Ya Kwanza kwa Timoteo 2:1-15

  • Sala kwa ajili ya watu wa namna zote (1-7)

    • Mungu mumoja, mupatanishi mumoja (5)

    • Bei ya ukombozi yenye kulingana kwa ajili ya wote (6)

  • Maagizo kwa wanaume na wanamuke (8-15)

2  Basi, kwanza kabisa, ninawatia ninyi moyo kwamba sala za kumulilia Mungu,* sala, kuombea wengine, na sala za shukrani, zifanywe kwa ajili ya watu wa namna zote, 2  kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye kuwa katika vyeo vya juu,*+ ili tuendelee kuishi maisha ya amani na yenye utulivu pamoja na ushikamanifu kamili kwa Mungu na kuchukua mambo kwa uzito.+ 3  Mambo hayo ni ya muzuri na yanakubaliwa mbele ya macho ya Mwokozi wetu, Mungu,+ 4  mwenye mapenzi yake ni kwamba watu wa namna zote waokolewe+ na wapate ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli.* 5  Kwa maana kuko Mungu mumoja,+ na kuko mupatanishi mumoja+ kati ya Mungu na wanadamu,+ mwanadamu, Kristo Yesu,+ 6  mwenye alijitoa kuwa bei ya ukombozi yenye kulingana kwa ajili ya wote*+⁠—⁠hili ndilo litatolewa ushahidi kwa wakati wake mwenyewe wenye kufaa. 7  Niliwekwa kuwa muhubiri na mutume kwa kusudi la ushahidi+ huo+⁠—⁠ninasema kweli, siseme uongo⁠—⁠mwalimu wa mataifa+ kuhusiana na imani na kweli. 8  Basi ninatamani kwamba kila mahali wanaume waendelee kutoa sala, wakiinua mikono yao kwa ushikamanifu,+ bila kasirani+ wala mabishano.+ 9  Vilevile, wanamuke wajipambe kwa nguo zenye kufaa,* kwa kiasi na akili ya muzuri,* hapana kwa namna za kusuka nywele, kwa zahabu ao lulu, ao nguo za bei sana,+ 10  lakini kwa njia yenye kufaa wanamuke wenye wanasema kama wanashikamana na Mungu,+ ni kusema, kupitia matendo ya muzuri. 11  Mwanamuke ajifunze akiwa kimya* na akiwa mwenye kujitiisha kwa ukamili.+ 12  Siruhusu mwanamuke afundishe ao akuwe na mamlaka juu ya mwanaume, lakini abakie kimya.*+ 13  Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.+ 14  Tena, Adamu hakudanganywa, lakini mwanamuke ndiye alidanganywa kabisa+ na akakuwa mutenda-zambi. 15  Hata hivyo, mwanamuke atalindwa salama kupitia kuzaa watoto,+ kama tu ataendelea* kuwa na imani na upendo na utakatifu pamoja na akili ya muzuri.*+

Maelezo ya Chini

Ao “dua.”
Ao “wenye mamlaka.”
Ao “ujuzi sahihi wa ile kweli.”
Ao “watu wa kila namna.”
Ao “za heshima.”
Ao “uwezo wa kuchukua maamuzi ya muzuri; busara.”
Ao “kwa utulivu.”
Ao “akuwe mutulivu.”
Tnn., “wataendelea.”
Ao “uwezo wa kuchukua maamuzi ya muzuri; busara.”