Mambo ya Walawi 12:1-8

12  Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia:  “Sema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Ikiwa mwanamke atachukua mimba+ na kuzaa mtoto wa kiume, atakuwa asiye safi kwa siku saba; kama vile katika siku za uchafu wakati anapokuwa na hedhi atakuwa asiye safi.+  Na siku ya nane ngozi ya govi la mtoto huyo itatahiriwa.+  Kwa siku 33 zaidi mwanamke huyo atakaa katika damu ya utakaso. Asiguse kitu chochote kilicho kitakatifu, wala asiingie mahali patakatifu mpaka kutimia kwa siku za utakaso wake.+  “‘Sasa, ikiwa atazaa mtoto wa kike, basi atakuwa asiye safi kwa siku 14, kama vile wakati wa kuwa na hedhi. Kwa siku 66 zaidi atakaa katika damu ya utakaso wake.  Kisha zitakapotimia siku za utakaso wake kwa ajili ya mwana au binti ataleta mwana-kondoo dume katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa+ na hua mchanga au njiwa-tetere+ kwa ajili ya toleo la dhambi kwenye mwingilio wa hema la mkutano kwa kuhani.  Naye atalitoa mbele za Yehova na kufanya upatanisho kwa ajili ya mwanamke huyo, naye atakuwa safi kutokana na chemchemi ya damu yake.+ Hiyo ndiyo sheria juu ya mwanamke anayezaa mtoto wa kiume au wa kike.  Lakini ikiwa hana uwezo wa kutosha wa kutoa kondoo, basi atachukua njiwa-tetere wawili au hua wachanga wawili,+ mmoja kwa ajili ya toleo la kuteketezwa na yule mwingine kwa ajili ya toleo la dhambi, naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake, naye atakuwa safi.’”

Maelezo ya Chini