Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Mutakuwa Mashahidi Wangu’

‘Mutakuwa Mashahidi Wangu’

“[Yesu] akawaambia: ‘. . . Mutakuwa mashahidi wangu . . . mupaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.’”MDO. 1:7, 8.

1, 2. (a) Ni nani aliye shahidi mukubwa zaidi wa Yehova? (b) Jina Yesu linamaanisha nini, na namna gani Yesu alitenda kulingana na jina lake?

“KWA ajili ya hili mimi nimezaliwa, na kwa ajili ya hili nimekuja ulimwenguni, ili nitoe ushahidi juu ya ile kweli.” (Soma Yohana 18:33-37.) Yesu alisema maneno hayo alipokuwa mbele ya Pilato, gavana Muroma wa jimbo la Yudea. Yesu alikuwa amekwisha kujitambulisha kuwa mufalme. Miaka mingi baadaye, mutume Paulo alitaja mufano huo wa ujasiri wa Yesu, ‘ambaye akiwa shahidi alifanya tangazo nzuri la hazarani mbele ya Pontio Pilato.’ (1 Tim. 6:13) Kwa kweli, wakati fulani inaomba bidii nyingi ili kuwa “shahidi mwaminifu na wa kweli” katika ulimwengu huu wa Shetani unaojaa chuki!—Ufu. 3:14.

2 Yesu alikuwa shahidi wa Yehova tangu kuzaliwa kwake, kwa sababu alikuwa Muyahudi. (Isa. 43:10) Lakini, ilikuwa wazi kwamba Yesu ndiye Shahidi mukubwa zaidi wa Yehova. Yesu alichukua kwa uzito pendeleo la kuitwa kwa jina la Mungu. Malaika alimuambia Yosefu, baba-mulishi wa Yesu, kwamba mimba ya Maria ilitokana na roho takatifu; kisha akaongeza hivi: ‘Yeye atazaa mwana, nawe lazima umwite jina lake Yesu, kwa maana ataokoa watu wake kutoka katika zambi zao.’ (Mt. 1:20, 21.) Watu wenye elimu ya Biblia wanakubali kwamba jina Yesu linatoka katika neno la Kiebrania, Yeshua, na linahusiana na maana ya jina la Mungu; jina hilo linamaanisha “Yehova Ni  Wokovu.” Kulingana na maana ya jina lake, Yesu alisaidia “kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli” watubu zambi zao ili Yehova awakubali tena. (Mt. 10:6; 15:24; Lu. 19:10) Kwa hiyo, Yesu alihubiri Ufalme wa Mungu kwa bidii. Injili ya Marko inasema hivi: “Yesu akaenda Galilaya, akihubiri habari njema ya Mungu na kusema: ‘Wakati uliowekwa umetimizwa, na ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni, na kuwa na imani katika habari njema.’” (Mk. 1:14, 15) Pia, kwa bidii Yesu alionyesha wazi unafiki wa viongozi wa dini ya Kiyahudi, ambao walifanya yote ili atundikwe kwenye muti.—Mk. 11:17, 18; 15:1-15.

‘MAMBO MAKUBWA YA MUNGU’

3. Ni jambo gani lilitokea siku tatu kisha kifo cha Yesu?

3 Jambo fulani lenye kushangaza lilitokea! Siku tatu kisha kifo cha Yesu, Yehova alimufufua akiwa kiumbe wa roho asiyeweza kufa. (1 Pet. 3:18) Ili kuonyesha kwamba alifufuliwa, Yesu alionekana katika mwili wa mwanadamu. Siku moja kisha kufufuliwa kwake, aliwatokea wanafunzi wake mara tano.—Mt. 28:8-10; Lu. 24:13-16, 30-36; Yoh. 20:11-18.

4. Kisha kufufuliwa, Yesu aliongoza mukutano gani, na alionyesha wazi daraka gani la wanafunzi wake?

4 Yesu alitokea mara ya tano ili kujionyesha kwa mitume wake na watu wengine waliokusanyika pamoja nao. Wakati huo wa pekee, alifanya mukutano ili kuwafundisha Neno la Mungu. ‘Alifungua akili zao ili kufahamu maana ya Maandiko.’ Wakati huo walielewa kwamba Maandiko yalikuwa yametabiri kwamba maadui wa Mungu wangemuua Yesu na kwamba Mungu angemufufua. Mwishoni mwa mukutano huo, Yesu aliwaonyesha wazi wasikilizaji wake jambo ambalo walipaswa kufanya. Aliwaambia kwamba ‘kwa musingi wa jina lake toba kwa musamaha wa zambi ingehubiriwa katika mataifa yote—kuanzia Yerusalemu.’ Aliongeza: ‘Ninyi munapaswa kuwa mashahidi wa mambo haya.’Lu. 24:44-48.

5, 6. (a) Sababu gani Yesu alisema: ‘Mutakuwa mashahidi wangu’? (b) Wanafunzi wa Yesu walipaswa kutangazia watu nini kuhusu kifo cha Yesu na kufufuliwa kwake?

5 Kwa hiyo, siku 40 baadaye, wakati Yesu aliwatokea kwa mara ya mwisho, mitume wake walikuwa wameelewa maana ya amri hii ya maana sana: ‘Mutakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu na pia katika Yudea yote na Samaria na mupaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.’ (Mdo. 1:8) Sababu gani Yesu alisema: ‘Mutakuwa mashahidi wangu,’ kuliko kusema mutakuwa Mashahidi wa Yehova? Yesu alisema hivyo kwa sababu wale aliokuwa akizungumuza nao walikuwa Waisraeli ambao tayari walikuwa Mashahidi wa Yehova.

Kwa sababu sisi ni wanafunzi wa Yesu, tunaendelea kujulisha watu kusudi la Yehova juu ya wakati unaokuja(Ona fungu la 5 na la 6)

6 Sasa, wanafunzi wa Yesu walipaswa kutangaza sehemu mupya ya kusudi la Yehova, ni kusema, jambo fulani kubwa sana kupita kukombolewa kwa Waisraeli katika utumwa huko Misri na baadaye katika Babiloni. Kifo cha Yesu Kristo na kufufuliwa kwake kungesaidia wanadamu wakombolewe katika utumwa mubaya zaidi, ni kusema, utumwa wa zambi na kifo. Wanafunzi wa Yesu waliotiwa mafuta kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33, walijulisha watu ‘mambo makubwa ya Mungu,’ na wengi waliosikia waliamini. Kwa hiyo, akiwa mbinguni, kwenye mukono wa kuume wa Baba yake, Yesu ameanza kuona namna watu wengi wametubu  na kumuamini yeye ambaye Yehova anatumia ili kuokoa watu.—Mdo. 2:5, 11, 37-41.

‘ZABIHU YA UKOMBOZI KWA AJILI YA WENGI’

7. Mambo yaliyotokea kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33 yalionyesha nini?

7 Mambo yaliyotokea kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33 yalionyesha kwamba Yehova alikubali zabihu ambayo Yesu alitoa, kuwa kifuniko kwa ajili ya zambi. (Ebr. 9:11, 12, 24) Yesu mwenyewe alisema kwamba alikuja ‘si kuhudumiwa lakini kuhudumu na kutoa uzima wake kuwa fidia [zabihu ya ukombozi] kwa ajili ya wengi.’ (Mt. 20:28) “Wengi” ambao wangefaidika na zabihu ya ukombozi ya Yesu hawakuwa tu Wayahudi waliotubu. Lakini, mapenzi ya Mungu ni kwamba “watu wa namna zote waokolewe,” kwa sababu zabihu ya ukombozi ‘inaondolea mbali zambi ya ulimwengu!’1 Tim. 2:4-6; Yoh. 1:29.

8. Wanafunzi wa Yesu walihubiri mupaka wapi, na iliwezekana namna gani?

8 Je, wanafunzi hao wapya wa Yesu walihitaji kuwa na bidii ili kuendelea kutoa ushahidi juu yake? Ndiyo kabisa, lakini hawangetimiza kazi hiyo kwa nguvu yao wenyewe. Roho takatifu ya Yehova iliwachochea na kuwapa nguvu ya kuendelea kutoa ushahidi. (Soma Matendo 5:30-32.) Miaka 27 kisha Pentekoste ya mwaka wa 33, ingeonekana wazi kwamba “kutangazwa kwa ile kweli ya habari njema” kulikuwa kumewafikia Wayahudi na Watu wa Mataifa “katika uumbaji wote ulio chini ya mbingu.”—Kol. 1:5, 23.

9. Kama ilivyotabiriwa, kutaniko la kwanza-kwanza la Kikristo lilipatwa na nini?

9 Lakini, jambo lenye kuhuzunisha ni kwamba, kutaniko la kwanza-kwanza lilianza kuharibika polepole. (Mdo. 20:29, 30; 2 Pet. 2:2, 3; Yuda 3, 4) Kama vile Yesu alisema, uasi-imani, ambao ulitokezwa na ‘yule muovu,’ Shetani, ungeendelea kuongezeka na ungejaribu kupoteza Ukristo wa kweli mupaka ‘umalizio wa mufumo wa mambo.’ (Mt. 13:37-43) Kisha, Yehova angemufanya Yesu kuwa Mufalme juu ya dunia yote. Jambo hilo lilitokea Mwezi wa 10, 1914; na hilo lilionyesha mwanzo wa “siku za mwisho” za ulimwengu huu muovu wa Shetani.—2 Tim. 3:1.

10. (a) Wakristo watiwa-mafuta wa siku zetu walisema ni mwaka gani ungekuwa wa maana sana? (b) Ni jambo gani lilitokea Mwezi wa 10, 1914, na namna gani jambo hilo limeonekana wazi kwa wote?

10 Wakristo watiwa-mafuta wa siku zetu walisema mbele ya wakati kwamba mwaka wa 1914 ungekuwa wa  maana sana. Walikuwa wamejifunza unabii wa Danieli kuhusu muti mukubwa uliokatwa na ambao ungeanza tena kuota kisha “nyakati saba.” (Dan. 4:16) Katika unabii kuhusu kuja kwake na ‘umalizio wa mufumo wa mambo,’ Yesu aliita kipindi hicho kuwa “nyakati zilizowekwa za mataifa.” Kuanzia mwaka wa 1914, ‘ishara ya kuwapo [kwa Kristo]’ akiwa Mufalme mupya wa dunia inaonekana wazi. (Mt. 24:3, 7, 14; Lu. 21:24) Kwa hiyo, kuanzia wakati huo ‘mambo makubwa ya Mungu’ yametia ndani kumufanya Yesu kuwa Mufalme juu ya wanadamu.

11, 12. (a) Mufalme mupya wa dunia alianza kufanya nini katika mwaka wa 1919? (b) Kuanzia mwaka wa 1935, ni jambo gani lilionekana wazi? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.)

11 Kisha tu kufanywa kuwa Mufalme, Yesu Kristo alianza kukomboa wafuasi wake watiwa-mafuta kutoka utumwa wa ‘Babiloni Mukubwa.’ (Ufu. 18:2, 4) Katika mwaka wa 1919, mwaka moja kisha Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, kulianzishwa kazi kubwa ya kuonyesha watu njia ambayo Mungu anatumia ili kutukomboa, na kuhubiri habari njema ya Ufalme. Wakristo watiwa-mafuta walitumia nafasi hiyo ili kuhubiri, na matokeo ni kwamba hesabu ya watiwa-mafuta, ambao ni wariti pamoja na Kristo, iliongezeka sana.

12 Katika mwaka wa 1935, ilionekana wazi kwamba Kristo alikuwa ameanza kukusanya mamilioni ya “kondoo wengine,” ambao wangefanyiza ‘mukutano mukubwa’ kutoka katika mataifa yote. Wanaongozwa na Wakristo watiwa-mafuta, pia wanaiga mufano wa ujasiri wa Yesu na wanatangaza wazi-wazi kwamba Mungu na Kristo ndio wamewaokoa. Wakristo wa mukutano mukubwa wanaendelea kuhubiri na wana imani katika zabihu ya ukombozi ya Kristo; kwa hiyo, watapata pendeleo la kuokoka ‘ziki kubwa,’ ambayo itamaliza ulimwengu huu wa Shetani.—Yoh. 10:16; Ufu. 7:9, 10, 14.

‘TUJIPATIE UJASIRI’ ILI KUTANGAZIA WATU HABARI NJEMA

13. Kwa sababu sisi ni Mashahidi wa Yehova, tumeazimia kufanya nini, na sababu gani tunaweza kuwa na uhakika kwamba tutaweza kufanya hivyo?

13 Tunapaswa kuendelea kuchukua kwa uzito pendeleo la kutoa ushahidi juu ya ‘mambo makubwa’ ambayo Yehova Mungu amefanya na juu ya ahadi zake za wakati unaokuja. Kwa kweli, sikuzote si vyepesi kutoa ushahidi juu ya mambo hayo. Ndugu zetu wengi wanahubiri katika maeneo ambamo watu hawapendezwe, wanawacheka, na wanawatesa sana. Tunaweza kufanya kama vile tu mutume Paulo na wenzake walifanya. Yeye alisema hivi: “Tulijipa ujasiri kwa njia ya Mungu wetu ili kuwaambia ninyi habari njema ya Mungu kwa kupambana sana.” (1 Thes. 2:2) Kwa hiyo, tusiache hata kidogo kuhubiri. Lakini, ulimwengu wa Shetani unapokaribia kuharibiwa tuendelee kuonyesha katika  maisha yetu kwamba tumejitoa kwa Mungu. (Isa. 6:11) Hatuwezi kufanya hivyo kwa nguvu yetu wenyewe, lakini tunapaswa kufuata mufano wa Wakristo wa kwanza; tunapaswa kusali kwa Yehova ili kupitia roho yake atupatie “nguvu zinazopita zile za kawaida.”—Soma 2 Wakorintho 4:1, 7; Lu. 11:13.

14, 15. (a) Wakristo walitendewa namna gani wakati wa mitume, na mutume Petro aliandika nini juu yao? (b) Tutajisikia namna gani ikiwa watu wanatutendea vibaya kwa sababu sisi ni Mashahidi wa Yehova?

14 Leo, watu wengi sana wanajiita Wakristo, ‘lakini wanamukana [Mungu] kwa matendo yao, kwa sababu ni wenye kuchukiza na wasiotii nao si wenye kukubalika kwa ajili ya kazi njema ya namna yoyote.’ (Tito 1:16) Ni vizuri tukumbuke kwamba wakati wa mitume, Wakristo wa kweli walichukiwa na watu wengi. Ndiyo sababu mutume Petro aliandika hivi: ‘Ikiwa munashutumiwa kwa ajili ya jina la Kristo, ninyi ni wenye furaha, kwa sababu . . . roho ya Mungu . . . inatulia juu yenu.’ —1 Pet. 4:14.

15 Je, maneno hayo yaliyoongozwa na roho yanahusu pia Mashahidi wa Yehova wa siku zetu? Ndiyo kabisa, kwa sababu tunatoa ushahidi juu ya utawala wa Kristo. Kwa hiyo, kuchukiwa kwa sababu tunaitwa kwa jina la Yehova ni sawa na ‘kushutumiwa kwa ajili ya jina la [Yesu] Kristo,’ ambaye aliwaambia wapinzani wake: ‘Mimi nimekuja katika jina la Baba yangu, lakini ninyi hamunipokee.’ (Yoh. 5:43) Kwa hiyo usivunjike moyo ikiwa unakutana na wapinzani unapohubiri. Kutendewa kwa namna hiyo kunaonyesha kwamba unakubaliwa na Mungu na kwamba roho yake ‘inatulia juu yako.’

16, 17. (a) Watumishi wa Yehova wanajionea nini katika sehemu nyingi za dunia? (b) Umeazimia kufanya nini?

16 Pia ni vizuri kukumbuka kwamba kuna ongezeko katika sehemu nyingi za dunia. Hata katika maeneo yanayohubiriwa sana, tunaendelea kupata watu walio tayari kutusikiliza na ambao tunaweza kuhubiria habari njema ya wokovu. Tusichoke kuwarudilia wale waliopendezwa, na ikiwezekana tujifunze nao Biblia, na hivyo kuwasaidia wafanye maendeleo mupaka wajitoe kwa Yehova na kubatizwa. Unaweza pia kujisikia kama dada Sarie, anayeishi Afrika ya Kusini, ambaye amehubiri kwa bidii kwa miaka zaidi ya 60. Anasema hivi: “Mimi ni mwenye shukrani sana kwa sababu, kupitia zabihu ya Yesu, nina uhusiano muzuri pamoja na Yehova, Mutawala Mukubwa wa ulimwengu wote, na nina furaha kwa sababu ninajulisha wengine jina lake.” Yeye pamoja na Martinus, bwana yake, wamesaidia watoto wao watatu, na pia watu wengine wengi kuwa watumishi wa Yehova. Sarie anaongeza hivi: “Hakuna kazi ingine inayoleta furaha kubwa zaidi, na kupitia roho yake takatifu, Yehova anapatia kila mumoja wetu nguvu anayohitaji ili kuendelea na kazi hiyo inayookoa uzima.”

17 Iwe tumebatizwa ao tunafanya maendeleo ili kufikia ubatizo, tuna sababu nzuri ya kuonyesha shukrani kwa pendeleo la kuwa katika kutaniko la Mashahidi wa Yehova la duniani pote. Kwa hiyo, endelea kutoa ushahidi kikamili na uendelee kujitenga na ulimwengu wa Shetani uliochafuka. Kwa kufanya hivyo, utamuletea utukufu Baba yetu wa mbinguni, ambaye tuna pendeleo la kuitwa kwa jina lake.