Ya Kwanza kwa Wakorinto 7:1-40

  • Shauri kwa wenye hawajaoa ao kuolewa (1-16)

  • Bakia katika hali yenye uliitwa ndani (17-24)

  • Wenye hawajaoa ao kuolewa, na wajane (25-40)

    • Faida za kubakia bila kuoa ao kuolewa (32-35)

    • Kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu” (39)

7  Sasa juu ya mambo yenye muliandika kuyahusu, ni muzuri mwanaume asiguse* mwanamuke;  lakini kwa sababu ya kuenea kwa uasherati,* kila mwanaume akuwe na bibi yake mwenyewe+ na kila mwanamuke akuwe na bwana yake mwenyewe.+  Bwana amupatie bibi yake haki yake, na bibi pia amufanyie bwana yake vilevile.+  Bibi hana mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe, lakini bwana yake ndiye iko* na mamlaka hayo; vilevile, bwana hana mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe, lakini bibi yake ndiye iko* na mamlaka hayo.  Musikuwe munaimana isipokuwa kwa mapatano kwa ajili ya wakati wenye uliwekwa, ili mukuwe na wakati kwa ajili ya sala na mukuje pamoja tena, ili Shetani asiendelee kuwajaribu kwa sababu munakosa kujizuia.  Hata hivyo, ninasema hilo ili kutoa ruhusa, lakini sitoe amri.  Lakini ningependa watu wote wakuwe kama vile mimi niko. Hata hivyo, kila mumoja iko* na zawadi yake mwenyewe+ kutoka kwa Mungu, mumoja kwa njia hii, mwingine kwa njia ile.  Sasa ninaambia wale wenye hawajaoa ao kuolewa, na wajane, kwamba ni muzuri wabakie kama vile mimi niko.+  Lakini kama hawawezi kujizuia, basi waoe ao waolewe, kwa maana ni muzuri kuoa ao kuolewa kuliko kuwaka tamaa.+ 10  Kwa watu wenye wameoa ao kuolewa ninatoa maagizo, haiko mimi lakini Bwana, kwamba bibi asitengane na bwana yake.+ 11  Lakini kama anatengana naye, abakie bila kuolewa, kama haiko vile, asikilizane tena na bwana yake; na bwana asimuache bibi yake.+ 12  Lakini kwa wale wengine ninasema, ndiyo, mimi, haiko Bwana:+ Kama ndugu yeyote iko* na bibi mwenye haamini na bibi huyo anakubali kubakia pamoja naye, basi asimuache; 13  na kama mwanamuke iko* na bwana mwenye haamini na bwana huyo anakubali kubakia pamoja naye, basi asimuache bwana yake. 14  Kwa maana bwana mwenye haamini anatakaswa kwa sababu ya bibi yake, na bibi mwenye haamini anatakaswa kwa sababu ya ule ndugu; tofauti na hilo, watoto wenu hawangekuwa safi, lakini sasa wao ni watakatifu. 15  Lakini kama ule mwenye haamini anaamua kuondoka,* basi aondoke; ndugu ao dada haiko mwenye kufungwa chini ya hali kama hizo, lakini Mungu amewaita ninyi kwenye amani.+ 16  Kwa maana, wewe bibi, unajua namna gani kama utamuokoa bwana yako?+ Ao, wewe bwana, unajua namna gani kama utamuokoa bibi yako? 17  Lakini, kama vile Yehova* amepatia kila mumoja fungu lake, kila mumoja ajiendeshe kama vile Mungu alimuita.+ Na ni vile ninatoa muongozo huo katika makutaniko yote. 18  Je, mutu ­yeyote aliitwa ­akiwa ­amekwisha kutahiriwa?+ Basi asibadilishe kutahiriwa kwake. Je, mutu yeyote ameitwa akiwa hajatahiriwa? Basi asitahiriwe.+ 19  Kutahiriwa hakumaanishe kitu, na kutokutahiriwa hakumaanishe kitu;+ jambo la maana ni kushika amri za Mungu.+ 20  Katika hali yoyote yenye kila mumoja aliitwa, abakie katika hali hiyo.+ 21  Je, uliitwa wakati ulikuwa ungali mutumwa? Usiache jambo hilo likuhangaishe;+ lakini kama unaweza kuwa huru, basi tumia nafasi hiyo. 22  Kwa maana kila mutu mwenye aliitwa katika Bwana akiwa mutumwa ni mutu wa Bwana mwenye aliwekwa huru;+ vilevile kila mutu mwenye aliitwa akiwa huru ni mutumwa wa Kristo. 23  Mulinunuliwa kwa bei;+ muache kuwa watumwa wa wanadamu. 24  Ndugu, katika hali yoyote yenye kila mumoja aliitwa, abakie katika hali hiyo mbele ya Mungu. 25  Sasa kuhusu mabikira,* sina amri kutoka kwa Bwana, lakini ninatoa mawazo yangu+ nikiwa mutu mwenye alionyeshwa rehema na Bwana kuwa muaminifu. 26  Kwa hiyo, ninawaza ni muzuri sana kwa mutu kuendelea kuwa vile iko* kwa sababu ya magumu ya sasa. 27  Je, umefungwa kwa bibi? Acha kutafuta kufunguliwa.+ Je, umewekwa huru kutoka kwa bibi? Acha kutafuta bibi. 28  Lakini hata kama unaoa, hautakuwa umefanya zambi. Na kama bikira anaolewa, mutu huyo hatakuwa amefanya zambi. Hata hivyo, wale wenye wanaoa ao kuolewa watakuwa na taabu katika mwili wao. Lakini ninajaribu kuwaepusha ninyi. 29  Zaidi ya hayo, ninasema hivi, ndugu, wakati wenye unabakia umepunguka.+ Tangu sasa wale wenye kuwa na bibi wakuwe kama wenye hawana, 30  na wale wenye wanalia wakuwe kama wale wenye hawalie, na wale wenye wanafurahi wakuwe kama wale wenye hawafurahi, na wale wenye wananunua wakuwe kama wale wenye hawana kitu, 31  na wale wenye wanatumia ulimwengu wakuwe kama wale wenye hawautumie kwa ukamili; kwa maana tamasha* ya ulimwengu huu inabadilika. 32  Kwa kweli, ninataka musihangaike. Mwanaume mwenye hajaoa anahangaikia mambo ya Bwana, namna anaweza kumupendeza Bwana. 33  Lakini mwanaume mwenye ameoa anahangaikia mambo ya ulimwengu,+ namna ­anaweza kumupendeza bibi yake, 34  na amegawanyika. Zaidi ya hayo, mwanamuke mwenye hajaolewa, na vilevile bikira, anahangaikia mambo ya Bwana,+ ili akuwe mutakatifu katika mwili wake na pia katika roho yake. Hata hivyo, mwanamuke mwenye ameolewa anahangaikia mambo ya ulimwengu, namna anaweza kumupendeza bwana yake. 35  Lakini ninasema vile kwa faida yenu wenyewe, hapana ili kuwazuia ninyi,* lakini ili kuwachochea kufanya jambo lenye linafaa na kujitoa kwa Bwana sikuzote kwa moyo wote bila kukengeushwa fikira. 36  Lakini kama mutu yeyote anawaza kwamba anajiendesha mubaya kwa kubakia bila kuoa ao kuolewa,* na kama amepita mwanzo wa kipindi cha ujana, basi inapaswa kuwa hivi: Afanye vile anataka; hafanye zambi. Aoe ao aolewe.+ 37  Hata hivyo, kama mutu yeyote ametulia katika moyo wake na hajisikie kuwa analazimika, lakini iko* na mamlaka juu ya nia yake mwenyewe na amefanya uamuzi katika moyo wake kubakia bila kuoa ao kuolewa,* atafanya muzuri.+ 38  Vilevile mutu yeyote mwenye anaoa ao anaolewa* anafanya muzuri, lakini mutu yeyote mwenye haoe ao haolewe atafanya muzuri zaidi.+ 39  Bibi amefungwa wakati wote wenye bwana yake angali muzima.+ Lakini kama bwana yake analala usingizi katika kifo, iko* huru kuolewa na mutu yeyote mwenye anataka, katika Bwana tu.+ 40  Lakini kulingana na mawazo yangu, mwanamuke huyo atakuwa na furaha zaidi kama anabakia vile iko;* na hakika ninafikiri mimi pia niko na roho ya Mungu.

Maelezo ya Chini

Ni kusema, asifanye ngono na.
Neno la Kigiriki por·neiʹa. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “kujitenga.”
Ao “wale wenye hawajaoa ao kuolewa hata siku moja.”
Ao “eko.”
Tamasha ni maonyesho ya michezo fulani.
Tnn., “kuwafunga kwa kamba.”
Ao “kuelekea ubikira wake.”
Ao “eko.”
Ao “kuchunga ubikira wake.”
Ao “anatoa ubikira wake katika ndoa.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”