matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto, mkate wa Mungu wao;+ nao watakuwa watakatifu.+  Kahaba+ au mwanamke aliyenajisiwa hawatamwoa; na mwanamke aliyetalikiwa+ kutoka kwa mume wake hawatamwoa,+ kwa sababu yeye ni mtakatifu kwa Mungu wake.  Basi utamtakasa,+ kwa sababu yeye ni mtu anayeutoa mkate wa Mungu wako. Atakuwa mtakatifu kwako,+ kwa sababu mimi Yehova, ninayewatakasa ninyi, mimi ni mtakatifu.+  “‘Sasa ikiwa binti ya kuhani atajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamtia unajisi baba yake. Binti huyo atateketezwa katika moto.+ 10  “‘Naye kuhani mkuu wa ndugu zake ambaye kichwa chake kimemiminiwa mafuta+ na ambaye mkono wake umejazwa nguvu ili kuvaa yale mavazi,+ hatakiacha kichwa chake bila kutunzwa,+ wala hatayararua mavazi yake.+ 11  Naye hatakuja mahali penye nafsi yoyote iliyokufa.+ Kwa ajili ya baba yake na mama yake hatajitia unajisi. 12  Pia hatatoka nje ya patakatifu wala kupatia unajisi patakatifu pa Mungu wake,+ kwa sababu ishara ya wakfu, yale mafuta ya Mungu wake yanayotumiwa kutia mafuta,+ yako juu yake. Mimi ni Yehova. 13  “‘Naye atamwoa mwanamke katika ubikira wake.+ 14  Na mwanamke mjane au aliyetalikiwa na yule aliyenajisiwa, kahaba, asimwoe yeyote kati ya hawa, lakini aoe bikira kutoka kwa watu wake awe mke wake. 15  Naye hatautia unajisi uzao wake kati ya watu wake,+ kwa sababu mimi ni Yehova ninayemtakasa.’”+ 16  Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 17  “Sema na Haruni, na kumwambia, ‘Mtu yeyote wa uzao wako katika vizazi vyao vyote ambaye ana kasoro+ asije karibu ili kuutoa mkate wa Mungu wake.+ 18  Ikiwa kuna mtu yeyote mwenye kasoro, asikaribie: mtu aliye kipofu au kilema au mwenye pua iliyokatika au mwenye kiungo kimoja kilicho kirefu mno,+ 19  au mtu aliyevunjika mguu au aliyevunjika mkono, 20  au mwenye kijongo au aliyekonda au mwenye ugonjwa wa macho au mwenye vigaga au mwenye mba au aliyevunjwa mapumbu yake.+ 21  Mtu yeyote wa uzao wa Haruni kuhani ambaye ana kasoro hatakaribia ili kutoa matoleo ya Yehova kwa njia ya moto.+ Kuna kasoro ndani yake. Hatakaribia ili kuutoa mkate wa Mungu wake.+ 22  Anaweza kula mkate wa Mungu wake kutoka kati ya vitu vitakatifu zaidi+ na kutoka kati ya vitu vitakatifu.+ 23  Hata hivyo, hatakaribia pazia,+ wala hatakaribia madhabahu,+ kwa sababu kuna kasoro ndani yake;+ naye hatapatia unajisi patakatifu pangu,+ kwa kuwa mimi ni Yehova ninayewatakasa wao.’”+ 24  Basi Musa akasema na Haruni na wanawe na wana wote wa Israeli.

Maelezo ya Chini