Mambo ya Walawi 27:1-34
27 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia:
2 “Sema na wana wa Israeli, nawe uwaambie, ‘Ikiwa mtu atamwekea Yehova nadhiri ya pekee+ kwa kumtolea Yehova nafsi kulingana na thamani iliyokadiriwa,
3 nayo thamani iliyokadiriwa iwe ya mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 mpaka miaka 60, basi thamani iliyokadiriwa itakuwa shekeli 50 za fedha kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
4 Lakini ikiwa ni mwanamke, basi thamani iliyokadiriwa itakuwa shekeli 30.
5 Na ikiwa umri ni kuanzia miaka 5 mpaka miaka 20, basi thamani iliyokadiriwa ya mwanamume itakuwa shekeli 20 na kwa ajili ya mwanamke itakuwa shekeli 10.
6 Na ikiwa umri ni kuanzia mwezi mmoja mpaka miaka mitano, basi thamani iliyokadiriwa ya mwanamume itakuwa shekeli tano+ za fedha na kwa ajili ya mwanamke thamani iliyokadiriwa itakuwa shekeli tatu za fedha.
7 “‘Sasa ikiwa umri ni kuanzia miaka 60 na zaidi, ikiwa ni mwanamume, basi thamani iliyokadiriwa itakuwa shekeli 15 na kwa ajili ya mwanamke itakuwa shekeli 10.
8 Lakini ikiwa amekuwa maskini mno kwa ajili ya ile thamani iliyokadiriwa,+ ndipo atakapomsimamisha mtu huyo mbele ya kuhani, naye kuhani atakadiria thamani yake.+ Kulingana na anachoweza+ yule mwenye kuweka nadhiri, kuhani atakadiria thamani yake.
9 “‘Na ikiwa ni mnyama kama yule ambaye mtu humtolea Yehova, kila kitu ambacho atampa Yehova kitakuwa kitu kitakatifu.+
10 Hataweka kingine mahali pake, wala kukibadili chema kwa kibaya au kibaya kwa chema. Lakini ikiwa ni lazima akibadili, mnyama kwa mnyama, basi lazima hicho chenyewe na kile kitakachobadilishwa nacho vitakuwa kitu kitakatifu.
11 Na ikiwa ni mnyama yeyote asiye safi+ kama yule ambaye mtu hawezi kumtoa katika toleo kwa Yehova,+ basi lazima amsimamishe mnyama huyo mbele ya kuhani.+
12 Naye kuhani atamkadiria thamani yake iwapo ni mzuri au mbaya. Kulingana na thamani iliyokadiriwa na kuhani,+ ndivyo atakavyokuwa.
13 Lakini ikiwa anataka kumnunua, basi atatoa sehemu yake ya tano+ kwa kuongezea ile thamani iliyokadiriwa.
14 “‘Sasa ikiwa mtu ataitakasa nyumba yake iwe kitu kitakatifu kwa Yehova, basi kuhani atakadiria thamani yake iwapo ni nzuri au mbaya.+ Kulingana na kadirio la kuhani ambalo ataikadiria, ndivyo itakavyogharimu.
15 Lakini ikiwa mtakasaji anataka kuinunua nyumba yake, basi atatoa sehemu ya tano ya thamani iliyokadiriwa kwa kuongezea thamani hiyo;+ nayo itakuwa yake.
16 “‘Na ikiwa ni sehemu ya shamba lililo mali yake+ ambalo mtu anataka kulitakasa kwa Yehova, basi thamani itakadiriwa kulingana na mbegu yake: ikiwa ni homeri+ moja ya mbegu ya shayiri, basi kwa shekeli 50 za fedha.
17 Ikiwa atalitakasa shamba lake kuanzia mwaka wa Yubile+ na kuendelea, litagharimu kulingana na thamani iliyokadiriwa.
18 Na ikiwa atalitakasa shamba lake baada ya Yubile, basi kuhani atafanya hesabu ya bei kulingana na miaka inayobaki mpaka mwaka wa Yubile inayofuata, na kiasi fulani kitapunguzwa kutoka katika thamani iliyokadiriwa.+
19 Lakini ikiwa mtakasaji wake atalinunua shamba hilo, basi atatoa sehemu ya tano ya pesa ya thamani iliyokadiriwa kwa kuongezea thamani hiyo, nalo litaendelea kuwa lake.+
20 Sasa ikiwa hatalinunua shamba hilo lakini shamba hilo liuziwe mtu mwingine, halitanunuliwa na kurudishwa tena.
21 Na wakati shamba hilo litakapotoka katika Yubile litakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova, kama shamba lililotolewa wakfu.+ Kuhani atalimiliki.+
22 “‘Na ikiwa atamtakasia Yehova shamba alilolinunua ambalo si sehemu ya shamba lililo mali yake,+
23 basi kuhani atamfanyia hesabu ya kadirio la thamani mpaka mwaka wa Yubile, naye atatoa thamani iliyokadiriwa katika siku hiyo.+ Ni kitu kitakatifu kwa Yehova.+
24 Katika mwaka wa Yubile shamba hilo litarudi kwa mtu aliyelinunua kutoka kwake, kwa mtu ambaye shamba hilo ni mali yake.+
25 “‘Sasa kila thamani itakadiriwa kwa shekeli ya mahali patakatifu. Shekeli itakuwa gera 20.+
26 “‘Ila mzaliwa wa kwanza kati ya wanyama, anayezaliwa akiwa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya Yehova,+ mtu yeyote asimtakase. Awe ni ng’ombe au kondoo, ni wa Yehova.+
27 Na ikiwa ni mmoja wa wanyama wasio safi+ naye ni lazima amkomboe kulingana na thamani iliyokadiriwa, basi atatoa sehemu yake ya tano kwa kuongezea juu yake.+ Lakini ikiwa hatanunuliwa, basi atauzwa kulingana na thamani iliyokadiriwa.
28 “‘Ila tu hakuna kitu chochote kilichotolewa wakfu ambacho huenda mtu akamtolea Yehova kwa ajili ya uharibifu+ kutoka katikati ya vyote vilivyo vyake, iwe ni kutoka kwa wanadamu au wanyama au kutoka katika shamba lililo mali yake, kitakachouzwa, wala hakuna aina yoyote ya kitu kilichotolewa ambacho kitanunuliwa.+ Hicho ni kitu kitakatifu zaidi kwa Yehova.
29 Hakuna mtu yeyote ambaye huenda akawa ametengwa kwa ajili ya kuharibiwa kutoka kati ya wanadamu atakayekombolewa.+ Lazima auawe.+
30 “‘Na kila sehemu ya kumi+ ya nchi, kutoka katika mbegu ya nchi na tunda la mti, ni ya Yehova. Ni kitu kitakatifu kwa Yehova.
31 Na ikiwa mtu anataka kununua sehemu yake yoyote ya kumi, atatoa sehemu yake ya tano kwa kuongezea juu ya hiyo.+
32 Na kwa kila sehemu ya kumi ya mifugo na ya kundi, kila kitu ambacho hupita chini ya bakora,+ kichwa cha kumi kitakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova.
33 Hatamchunguza iwapo ni mzuri au mbaya, wala hatambadilisha. Lakini akimbadilisha, hicho chenyewe na kile kilichobadilishwa nacho vitakuwa kitu kitakatifu.+ Hatanunuliwa.’”
34 Hizo ndizo amri+ ambazo Yehova alimpa Musa kuwa amri kwa wana wa Israeli katika Mlima Sinai.+