Ya Kwanza ya Petro 5:1-14

  • Muchunge kundi la Mungu (1-4)

  • Mukuwe wanyenyekevu na mukeshe (5-11)

    • Mumutupie Mungu mahangaiko yenu yote (7)

    • Ibilisi ni kama simba mwenye kunguruma (8)

  • Maneno ya kumalizia (12-14)

5  Kwa hiyo, mimi kama muzee mwenzenu, nikiwa shahidi wa mateso ya Kristo na mushiriki wa utukufu wenye utafunuliwa,+ ninaomba hivi kwa* wazee wenye kuwa kati yenu:  Muchunge kundi la Mungu+ lenye liko chini ya uongozi wenu, mukiwa waangalizi,* hapana kwa kulazimishwa, lakini kwa kupenda mbele ya Mungu;+ hapana kwa kupenda faida yenye haiko ya haki,+ lakini kwa hamu;  hapana kwa kupiga ubwana juu ya wale wenye kuwa uriti wa Mungu,+ lakini mukuwe mifano kwa kundi.+  Na wakati muchungaji mukubwa+ atafunuliwa, mutapokea taji la utukufu lenye haliwezi kufifia.+  Katika njia ileile, ninyi vijana, mujitiishe kwa wanaume wazee.*+ Lakini ninyi wote muvae* unyenyekevu* wamoja kuelekea wengine, kwa sababu Mungu anawapinga wenye majivuno, lakini anawapatia wanyenyekevu fazili zenye hazistahiliwe.+  Kwa hiyo, mujinyenyekeze chini ya mukono wenye nguvu wa Mungu, ili awainue ninyi katika wakati wenye kufaa,+  wakati uleule mumutupie mahangaiko* yenu yote,+ kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.+  Mulinde akili zenu, mukuwe macho!+ Adui yenu, Ibilisi, anatembea huku na huku kama simba mwenye kunguruma, akitafuta kumumeza mutu.*+  Lakini mumupinge,+ mukiwa imara katika imani, mukijua kwamba mateso yaleyale yanapata ushirika muzima wa ndugu zenu* katika ulimwengu.+ 10  Lakini, kisha ninyi kuteseka wakati kidogo, Mungu wa fazili zote zenye hazistahiliwe, mwenye aliwaita kwenye utukufu wake wa milele+ katika umoja na Kristo, yeye mwenyewe atamaliza mazoezi yenu. Atawafanya kuwa imara,+ atawatia nguvu,+ atawafanya ninyi musitikisike. 11  Kwake yeye kukuwe nguvu milele. Amina. 12  Kupitia Silvano,*+ mwenye ninaona kuwa ndugu muaminifu, nimewaandikia ninyi kwa maneno kidogo ili kuwatia moyo na kutoa ushahidi kwa bidii kwamba hizi ndizo fazili zenye hazistahiliwe za Mungu zenye kuwa za kweli. Musimame imara katika fazili hizo. 13  Mwanamuke mwenye kuwa katika Babiloni, muchaguliwa kama ninyi, anawatumia salamu zake, na vilevile Marko,+ mwana wangu. 14  Musalimiane kwa busu ya upendo. Ninyi wote wenye kuwa katika umoja na Kristo mukuwe na amani.

Maelezo ya Chini

Ao “ninawatia moyo hivi.”
Ao “mukilichunga kwa uangalifu.”
Ao “kwa wazee.”
Ao “mujifunge.”
Ao “unyenyekevu wa akili.”
Ao “matatizo; wasiwasi.”
Ao “akitafuta mutu wa kumeza.”
Tnn., “undugu wenu.”
Anaitwa pia Sila.