Mambo ya Walawi 11:1-47
11 Na Yehova akasema na Musa na Haruni, akiwaambia:
2 “Semeni na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Hiki ndicho kiumbe hai ambacho mnaweza kula+ kati ya wanyama wote walio kwenye uso wa dunia:
3 Kila kiumbe kati ya wanyama chenye ukwato uliopasuka na chenye mwanya kwenye ukwato na kinachocheua, hicho ndicho mnachoweza kula.+
4 “‘Ila hiki ndicho ambacho hamtakula kati ya wacheuaji na wenye ukwato uliopasuka: ngamia, kwa sababu ni mcheuaji lakini hana ukwato uliopasuka. Huyo si safi kwenu.+
5 Pia wibari,+ kwa sababu ni mcheuaji lakini hana ukwato uliopasuka. Huyo si safi kwenu.
6 Pia sungura,+ kwa sababu ni mcheuaji lakini hana ukwato uliopasuka. Huyo si safi kwenu.
7 Pia nguruwe,+ kwa sababu ana ukwato uliopasuka naye ana mwanya kwenye ukwato, lakini yeye mwenyewe hacheui. Huyo si safi kwenu.
8 Msile yoyote kati ya nyama zao, wala msiguse mizoga yao.+ Hao si safi kwenu.+
9 “‘Hiki ndicho mnachoweza kula kati ya kila kitu kilicho majini:+ Kila kitu chenye mapezi na magamba+ majini, katika bahari na katika mito, hivyo mnaweza kula.
10 Na kila kitu katika bahari na katika mito ambacho hakina mapezi na magamba, kati ya kila kiumbe kinachozaana kwa wingi cha majini na kati ya kila nafsi hai iliyo majini, hivyo ni vitu vyenye kuchukiza kwenu.
11 Naam, vitakuwa chukizo kwenu. Msile yoyote kati ya nyama zao,+ nanyi mtaichukia mizoga yao.
12 Kila kitu majini ambacho hakina mapezi na magamba ni chukizo kwenu.
13 “‘Navyo hivi ndivyo mtakavyovichukia kati ya viumbe vinavyoruka.+ Visiliwe. Hivyo ni chukizo: tai+ na furukombe na tai-mzoga mweusi,
14 na mwewe mwekundu na mwewe mweusi+ kulingana na aina yake,
15 na kila kunguru+ kulingana na aina yake,
16 na mbuni+ na bundi na shakwe na kipanga kulingana na aina yake,
17 na bundi mdogo na mnandi na bundi mwenye masikio marefu,+
18 na bata-maji na mwari na tai-mzoga,+
19 na korongo, kulastara kulingana na aina yake na hudihudi na popo.+
20 Kila kiumbe chenye mabawa kinachozaana kwa wingi ambacho hutembea kwa miguu minne ni chukizo kwenu.+
21 “‘Ila hiki ndicho mnachoweza kula kati ya viumbe vyote vyenye mabawa vinavyozaana kwa wingi ambavyo hutembea kwa miguu minne, vile vyenye miguu ya kuruka juu ya miguu yao, ili kuruka nayo juu ya dunia.
22 Hawa ndio mnaoweza kula kati yao: nzige mwenye kuhama+ kulingana na aina yake, na nzige anayeweza kuliwa+ kulingana na aina yake, na nyenje kulingana na aina yake na panzi+ kulingana na aina yake.
23 Na kila kiumbe kingine chenye mabawa kinachozaana kwa wingi chenye miguu minne ni chukizo+ kwenu.
24 Basi kupitia kwao mtajifanya wenyewe msiwe safi. Kila mtu anayegusa mizoga yao atakuwa asiye safi mpaka jioni.+
25 Na kila mtu anayebeba wowote kati ya mizoga yao atayafua+ mavazi yake, naye atakuwa asiye safi mpaka jioni.
26 “‘Na mnyama yeyote ambaye ana ukwato uliopasuka lakini hana mwanya wala si mcheuaji, hao si safi kwenu. Kila mtu anayewagusa hao atakuwa si safi.+
27 Na kila kiumbe kinachotembea kwa miguu yenye makucha kati ya viumbe hai vinavyoenda kwa miguu minne, hao si safi kwenu. Kila mtu anayeigusa mizoga yao atakuwa asiye safi mpaka jioni.
28 Naye anayeibeba mizoga+ yao atafua mavazi yake,+ naye atakuwa asiye safi mpaka jioni. Hao si safi kwenu.
29 “‘Nacho hiki ndicho kisicho safi kwenu kati ya viumbe vinavyozaana kwa wingi ambavyo hujaa duniani:+ fuko na panya anayeruka+ na mjusi kulingana na aina yake,
30 na mjusi kafiri na mjusi mkubwa na mjusi wa majini na mjusi wa mchangani na kinyonga.
31 Hao si safi kwenu kati ya viumbe vyote vinavyozaana kwa wingi.+ Kila mtu anayevigusa viumbe hivyo vikiwa vimekufa atakuwa asiye safi mpaka jioni.+
32 “‘Sasa chochote ambacho yeyote kati yao ataangukia akiwa amekufa kitakuwa kisicho safi, kiwe ni chombo cha mbao+ au nguo au ngozi+ au nguo ya gunia.+ Chombo chochote ambacho hutumiwa kwa njia fulani kitatiwa katika maji, nacho kitakuwa kisicho safi mpaka jioni halafu kitakuwa safi.
33 Nacho chombo chochote cha udongo+ ambacho yeyote kati yao ataanguka ndani yake, chochote kilicho ndani yake kitakuwa kisicho safi, nanyi mtakivunja.+
34 Chakula cha namna yoyote ambacho huenda kikaliwa kitakachopata maji kutoka katika chombo hicho kitakuwa kisicho safi, na kinywaji chochote ambacho kinaweza kunywewa katika chombo chochote kitakuwa kisicho safi.
35 Na kila kitu ambacho juu yake huenda wowote kati ya mizoga yao ukaangukia kitakuwa kisicho safi. Iwe ni jiko au kinara cha mtungi, kitavunjwa. Vitu hivyo si safi, navyo vitakuwa si safi kwenu.
36 Ila tu bubujiko na shimo la maji yaliyozuiliwa ndiyo yatakayoendelea kuwa safi, lakini mtu yeyote anayegusa mizoga yao atakuwa asiye safi.
37 Na wowote wa mizoga ukianguka juu ya mbegu yoyote ya mmea wa kupandwa, ni safi.
38 Lakini ikiwa maji yatatiwa juu ya mbegu na kitu fulani cha mizoga yao kianguke juu yake, si safi kwenu.
39 “‘Sasa, ikiwa mnyama yeyote aliye wenu kwa ajili ya chakula atakufa, mtu anayeugusa mzoga wake atakuwa asiye safi mpaka jioni.+
40 Naye anayekula+ sehemu yoyote ya mzoga wake atayafua mavazi yake, naye atakuwa asiye safi mpaka jioni; naye anayeubeba mzoga wake atayafua mavazi yake, naye atakuwa asiye safi mpaka jioni.
41 Na kila kiumbe kinachozaana kwa wingi ambacho kinajaa duniani ni chukizo.+ Kisiliwe.
42 Nacho kiumbe chochote ambacho hutembea kwa tumbo+ na kiumbe chochote ambacho hutembea kwa miguu yote minne au hesabu yoyote kubwa ya miguu ya viumbe vyote vinavyozaana kwa wingi ambavyo vinajaa duniani, msivile, kwa sababu hivyo ni chukizo.+
43 Msifanye nafsi zenu ziwe zenye kuchukiza kutokana na kiumbe chochote kinachozaana kwa wingi ambacho kinajaa, wala msijifanye kuwa wasio safi kutokana nao na kupata kuwa wasio safi kutokana nao.+
44 Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wenu;+ nanyi mtajitakasa wenyewe nanyi mtakuwa watakatifu,+ kwa sababu mimi ni mtakatifu.+ Kwa hiyo msifanye nafsi zenu kuwa zisizo safi kutokana na kiumbe chochote kinachozaana kwa wingi ambacho hutembea juu ya dunia.
45 Kwa maana mimi ni Yehova anayewaongoza ninyi kutoka katika nchi ya Misri ili kujionyesha kuwa Mungu kwenu;+ nanyi mtakuwa watakatifu,+ kwa sababu mimi ni mtakatifu.+
46 “‘Hiyo ndiyo sheria juu ya mnyama na kiumbe kinachoruka na kila nafsi hai ambayo hutembea majini+ na kuhusu kila nafsi inayojazana duniani,
47 ili kufanya tofauti+ kati ya kisicho safi na kilicho safi na kati ya kiumbe hai kinachoweza kuliwa na kiumbe hai kisichopasa kuliwa.’”