Ya Kwanza ya Petro 4:1-19

  • Muishi kwa ajili ya mapenzi ya Mungu, kama vile Kristo alifanya (1-6)

  • Mwisho wa mambo yote umekaribia (7-11)

  • Kuteseka kwa sababu ya kuwa Mukristo (12-19)

4  Kwa kuwa Kristo aliteseka katika mwili,+ ninyi pia mujipatie nguvu kwa muelekeo* uleule wa akili; kwa sababu mutu mwenye ameteseka katika mwili ameachana na zambi,+ 2  ili aishi wakati wake wenye kubakia katika mwili, hapana tena kwa ajili ya tamaa za wanadamu,+ lakini kwa ajili ya mapenzi ya Mungu.+ 3  Kwa maana wakati wenye ulipita uliwatosha ninyi kufanya mapenzi ya mataifa+ wakati mulifanya matendo ya mwenendo mupotovu wa bila haya,* tamaa kali yenye haiwezi kuzuiwa, kunywa kupita kiasi, karamu za kupitisha mipaka, mashindano ya kunywa, na ibada za sanamu zenye kuchukiza.+ 4  Wanashangaa kwa sababu hamuendelee kukimbia pamoja nao katika mwendo uleule mubaya sana wa upotovu, basi wanawatukana ninyi.+ 5  Lakini watu hao watatoa hesabu kwa ule mwenye iko* tayari kuhukumu wazima na wafu.+ 6  Kwa kweli, hiyo ndiyo sababu habari njema ilitangazwa kwa wafu pia,+ ili hata kama wanahukumiwa katika mwili kwa maoni ya wanadamu, waishi kwa kupatana na roho kulingana na maoni ya Mungu. 7  Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia. Kwa hiyo, mukuwe na akili ya muzuri,+ na mukeshe* kuhusiana na sala.+ 8  Zaidi ya mambo yote, mukuwe na upendo mwingi ninyi kwa ninyi,+ kwa sababu upendo unafunika zambi nyingi.+ 9  Mukaribishane bila kunungunika.+ 10  Kwa kadiri kila mumoja amepokea zawadi, muitumie ili kutumikiana kama wasimamizi-nyumba wazuri wa fazili zenye hazistahiliwe za Mungu zenye zinaonyeshwa kwa njia mbalimbali.+ 11  Kama mutu yeyote anasema, afanye hivyo kama vile anasema maneno matakatifu kutoka kwa Mungu; kama mutu yeyote anatumikia, afanye hivyo kama vile anategemea nguvu zenye Mungu anatoa;+ ili katika mambo yote Mungu atukuzwe+ kupitia Yesu Kristo. Utukufu na nguvu ni zake milele na milele. Amina. 12  Wapendwa, musishangazwe na majaribu yenye kuwaka moto yenye yanawapata ninyi,+ kama vile munapatwa na kitu kigeni. 13  Tofauti na hilo, muendelee kufurahi+ kwa kadiri ninyi ni washiriki katika mateso ya Kristo,+ ili mufurahi na kuwa na furaha sana pia wakati wa ufunuo wa utukufu wake.+ 14  Kama munalaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo, ninyi ni wenye furaha,+ kwa sababu roho ya utukufu, ndiyo, roho ya Mungu, inatulia juu yenu. 15  Hata hivyo, mutu yeyote kati yenu asiteseke kwa sababu yeye ni muuaji ao mwizi ao mutenda-maovu ao mutu mwenye kujiingiza katika mambo ya watu wengine.+ 16  Lakini kama mutu yeyote anateseka kwa sababu yeye ni Mukristo, asisikie haya,+ lakini aendelee kumutukuza Mungu wakati wenye anabeba jina hili. 17  Kwa maana ni wakati wenye uliwekwa wa hukumu kuanza na nyumba ya Mungu.+ Sasa kama inaanza na sisi kwanza,+ basi itakuwa namna gani kwa wale wenye hawatii habari njema ya Mungu?+ 18  “Na kama mwenye haki anaokolewa kwa shida, itakuwa namna gani kwa mutu mwenye hamuogope Mungu na kwa mutenda-zambi?”+ 19  Kwa hiyo basi, wale wenye wanateseka kwa kufanya mapenzi ya Mungu waendelee kujitoa wenyewe* kwa Muumbaji muaminifu wakati wanatenda mema.+

Maelezo ya Chini

Ao “azimio; musimamo.”
Ao “matendo ya mwenendo wa bila haya.” Uwingi wa neno la Kigiriki a·selʹgei·a. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “eko.”
Ao “mukuwe macho.”
Ao “kupendekeza nafsi zao.”