Mambo ya Walawi 24:1-23
24 Na Yehova akasema na Musa, na kumwambia:
2 “Waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta safi ya zeituni zilizopondwa kwa ajili ya mwanga,+ ili kuiwasha taa daima.+
3 Nje ya pazia la Ushuhuda katika hema la mkutano Haruni ataiweka kwa utaratibu toka jioni mpaka asubuhi mbele za Yehova daima. Ni sheria mpaka wakati usio na kipimo katika vizazi vyenu vyote.
4 Juu ya kinara cha taa+ cha dhahabu safi ataziweka taa+ kwa utaratibu mbele za Yehova daima.+
5 “Nawe utachukua unga laini na kuuoka uwe keki kumi na mbili za mviringo. Kila keki itafanyizwa kwa sehemu mbili za efa.
6 Nawe utaziweka katika vikundi viwili vya tabaka, sita katika kikundi kimoja cha tabaka,+ juu ya meza ya dhahabu safi mbele za Yehova.+
7 Nawe utaweka ubani safi juu ya kila kikundi cha tabaka, nao utakuwa mkate kwa ajili ya kumbukumbu,+ toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.
8 Katika siku moja ya sabato baada ya nyingine atauweka kwa utaratibu mbele za Yehova daima.+ Ni agano pamoja na wana wa Israeli mpaka wakati usio na kipimo.
9 Nao utakuwa wa Haruni na wa wanawe,+ nao wataula katika mahali patakatifu,+ kwa sababu ni kitu kitakatifu zaidi kwa ajili yake kutoka kwa matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto, kama sharti mpaka wakati usio na kipimo.”
10 Sasa mwana wa mwanamke Mwisraeli, ambaye, hata hivyo, alikuwa mwana wa mwanamume Mmisri,+ akatoka kwenda katikati ya wana wa Israeli, naye yule mwana wa mwanamke Mwisraeli akaanza kupambana+ na mwanamume Mwisraeli kambini.
11 Naye yule mwana wa mwanamke Mwisraeli akaanza kulitukana lile Jina+ na kulilaani.+ Basi wakamleta kwa Musa.+ Basi jina la mama yake lilikuwa Shelomithi, binti ya Dibri wa kabila la Dani.
12 Ndipo wakamtia kifungoni+ mpaka kuwe na tangazo lililo wazi kulingana na neno la Yehova.+
13 Na Yehova akasema na Musa, na kumwambia:
14 “Mtoe nje ya kambi+ yule aliyelaani; na wale wote waliomsikia wataweka mikono+ yao juu ya kichwa chake, nalo kusanyiko lote litampiga kwa mawe.+
15 Nawe utasema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Ikiwa mtu yeyote atamlaani Mungu wake, basi atajibu kwa dhambi yake.
16 Kwa hiyo lazima yule mtukanaji wa jina la Yehova auawe.+ Lazima kusanyiko lote limpige kwa mawe. Mkaaji mgeni hali kadhalika mwenyeji atauawa kwa kulitukana lile Jina.+
17 “‘Na ikiwa mtu ataipiga nafsi yoyote ya mwanadamu kiasi cha kuiua, lazima atauawa.+
18 Naye mwenye kuipiga nafsi ya mnyama wa kufugwa kiasi cha kuiua atalipa, nafsi kwa nafsi.+
19 Na ikiwa mtu atamtia mwenzake kasoro, basi kama vile tu ambavyo yeye amefanya, ndivyo atakavyofanywa.+
20 Mfupa uliovunjika kwa mfupa uliovunjika, jicho kwa jicho, jino kwa jino; aina ileile ya kasoro ambayo huenda akamtia mtu, hiyo ndiyo atakayotiwa.+
21 Naye mwenye kumpiga mnyama kiasi cha kumuua+ atalipa,+ lakini mwenye kumpiga mwanadamu kiasi cha kumuua atauawa.+
22 “‘Uamuzi mmoja wa hukumu utatumika kwenu. Mkaaji mgeni atakuwa sawa na mwenyeji,+ kwa sababu mimi ni Yehova Mungu wenu.’”+
23 Kisha Musa akasema na wana wa Israeli, nao wakamtoa nje ya kambi yule aliyekuwa amelaani, wakampiga kwa mawe.+ Basi wana wa Israeli wakafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.