Ya Kwanza kwa Timoteo 2:1-15
2 Basi, kwanza kabisa, ninawatia ninyi moyo kwamba sala za kumulilia Mungu,* sala, kuombea wengine, na sala za shukrani, zifanywe kwa ajili ya watu wa namna zote,
2 kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye kuwa katika vyeo vya juu,*+ ili tuendelee kuishi maisha ya amani na yenye utulivu pamoja na ushikamanifu kamili kwa Mungu na kuchukua mambo kwa uzito.+
3 Mambo hayo ni ya muzuri na yanakubaliwa mbele ya macho ya Mwokozi wetu, Mungu,+
4 mwenye mapenzi yake ni kwamba watu wa namna zote waokolewe+ na wapate ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli.*
5 Kwa maana kuko Mungu mumoja,+ na kuko mupatanishi mumoja+ kati ya Mungu na wanadamu,+ mwanadamu, Kristo Yesu,+
6 mwenye alijitoa kuwa bei ya ukombozi yenye kulingana kwa ajili ya wote*+—hili ndilo litatolewa ushahidi kwa wakati wake mwenyewe wenye kufaa.
7 Niliwekwa kuwa muhubiri na mutume kwa kusudi la ushahidi+ huo+—ninasema kweli, siseme uongo—mwalimu wa mataifa+ kuhusiana na imani na kweli.
8 Basi ninatamani kwamba kila mahali wanaume waendelee kutoa sala, wakiinua mikono yao kwa ushikamanifu,+ bila kasirani+ wala mabishano.+
9 Vilevile, wanamuke wajipambe kwa nguo zenye kufaa,* kwa kiasi na akili ya muzuri,* hapana kwa namna za kusuka nywele, kwa zahabu ao lulu, ao nguo za bei sana,+
10 lakini kwa njia yenye kufaa wanamuke wenye wanasema kama wanashikamana na Mungu,+ ni kusema, kupitia matendo ya muzuri.
11 Mwanamuke ajifunze akiwa kimya* na akiwa mwenye kujitiisha kwa ukamili.+
12 Siruhusu mwanamuke afundishe ao akuwe na mamlaka juu ya mwanaume, lakini abakie kimya.*+
13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.+
14 Tena, Adamu hakudanganywa, lakini mwanamuke ndiye alidanganywa kabisa+ na akakuwa mutenda-zambi.
15 Hata hivyo, mwanamuke atalindwa salama kupitia kuzaa watoto,+ kama tu ataendelea* kuwa na imani na upendo na utakatifu pamoja na akili ya muzuri.*+
Maelezo ya Chini
^ Ao “dua.”
^ Ao “wenye mamlaka.”
^ Ao “ujuzi sahihi wa ile kweli.”
^ Ao “watu wa kila namna.”
^ Ao “za heshima.”
^ Ao “uwezo wa kuchukua maamuzi ya muzuri; busara.”
^ Ao “kwa utulivu.”
^ Ao “akuwe mutulivu.”
^ Tnn., “wataendelea.”
^ Ao “uwezo wa kuchukua maamuzi ya muzuri; busara.”