Mambo ya Walawi 8:1-36
8 Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia:
2 “Mchukue Haruni na wanawe pamoja naye+ na yale mavazi+ na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta+ na yule ng’ombe-dume wa toleo la dhambi+ na wale kondoo-dume wawili na kile kikapu cha keki zisizo na chachu,+
3 nawe ukutanishe kusanyiko lote+ kwenye mwingilio wa hema la mkutano.”+
4 Ndipo Musa akafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru, nalo kusanyiko likakutanika kwenye mwingilio+ wa hema la mkutano.
5 Sasa Musa akaliambia kusanyiko: “Hili ndilo jambo ambalo Yehova ametoa amri lifanywe.”+
6 Basi Musa akawaleta karibu Haruni na wanawe na kuwaosha+ kwa maji.+
7 Baada ya hayo akamvika kanzu+ na kumfunga ukumbuu+ na kumvika lile koti lisilo na mikono+ na kumvika efodi+ na kumfunga kwa mshipi+ wa ile efodi na kuufunga imara kwa mshipi huo.
8 Kisha akamvika kile kifuko cha kifuani+ na kutia Urimu na Thumimu+ ndani ya kifuko hicho.
9 Kisha akakiweka kilemba+ juu ya kichwa chake na kuweka juu ya kile kilemba upande wa mbele bamba linalong’aa la dhahabu, ile ishara takatifu ya wakfu,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
10 Sasa Musa akachukua yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta, akaitia mafuta ile maskani+ na vyote vilivyokuwa ndani yake na kuvitakasa.
11 Kisha akatapanya sehemu yake mara saba kwenye madhabahu na kuitia mafuta madhabahu+ na vyombo vyake vyote na ile beseni na kinara chake ili kuvitakasa.
12 Mwishowe akamimina sehemu ya mafuta hayo ya kutia mafuta juu ya kichwa cha Haruni na kumtia mafuta ili kumtakasa.+
13 Halafu Musa akawaleta karibu wana wa Haruni+ na kuwavika kanzu na kuwafunga ukumbuu+ na kuwafunga valio la kichwani,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
14 Halafu akamwongoza ng’ombe-dume+ wa toleo la dhambi na Haruni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa+ cha yule ng’ombe wa toleo la dhambi.
15 Naye Musa akamchinja+ na kuichukua damu+ yake na kuitia kwa kidole chake juu ya pembe za madhabahu kuizunguka pande zote na kuitakasa madhabahu kutokana na dhambi, lakini ile damu nyingine akaimimina kwenye msingi wa madhabahu, apate kuitakasa ili afanye upatanisho+ juu yake.
16 Kisha akachukua mafuta yote yaliyokuwa kwenye matumbo, na kipasho cha ini na figo mbili na mafuta yake naye Musa akayafukiza juu ya madhabahu.+
17 Naye akamteketeza kwa moto yule ng’ombe-dume pamoja na ngozi yake na nyama yake na mavi yake nje ya kambi,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
18 Sasa akamleta karibu kondoo-dume wa toleo la kuteketezwa, naye Haruni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.+
19 Kisha Musa akamchinja na kuinyunyiza damu yake juu ya madhabahu kuizunguka pande zote.+
20 Naye akamkata kondoo huyo vipande-vipande,+ naye Musa akakifukiza kichwa na vile vipande na yale mafuta.
21 Naye akaosha matumbo na miguu kwa maji, na Musa akamfukiza kondoo mzima juu ya madhabahu.+ Lilikuwa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya harufu ya kutuliza.+ Lilikuwa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
22 Kisha akamleta karibu kondoo-dume wa pili, yule kondoo wa kuweka rasmi,+ naye Haruni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.
23 Baada ya hayo Musa akamchinja na kuchukua sehemu ya damu yake na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la Haruni na kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.+
24 Kisha Musa akawaleta karibu wana wa Haruni na kutia sehemu ya damu kwenye ncha ya sikio lao la kuume na kwenye kidole gumba chao cha mkono wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha mguu wao wa kuume; lakini Musa akainyunyiza ile damu iliyobaki juu ya madhabahu kuizunguka pande zote.+
25 Kisha akachukua yale mafuta na ule mkia mnono na mafuta yote yaliyokuwa kwenye matumbo,+ na kipasho cha ini na zile figo mbili na mafuta yake na mguu wa kuume.+
26 Na kutoka katika kikapu cha keki zisizo na chachu kilichokuwa mbele za Yehova akachukua keki moja ya mviringo isiyo na chachu+ na keki moja ya mviringo ya mkate uliotiwa mafuta+ na mkate mmoja mwembamba.+ Halafu akaviweka juu ya vile vipande vyenye mafuta na ule mguu wa kuume.
27 Baada ya hayo akaviweka vyote hivyo juu ya mikono ya Haruni na mikono ya wanawe na kuanza kuvitikisa huku na huku vikiwa toleo la kutikisa mbele za Yehova.+
28 Kisha Musa akavichukua kutoka mikononi mwao na kuvifukiza kwenye madhabahu juu ya lile toleo la kuteketezwa.+ Hivyo vilikuwa dhabihu ya kuweka rasmi+ kwa ajili ya harufu ya kutuliza.+ Lilikuwa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.+
29 Naye Musa akachukua kidari+ na kukitikisa huku na huku kikiwa toleo la kutikisa mbele za Yehova.+ Kutoka katika yule kondoo-dume wa kuweka rasmi kikawa fungu+ la Musa, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
30 Baada ya hayo Musa akachukua sehemu ya mafuta yanayotumiwa kutia mafuta+ na sehemu ya damu iliyokuwa juu ya madhabahu na kuvitapanya juu ya Haruni na mavazi yake na juu ya wanawe na mavazi ya wanawe. Basi akamtakasa+ Haruni na mavazi yake na wanawe+ na mavazi ya wanawe.
31 Kisha Musa akamwambia Haruni na wanawe: “Itokoseni+ nyama kwenye mwingilio wa hema la mkutano, na hapo ndipo mtakapoila+ na mkate ulio katika kile kikapu cha kuweka rasmi, kama vile nilivyopewa amri, kusema, ‘Haruni na wanawe wataila.’
32 Na kinachobaki cha ile nyama na ule mkate mtakiteketeza kwa moto.+
33 Nanyi msitoke nje ya mwingilio wa hema la mkutano kwa siku saba,+ mpaka siku ya kutimia kwa siku za kuwekwa kwenu rasmi, kwa sababu itachukua siku saba kuujaza mkono wenu nguvu.+
34 Kama vile ambavyo imefanywa leo, Yehova ameamuru ifanywe hivyo ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.+
35 Nanyi mtakaa katika mwingilio wa hema la mkutano mchana na usiku kwa siku saba,+ nanyi mtashika kesha la lazima la Yehova,+ msije mkafa; kwa maana hivyo ndivyo nimeamriwa.”
36 Naye Haruni na wanawe wakafanya mambo yote ambayo Yehova alikuwa amewaamuru kupitia Musa.