Kulingana na Yohana 1:1-51

  • Neno akakuwa mwili (1-18)

  • Ushahidi wenye Yohana Mubatizaji alitoa (19-28)

  • Yesu, Mwana-kondoo wa Mungu (29-34)

  • Wanafunzi wa kwanza wa Yesu (35-42)

  • Filipo na Natanaeli (43-51)

1  Katika mwanzo Neno alikuwa,+ na Neno alikuwa pamoja na Mungu,+ na Neno alikuwa mungu.*+ 2  Huyo alikuwa pamoja na Mungu katika mwanzo. 3  Vitu vyote vilifanywa kupitia yeye,+ na bila yeye hakuna hata kitu kimoja chenye kilifanywa. Kile chenye kimefanywa 4  kupitia yeye kilikuwa uzima, na uzima ulikuwa mwangaza wa wanadamu.+ 5  Na mwangaza unaangaza katika giza,+ lakini giza halikushinda mwangaza. 6  Kulitokea mutu mumoja mwenye alitumwa kama mwakilishi wa Mungu; jina lake lilikuwa Yohana.+ 7  Mutu huyo alikuja kama shahidi, ili atoe ushahidi juu ya mwangaza,+ kusudi watu wa namna zote waamini kupitia yeye. 8  Yeye hakukuwa mwangaza huo,+ lakini alipaswa kutoa ushahidi juu ya mwangaza huo. 9  Mwangaza wa kweli wenye unaangazia watu wa kila namna ulikuwa karibu kuja katika ulimwengu.+ 10  Alikuwa katika ulimwengu,+ na ulimwengu ulifanywa kupitia yeye,+ lakini ulimwengu haukumujua. 11  Alikuja kwa watu wake mwenyewe, lakini watu wake mwenyewe hawakumukubali. 12  Hata hivyo, wale wote wenye walimupokea, aliwapatia mamlaka ya kuwa watoto wa Mungu,+ kwa sababu walikuwa wanaonyesha imani katika jina lake.+ 13  Na hawakuzaliwa kutokana na damu ao kutokana na mapenzi ya mwili ao kutokana na mapenzi ya mwanadamu, lakini walizaliwa kutokana na Mungu.+ 14  Basi Neno akakuwa mwili+ na akakaa kati yetu, na tukaona utukufu wake, utukufu kama wa mwana muzaliwa-pekee+ kutoka kwa baba; na alikuwa amekubaliwa sana na Mungu* na alikuwa amejaa kweli. 15  (Yohana alitoa ushahidi juu yake, ndiyo, alisema kwa sauti kubwa: “Huyu ndiye nilisema juu yake, ‘Ule mwenye anakuja nyuma yangu ametangulia mbele yangu, kwa maana alikuwa mbele yangu.’”)+ 16  Kwa maana sisi wote tulipokea kutokana na wingi wake, hata fazili zenye hazistahiliwe juu ya fazili zenye hazistahiliwe. 17  Kwa sababu Sheria ilitolewa kupitia Musa,+ fazili zenye hazistahiliwe+ na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.+ 18  Hakuna mwanadamu mwenye amemuona Mungu wakati wowote;+ mungu muzaliwa-pekee+ mwenye kuwa pembeni ya*+ Baba ndiye ameeleza juu Yake.+ 19  Huu ndio ushahidi wenye Yohana alitoa wakati Wayahudi walituma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamuulize: “Wewe ni nani?”+ 20  Na akakubali jambo hilo na hakulikana, kwa kusema: “Mimi siko Kristo.” 21  Na wakamuuliza: “Basi, wewe ni nani? Je, wewe ndiye Eliya?”+ Akajibu: “Haiko mimi.” “Je, wewe ndiye ule Nabii?”+ Akajibu: “Hapana!” 22  Basi wakamuambia: “Wewe ni nani? Tuambie ili tujibu wale wenye walitutuma. Unasema nini juu yako mwenyewe?” 23  Akasema: “Mimi ni sauti ya mutu mwenye kusema kwa sauti kubwa katika jangwa, ‘Munyooshe njia ya Yehova,’*+ kama vile nabii Isaya alisema.”+ 24  Sasa wale wenye walimuuliza maulizo walikuwa wametumwa na Wafarisayo. 25  Kwa hiyo wakamuuliza: “Basi, sababu gani unabatiza kama wewe hauko Kristo ao Eliya ao ule Nabii?” 26  Yohana akawajibu: “Mimi ninabatiza katika maji. Kuko mutu mwenye amesimama katikati yenu mwenye ninyi hamumujue, 27  ule mwenye anakuja nyuma yangu, mwenye sistahili kufungua kamba ya kiatu chake.”+ 28  Mambo hayo yalifanyika kule Betania ngambo ingine ya Yordani, kwenye Yohana alikuwa anabatizia.+ 29  Siku yenye ilifuata alimuona Yesu anakuja kwake, na akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu mwenye anatosha zambi+ ya ulimwengu!+ 30  Huyu ndiye nilisema juu yake: ‘Kuko mwanaume mwenye anakuja nyuma yangu mwenye ametangulia mbele yangu, kwa maana alikuwa mbele yangu.’+ 31  Hata mimi sikumujua, lakini nilikuja kubatiza katika maji ili afunuliwe kwa Israeli.”+ 32  Yohana pia alitoa ushahidi, kwa kusema: “Niliona roho ikishuka kama njiwa kutoka mbinguni, na ikakaa juu yake.+ 33  Hata mimi sikumujua, lakini Ule mwenye alinituma nibatize katika maji aliniambia: ‘Mutu yeyote mwenye utaona roho inashuka na kukaa juu yake,+ huyo ndiye mwenye anabatiza katika roho takatifu.’+ 34  Na mimi nimeona, na nimetoa ushahidi kwamba huyo ndiye Mwana wa Mungu.”+ 35  Tena siku yenye ilifuata, Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili kati ya wanafunzi wake, 36  na wakati aliangalia Yesu anapita, akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu!” 37  Wakati wanafunzi hao wawili walisikia anasema vile, wakamufuata Yesu. 38  Kisha Yesu akageuka, na wakati aliona wanamufuata, akawauliza: “Munatafuta nini?” Wakamuambia: “Rabi (neno lenye wakati linatafsiriwa linamaanisha, “Mwalimu”), unakaa wapi?” 39  Akawaambia: “Mukuje na mutaona.” Basi wakaenda na kuona mahali alikuwa anakaa, na wakakaa pamoja naye siku hiyo; ilikuwa karibu saa ya kumi (10).* 40  Andrea,+ ndugu ya Simoni Petro, alikuwa mumoja wa wale wawili wenye walisikia mambo yenye Yohana alisema na akamufuata Yesu. 41  Kwanza alimupata Simoni ndugu yake na kumuambia: “Tumemupata Masiya”+ (neno lenye wakati linatafsiriwa linamaanisha, “Kristo”), 42  kisha akamupeleka kwa Yesu. Wakati Yesu alimuona, akasema: “Wewe ni Simoni,+ mwana wa Yohana; utaitwa Kefa” (jina lenye linatafsiriwa, “Petro”).+ 43  Siku yenye ilifuata alitaka kutoka na kuenda Galilaya. Basi Yesu akamupata Filipo+ na kumuambia: “Kuwa mufuasi wangu.” 44  Sasa Filipo alikuwa wa Betsaida, muji wa Andrea na Petro. 45  Filipo akamukuta Natanaeli+ na kumuambia: “Tumemupata ule mwenye Musa, katika Sheria, na Manabii waliandika juu yake: Yesu, mwana wa Yosefu,+ kutoka Nazareti.” 46  Lakini Natanaeli akamuambia: “Je, kuko kitu kizuri chenye kinaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamuambia: “Kuja na uone.” 47  Yesu akamuona Natanaeli anakuja kwenye alikuwa, na akasema hivi juu yake: “Ona, Mwisraeli wa kweli mwenye hana udanganyifu ndani yake.”+ 48  Natanaeli akamuuliza: “Umenijua namna gani?” Yesu akamujibu: “Mbele Filipo akuite, wakati ulikuwa chini ya muti wa tini, nilikuona.” 49  Natanaeli akamuambia: “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Israeli.”+ 50  Yesu akamuambia: “Je, unaamini kwa sababu nimekuambia nilikuona chini ya muti wa tini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.” 51  Kisha akamuambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, mutaona mbingu imefunguliwa na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka kwenye Mwana wa binadamu iko.”*+

Maelezo ya Chini

Ao “alikuwa wa kimungu.”
Ao “alikuwa amejaa fazili zenye hazistahiliwe.”
Ao “katika kifua cha Baba.” Inamaanisha mahali pa pendeleo la pekee.
Ni kusema, karibu saa 10 kisha muchana-kati (16:00).
Ao “eko.”