Mambo ya Walawi 18:1-30

18  Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia:  “Sema na wana wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Mimi ni Yehova Mungu wenu.+  Jinsi inavyofanya nchi ya Misri ambamo mlikaa, msifanye;+ na jinsi inavyofanya nchi ya Kanaani, ambamo nitawaleta, msifanye;+ na katika sheria zao msitembee.  Maamuzi yangu ya hukumu+ mtayatenda, na sheria+ zangu mtazishika ili kutembea katika hizo.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.  Nanyi mtazishika sheria zangu na maamuzi yangu ya hukumu, ambazo ikiwa mtu atazifanya, yeye pia ataishi kwa hizo.+ Mimi ni Yehova.+  “‘Yeyote kati yenu asimkaribie mtu yeyote wa jamaa yake, wa kimwili, wa karibu ili kufunua uchi.+ Mimi ni Yehova.  Uchi wa baba yako+ na uchi wa mama yako usiufunue. Yeye ni mama yako. Usiufunue uchi wake.  “‘Uchi wa mke wa baba yako usiufunue.+ Ni uchi wa baba yako.  “‘Nao uchi wa dada yako, binti ya baba yako au binti ya mama yako, awe amezaliwa katika nyumba hiyo hiyo au amezaliwa nje, usiufunue uchi wao.+ 10  “‘Nao uchi wa binti ya mwana wako au binti ya binti yako, usiufunue uchi wao, kwa sababu wao ni uchi wako. 11  “‘Nao uchi wa binti ya mke wa baba yako, uzao wa baba yako, kwa kuwa yeye ni dada yako, usiufunue uchi wake. 12  “‘Uchi wa dada ya baba yako usiufunue. Yeye ana uhusiano wa damu na baba yako.+ 13  “‘Uchi wa dada ya mama yako usiufunue, kwa sababu yeye ana uhusiano wa damu na mama yako. 14  “‘Uchi wa ndugu ya baba yako usiufunue. Usimkaribie mke wake. Yeye ni shangazi yako.+ 15  “‘Uchi wa binti-mkwe+ wako usiufunue. Yeye ni mke wa mwana wako. Usiufunue uchi wake. 16  “‘Uchi wa mke wa ndugu yako+ usiufunue. Ni uchi wa ndugu yako. 17  “‘Uchi wa mwanamke na binti yake usiufunue.+ Binti ya mwana wake na binti ya binti yake usimchukue ili kuufunua uchi wake. Wao wana uhusiano wa damu. Ni mwenendo mpotovu.+ 18  “‘Nawe usimchukue mwanamke pamoja na dada yake awe mshindani+ ili kuufunua uchi wake, yaani, pamoja naye akiwa angali hai. 19  “‘Nawe usimkaribie mwanamke wakati wa hedhi+ ya uchafu wake ili kuufunua uchi wake.+ 20  “‘Nawe usimpe mke wa mwenzako shahawa inayokutoka awe asiye safi kutokana nayo.+ 21  “‘Nawe usiuruhusu uzao wako wowote utolewe+ kwa Moleki.+ Usilitie unajisi+ jina la Mungu wako kwa njia hiyo. Mimi ni Yehova.+ 22  “‘Nawe usilale na mwanamume+ kama vile unavyolala na mwanamke.+ Ni jambo lenye kuchukiza. 23  “‘Nawe usimpe mnyama yeyote shahawa+ yako awe asiye safi kutokana nayo, na mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kuungana naye.+ Ni kuvunja jambo lililo la asili. 24  “‘Msijifanye wenyewe kuwa wasio safi kwa lolote la mambo hayo, kwa sababu kwa mambo yote hayo mataifa ninayoyafukuza kutoka mbele yenu yamejifanya yenyewe kuwa si safi.+ 25  Kwa hiyo nchi si safi, nami nitaleta adhabu kwa ajili ya kosa lake juu yake, nayo nchi itawatapika wakaaji wake.+ 26  Nanyi mtazishika sheria zangu na maamuzi yangu ya hukumu,+ nanyi msifanye lolote la mambo hayo yenye kuchukiza, iwe ni mwenyeji au mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni katikati yenu.+ 27  Kwa maana mambo yote hayo yenye kuchukiza, watu wa nchi waliokuwa mbele yenu wameyafanya,+ hivi kwamba nchi si safi. 28  Ndipo nchi haitawatapika ninyi kwa sababu ya kuitia kwenu unajisi kama vile itakavyoyatapika mataifa yaliyokuwa mbele yenu.+ 29  Ikiwa mtu yeyote atafanya lolote la mambo yote hayo yenye kuchukiza, basi nafsi zinazoyafanya zitakatiliwa mbali kutoka katikati ya watu wao.+ 30  Nanyi mtatimiza wajibu wenu kwangu ili kutoendeleza yoyote kati ya desturi hizo zenye kuchukiza ambazo zimeendelezwa mbele yenu,+ ili msijifanye kuwa wasio safi kutokana nazo. Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”

Maelezo ya Chini