Ya Kwanza kwa Timoteo 4:1-16

  • Onyo juu ya mafundisho ya pepo wachafu (1-5)

  • Namna ya kuwa mutumishi muzuri wa Kristo (6-10)

    • Tofauti kati ya mazoezi ya mwili na ushikamanifu kwa Mungu (8)

  • Ukuwe muangalifu kuhusu kufundisha kwako (11-16)

4  Lakini, neno lenye liliongozwa na roho linasema* wazi kama nyakati zenye kuja, watu fulani wataacha imani na kusikiliza maneno yenye kupotosha yenye kuongozwa na roho*+ na mafundisho ya pepo wachafu,  na hii ni kwa sababu ya uongo wenye kusemwa na wanafiki,+ wenye zamiri zao zimekuwa kama kovu lenye lilifanywa kwa chuma cha moto cha kutilia alama.  Wanakataza kuoa ao kuolewa+ na wanaamuru watu wasikule vyakula+ vyenye Mungu aliumba ili vikuliwe+ kwa kutoa shukrani na watu wenye kuwa na imani+ na wenye wanajua kweli kwa njia yenye haina makosa.*  Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri,+ na hakuna kitu chenye kinapaswa kukataliwa+ kama kinakuliwa kwa kutoa shukrani,  kwa maana kinatakaswa kupitia neno la Mungu na sala yenye kutolewa juu yake.  Kwa kupatia ndugu shauri hili, utakuwa mutumishi muzuri wa Kristo Yesu, mwenye kukulishwa maneno ya imani na fundisho la muzuri lenye umefuata kwa ukaribu.+  Lakini kataa hadisi za uongo zenye zinamuvunjia Mungu heshima,+ kama zile zenye kuelezwa na wanamuke wazee. Kwa upande mwingine, ujizoeze ukiwa na kusudi la ushikamanifu kwa Mungu.  Kwa maana mazoezi ya mwili ni yenye faida kidogo, lakini ushikamanifu kwa Mungu uko na faida katika mambo yote, kwa maana uko na ahadi ya uzima wa sasa na ya ule wenye utakuja.+  Neno hilo ni lenye kutegemeka na linastahili kukubaliwa kabisa. 10  Hii ndiyo sababu tunafanya kazi kwa bidii na tunajikaza,+ kwa sababu tumeweka tumaini letu katika Mungu mwenye kuishi, ambaye ni Mwokozi+ wa watu wa namna zote,+ zaidi sana wa watu waaminifu. 11  Endelea kutoa amri hizi na kuzifundisha. 12  Usiruhusu hata kidogo mutu yeyote azarau ujana wako. Lakini, ukuwe mufano kwa waaminifu katika kusema, katika mwenendo, katika upendo, katika imani, na katika mwenendo safi. 13  Mupaka wakati nitakuja, endelea kufanya bidii katika kusoma mbele ya watu,+ kutia moyo,* na kufundisha. 14  Usizarau zawadi yenye kuwa ndani yako, yenye ulipata kupitia unabii wenye ulitolewa juu yako, wakati baraza la wazee liliweka mikono juu yako.+ 15  Fikiri sana* juu ya mambo hayo; zama katika mambo hayo, ili maendeleo yako yaonekane wazi kwa watu wote. 16  Endelea kuwa muangalifu juu yako mwenyewe na kuhusu kufundisha kwako.+ Endelea kufanya mambo hayo, kwa maana kwa kufanya vile utajiokoa wewe mwenyewe na utaokoa pia wale wenye wanakusikiliza.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “roho inasema.”
Tnn., “roho wenye kupotosha.”
Ao “kwa usahihi.”
Ao “kuhimiza.”
Ao “Tafakari.”