Mambo ya Walawi 10:1-20

10  Baadaye Nadabu na Abihu,+ wana wa Haruni, wakachukua na kuleta kila mmoja wao chetezo+ chake na kutia moto ndani yake na kutia uvumba+ juu yake, nao wakaanza kumtolea Yehova moto haramu,+ ambao hakuwa amewaamuru.  Ndipo moto ukatoka mbele za Yehova na kuwateketeza,+ hivi kwamba wakafa mbele za Yehova.+  Ndipo Musa akamwambia Haruni: “Hivi ndivyo Yehova amesema, ‘Na nitakaswe+ kati ya wale walio karibu nami,+ nami nitukuzwe mbele ya uso wa watu wote.’”+ Naye Haruni akakaa kimya.  Basi Musa akamwita Mishaeli na Elsafani, wana wa Uzieli,+ ndugu ya baba ya Haruni, akawaambia: “Njooni karibu, wachukueni ndugu zenu kutoka mbele ya mahali patakatifu mpaka nje ya kambi.”+  Basi wakakaribia na kuwachukua wakiwa na kanzu zao mpaka nje ya kambi, kama vile Musa alivyokuwa amesema.  Kwa hiyo Musa akamwambia Haruni na Eleazari na Ithamari wale wanawe wengine: “Msiache vichwa vyenu vikose kuwa nadhifu,+ wala msiyararue mavazi yenu, msije mkafa wala asije akalikasirikia kusanyiko lote;+ lakini ndugu zenu wa nyumba yote ya Israeli watalilia kule kuteketeza, ambako Yehova aliteketeza.  Nanyi msitoke katika mwingilio wa hema la mkutano msije mkafa,+ kwa sababu mafuta ya Yehova yanayotumiwa kutia mafuta yako juu yenu.”+ Basi wakafanya kulingana na neno la Musa.  Naye Yehova akasema na Haruni, na kumwambia:  “Usinywe divai wala kileo,+ wewe na wanao pamoja nawe, mnapoingia ndani ya hema la mkutano, msije mkafa. Hiyo ni sheria mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili ya vizazi vyenu, 10  na ili kufanya tofauti kati ya kitu kitakatifu na kile najisi na kati ya kitu kisicho safi na kilicho safi,+ 11  na ili kuwafundisha wana wa Israeli+ masharti yote ambayo Yehova amesema kupitia Musa.” 12  Ndipo Musa akasema na Haruni na wanawe waliobaki, yaani, Eleazari na Ithamari: “Chukueni toleo la nafaka+ lililobaki kutoka katika matoleo ya Yehova yaliyotolewa kwa njia ya moto na mle pasipo kutiwa chachu karibu na madhabahu, kwa sababu hilo ni kitu kitakatifu zaidi.+ 13  Nanyi mtakula katika mahali patakatifu,+ kwa maana ndilo posho lenu na posho la wana wenu kutoka kwa matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto; kwa maana hivyo ndivyo nimeamriwa. 14  Nanyi mtakula kile kidari cha toleo la kutikisa+ na ule mguu wa lile fungu takatifu+ katika mahali safi, wewe na wanao na binti zako pamoja nawe,+ kwa sababu vimetolewa kuwa posho lako na posho la wanao kutoka katika dhabihu za ushirika za wana wa Israeli. 15  Watauleta mguu wa lile fungu takatifu na kile kidari cha toleo la kutikisa+ pamoja na matoleo yanayotolewa kwa njia ya moto, ya vile vipande vyenye mafuta, ili kutikisa toleo la kutikisa huku na huku, mbele za Yehova; nalo litakuwa posho+ mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili yako na wanao pamoja nawe, kama vile Yehova ameamuru.” 16  Naye Musa akamtafuta sana huyo mbuzi wa toleo la dhambi,+ na, tazama! alikuwa ameteketezwa kabisa. Basi akawaka hasira kuwaelekea Eleazari na Ithamari, wana wa Haruni waliokuwa wamebaki, na kusema: 17  “Kwa nini hamkula lile toleo la dhambi katika mahali palipo patakatifu,+ kwa kuwa ni kitu kitakatifu zaidi naye amewapa ninyi mpate kujibu kwa ajili ya kosa la kusanyiko ili kufanya upatanisho kwa ajili yao mbele za Yehova?+ 18  Tazama! damu yake haijaletwa ndani katika mahali patakatifu.+ Mlipaswa kula toleo hilo katika mahali patakatifu, kama vile nilivyokuwa nimeamriwa.”+ 19  Basi Haruni akasema na Musa: “Tazama! Leo wametoa toleo lao la dhambi na toleo lao la kuteketezwa mbele za Yehova,+ kisha mambo haya yameanza kunipata; na ikiwa ningekuwa nimekula toleo la dhambi leo, je, jambo hilo lingekuwa jema machoni pa Yehova?”+ 20  Musa aliposikia hilo, ndipo hilo likawa jema machoni pake.

Maelezo ya Chini