Mambo ya Walawi 12:1-8
12 Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia:
2 “Sema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Ikiwa mwanamke atachukua mimba+ na kuzaa mtoto wa kiume, atakuwa asiye safi kwa siku saba; kama vile katika siku za uchafu wakati anapokuwa na hedhi atakuwa asiye safi.+
3 Na siku ya nane ngozi ya govi la mtoto huyo itatahiriwa.+
4 Kwa siku 33 zaidi mwanamke huyo atakaa katika damu ya utakaso. Asiguse kitu chochote kilicho kitakatifu, wala asiingie mahali patakatifu mpaka kutimia kwa siku za utakaso wake.+
5 “‘Sasa, ikiwa atazaa mtoto wa kike, basi atakuwa asiye safi kwa siku 14, kama vile wakati wa kuwa na hedhi. Kwa siku 66 zaidi atakaa katika damu ya utakaso wake.
6 Kisha zitakapotimia siku za utakaso wake kwa ajili ya mwana au binti ataleta mwana-kondoo dume katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa+ na hua mchanga au njiwa-tetere+ kwa ajili ya toleo la dhambi kwenye mwingilio wa hema la mkutano kwa kuhani.
7 Naye atalitoa mbele za Yehova na kufanya upatanisho kwa ajili ya mwanamke huyo, naye atakuwa safi kutokana na chemchemi ya damu yake.+ Hiyo ndiyo sheria juu ya mwanamke anayezaa mtoto wa kiume au wa kike.
8 Lakini ikiwa hana uwezo wa kutosha wa kutoa kondoo, basi atachukua njiwa-tetere wawili au hua wachanga wawili,+ mmoja kwa ajili ya toleo la kuteketezwa na yule mwingine kwa ajili ya toleo la dhambi, naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake, naye atakuwa safi.’”