Mambo ya Walawi 5:1-19
5 “‘Ikiwa nafsi+ inatenda dhambi kwa kuwa amesikia laana+ ya hadharani naye ni shahidi au ameiona au amepata kujua juu yake, asipotoa habari,+ ndipo atakapojibu kwa sababu ya kosa lake.
2 “‘Au nafsi inapogusa kitu kisicho safi, iwe ni mzoga wa mnyama-mwitu asiye safi au mzoga wa mnyama wa kufugwa asiye safi au mzoga wa kiumbe kinachozaana kwa wingi kisicho safi,+ ingawa ulikuwa umefichwa machoni pake,+ bado yeye si safi naye amekuwa na hatia.+
3 Au ikiwa anagusa uchafu wa mwanadamu kuhusiana na uchafu+ wowote wake ambao huenda ukamfanya asiwe safi, ingawa ulikuwa umefichwa machoni pake, na hata hivyo yeye mwenyewe amepata kujua, basi amekuwa na hatia.
4 “‘Au ikiwa nafsi inaapa kiasi cha kusema kwa midomo yake bila kufikiri+ kwamba itende uovu+ au kufanya mema kuhusiana na jambo lolote ambalo huenda mtu huyo akasema bila kufikiri katika ahadi yenye kiapo,+ ingawa lilikuwa limefichwa machoni pake, na hata hivyo yeye mwenyewe amepata kulijua, basi amekuwa na hatia kuhusiana na moja kati ya mambo hayo.
5 “‘Na itakuwa kwamba ikiwa anakuwa na hatia kwa sababu ya moja kati ya mambo hayo, ndipo atakapoungama+ jinsi ambavyo ametenda dhambi.
6 Naye ataleta toleo lake la hatia+ mbele za Yehova kwa ajili ya dhambi yake ambayo ametenda, yaani, wa kike kutoka katika kundi, mwana-kondoo jike au mwana-mbuzi jike,+ kwa ajili ya toleo la dhambi; naye kuhani atamfanyia upatanisho kwa ajili ya dhambi yake.+
7 “‘Hata hivyo, ikiwa hana uwezo wa kutoa kondoo,+ basi atamletea Yehova njiwa-tetere+ wawili au hua wawili wachanga wawe toleo lake la hatia+ kwa ajili ya dhambi ambayo ametenda, mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi na mmoja kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.
8 Naye atawaleta kwa kuhani, ambaye kwanza atamtoa yule wa toleo la dhambi na kukongonyoa+ kichwa chake upande wa mbele wa shingo yake, lakini asikikate kabisa.
9 Naye atatapanya sehemu ya damu ya toleo la dhambi kando ya madhabahu, lakini damu inayobaki itaachwa itiririke kwenye msingi wa madhabahu.+ Hilo ni toleo la dhambi.
10 Na yule mwingine atamtoa kuwa toleo la kuteketezwa kulingana na utaratibu wa kawaida;+ naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake kwa sababu ya dhambi yake ambayo ametenda, naye atasamehewa.+
11 “‘Sasa ikiwa hana uwezo+ wa kutoa njiwa-tetere wawili au hua wawili wachanga, basi ataleta sehemu ya kumi ya efa+ ya unga laini kwa ajili ya toleo la dhambi, uwe toleo lake la dhambi. Naye hatatia mafuta+ juu yake wala hataweka ubani juu yake, kwa maana ni toleo la dhambi.+
12 Naye atauleta kwa kuhani, naye kuhani atachukua kipimo cha mkono mmoja uwe kumbukumbu+ lake naye ataufukiza kwenye madhabahu juu ya toleo la Yehova linalotolewa kwa njia ya moto.+ Hilo ni toleo la dhambi.+
13 Naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake kwa sababu ya dhambi yake ambayo ametenda, yoyote kati ya dhambi hizo, naye atasamehewa; nao utakuwa wa kuhani+ sawa na toleo la nafaka.’”
14 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia:
15 “Ikiwa nafsi inajiendesha kwa njia isiyo ya uaminifu kwa kutenda dhambi bila kukusudia juu ya mambo matakatifu ya Yehova,+ basi atamtolea Yehova kondoo-dume ambaye hana kasoro kutoka katika kundi, awe toleo lake la hatia,+ kulingana na ile thamani iliyokadiriwa ya shekeli za fedha,+ kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, kuwa toleo la hatia.
16 Naye atalipa kwa ajili ya dhambi ambayo amepatendea mahali patakatifu naye ataongeza juu yake sehemu yake ya tano,+ naye atampa kuhani, ili kuhani afanye upatanisho+ kwa ajili yake kwa kutumia yule kondoo-dume wa toleo la hatia, naye atasamehewa.+
17 “Na ikiwa nafsi inatenda dhambi kwa kuwa anafanya moja kati ya mambo ambayo Yehova anaamuru yasifanywe, ingawa hakujua,+ hata hivyo amekuwa na hatia na lazima atajibu kwa sababu ya kosa lake.+
18 Naye atamleta kondoo-dume ambaye hana kasoro kutoka katika kundi kulingana na thamani iliyokadiriwa, kwa ajili ya toleo la hatia,+ kwa kuhani; naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake kwa sababu ya kosa alilofanya bila kukusudia, ingawa yeye mwenyewe hakujua, naye atasamehewa.+
19 Hilo ni toleo la hatia.+ Hakika amekuwa na hatia dhidi ya Yehova.”