Mambo ya Walawi 5:1-19

5  “‘Ikiwa nafsi+ inatenda dhambi kwa kuwa amesikia laana+ ya hadharani naye ni shahidi au ameiona au amepata kujua juu yake, asipotoa habari,+ ndipo atakapojibu kwa sababu ya kosa lake.  “‘Au nafsi inapogusa kitu kisicho safi, iwe ni mzoga wa mnyama-mwitu asiye safi au mzoga wa mnyama wa kufugwa asiye safi au mzoga wa kiumbe kinachozaana kwa wingi kisicho safi,+ ingawa ulikuwa umefichwa machoni pake,+ bado yeye si safi naye amekuwa na hatia.+  Au ikiwa anagusa uchafu wa mwanadamu kuhusiana na uchafu+ wowote wake ambao huenda ukamfanya asiwe safi, ingawa ulikuwa umefichwa machoni pake, na hata hivyo yeye mwenyewe amepata kujua, basi amekuwa na hatia.  “‘Au ikiwa nafsi inaapa kiasi cha kusema kwa midomo yake bila kufikiri+ kwamba itende uovu+ au kufanya mema kuhusiana na jambo lolote ambalo huenda mtu huyo akasema bila kufikiri katika ahadi yenye kiapo,+ ingawa lilikuwa limefichwa machoni pake, na hata hivyo yeye mwenyewe amepata kulijua, basi amekuwa na hatia kuhusiana na moja kati ya mambo hayo.  “‘Na itakuwa kwamba ikiwa anakuwa na hatia kwa sababu ya moja kati ya mambo hayo, ndipo atakapoungama+ jinsi ambavyo ametenda dhambi.  Naye ataleta toleo lake la hatia+ mbele za Yehova kwa ajili ya dhambi yake ambayo ametenda, yaani, wa kike kutoka katika kundi, mwana-kondoo jike au mwana-mbuzi jike,+ kwa ajili ya toleo la dhambi; naye kuhani atamfanyia upatanisho kwa ajili ya dhambi yake.+  “‘Hata hivyo, ikiwa hana uwezo wa kutoa kondoo,+ basi atamletea Yehova njiwa-tetere+ wawili au hua wawili wachanga wawe toleo lake la hatia+ kwa ajili ya dhambi ambayo ametenda, mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi na mmoja kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.  Naye atawaleta kwa kuhani, ambaye kwanza atamtoa yule wa toleo la dhambi na kukongonyoa+ kichwa chake upande wa mbele wa shingo yake, lakini asikikate kabisa.  Naye atatapanya sehemu ya damu ya toleo la dhambi kando ya madhabahu, lakini damu inayobaki itaachwa itiririke kwenye msingi wa madhabahu.+ Hilo ni toleo la dhambi. 10  Na yule mwingine atamtoa kuwa toleo la kuteketezwa kulingana na utaratibu wa kawaida;+ naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake kwa sababu ya dhambi yake ambayo ametenda, naye atasamehewa.+ 11  “‘Sasa ikiwa hana uwezo+ wa kutoa njiwa-tetere wawili au hua wawili wachanga, basi ataleta sehemu ya kumi ya efa+ ya unga laini kwa ajili ya toleo la dhambi, uwe toleo lake la dhambi. Naye hatatia mafuta+ juu yake wala hataweka ubani juu yake, kwa maana ni toleo la dhambi.+ 12  Naye atauleta kwa kuhani, naye kuhani atachukua kipimo cha mkono mmoja uwe kumbukumbu+ lake naye ataufukiza kwenye madhabahu juu ya toleo la Yehova linalotolewa kwa njia ya moto.+ Hilo ni toleo la dhambi.+ 13  Naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake kwa sababu ya dhambi yake ambayo ametenda, yoyote kati ya dhambi hizo, naye atasamehewa; nao utakuwa wa kuhani+ sawa na toleo la nafaka.’” 14  Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 15  “Ikiwa nafsi inajiendesha kwa njia isiyo ya uaminifu kwa kutenda dhambi bila kukusudia juu ya mambo matakatifu ya Yehova,+ basi atamtolea Yehova kondoo-dume ambaye hana kasoro kutoka katika kundi, awe toleo lake la hatia,+ kulingana na ile thamani iliyokadiriwa ya shekeli za fedha,+ kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, kuwa toleo la hatia. 16  Naye atalipa kwa ajili ya dhambi ambayo amepatendea mahali patakatifu naye ataongeza juu yake sehemu yake ya tano,+ naye atampa kuhani, ili kuhani afanye upatanisho+ kwa ajili yake kwa kutumia yule kondoo-dume wa toleo la hatia, naye atasamehewa.+ 17  “Na ikiwa nafsi inatenda dhambi kwa kuwa anafanya moja kati ya mambo ambayo Yehova anaamuru yasifanywe, ingawa hakujua,+ hata hivyo amekuwa na hatia na lazima atajibu kwa sababu ya kosa lake.+ 18  Naye atamleta kondoo-dume ambaye hana kasoro kutoka katika kundi kulingana na thamani iliyokadiriwa, kwa ajili ya toleo la hatia,+ kwa kuhani; naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake kwa sababu ya kosa alilofanya bila kukusudia, ingawa yeye mwenyewe hakujua, naye atasamehewa.+ 19  Hilo ni toleo la hatia.+ Hakika amekuwa na hatia dhidi ya Yehova.”

Maelezo ya Chini