Kulingana na Yohana 1:1-51
1 Katika mwanzo Neno alikuwa,+ na Neno alikuwa pamoja na Mungu,+ na Neno alikuwa mungu.*+
2 Huyo alikuwa pamoja na Mungu katika mwanzo.
3 Vitu vyote vilifanywa kupitia yeye,+ na bila yeye hakuna hata kitu kimoja chenye kilifanywa.
Kile chenye kimefanywa
4 kupitia yeye kilikuwa uzima, na uzima ulikuwa mwangaza wa wanadamu.+
5 Na mwangaza unaangaza katika giza,+ lakini giza halikushinda mwangaza.
6 Kulitokea mutu mumoja mwenye alitumwa kama mwakilishi wa Mungu; jina lake lilikuwa Yohana.+
7 Mutu huyo alikuja kama shahidi, ili atoe ushahidi juu ya mwangaza,+ kusudi watu wa namna zote waamini kupitia yeye.
8 Yeye hakukuwa mwangaza huo,+ lakini alipaswa kutoa ushahidi juu ya mwangaza huo.
9 Mwangaza wa kweli wenye unaangazia watu wa kila namna ulikuwa karibu kuja katika ulimwengu.+
10 Alikuwa katika ulimwengu,+ na ulimwengu ulifanywa kupitia yeye,+ lakini ulimwengu haukumujua.
11 Alikuja kwa watu wake mwenyewe, lakini watu wake mwenyewe hawakumukubali.
12 Hata hivyo, wale wote wenye walimupokea, aliwapatia mamlaka ya kuwa watoto wa Mungu,+ kwa sababu walikuwa wanaonyesha imani katika jina lake.+
13 Na hawakuzaliwa kutokana na damu ao kutokana na mapenzi ya mwili ao kutokana na mapenzi ya mwanadamu, lakini walizaliwa kutokana na Mungu.+
14 Basi Neno akakuwa mwili+ na akakaa kati yetu, na tukaona utukufu wake, utukufu kama wa mwana muzaliwa-pekee+ kutoka kwa baba; na alikuwa amekubaliwa sana na Mungu* na alikuwa amejaa kweli.
15 (Yohana alitoa ushahidi juu yake, ndiyo, alisema kwa sauti kubwa: “Huyu ndiye nilisema juu yake, ‘Ule mwenye anakuja nyuma yangu ametangulia mbele yangu, kwa maana alikuwa mbele yangu.’”)+
16 Kwa maana sisi wote tulipokea kutokana na wingi wake, hata fazili zenye hazistahiliwe juu ya fazili zenye hazistahiliwe.
17 Kwa sababu Sheria ilitolewa kupitia Musa,+ fazili zenye hazistahiliwe+ na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.+
18 Hakuna mwanadamu mwenye amemuona Mungu wakati wowote;+ mungu muzaliwa-pekee+ mwenye kuwa pembeni ya*+ Baba ndiye ameeleza juu Yake.+
19 Huu ndio ushahidi wenye Yohana alitoa wakati Wayahudi walituma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamuulize: “Wewe ni nani?”+
20 Na akakubali jambo hilo na hakulikana, kwa kusema: “Mimi siko Kristo.”
21 Na wakamuuliza: “Basi, wewe ni nani? Je, wewe ndiye Eliya?”+ Akajibu: “Haiko mimi.” “Je, wewe ndiye ule Nabii?”+ Akajibu: “Hapana!”
22 Basi wakamuambia: “Wewe ni nani? Tuambie ili tujibu wale wenye walitutuma. Unasema nini juu yako mwenyewe?”
23 Akasema: “Mimi ni sauti ya mutu mwenye kusema kwa sauti kubwa katika jangwa, ‘Munyooshe njia ya Yehova,’*+ kama vile nabii Isaya alisema.”+
24 Sasa wale wenye walimuuliza maulizo walikuwa wametumwa na Wafarisayo.
25 Kwa hiyo wakamuuliza: “Basi, sababu gani unabatiza kama wewe hauko Kristo ao Eliya ao ule Nabii?”
26 Yohana akawajibu: “Mimi ninabatiza katika maji. Kuko mutu mwenye amesimama katikati yenu mwenye ninyi hamumujue,
27 ule mwenye anakuja nyuma yangu, mwenye sistahili kufungua kamba ya kiatu chake.”+
28 Mambo hayo yalifanyika kule Betania ngambo ingine ya Yordani, kwenye Yohana alikuwa anabatizia.+
29 Siku yenye ilifuata alimuona Yesu anakuja kwake, na akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu mwenye anatosha zambi+ ya ulimwengu!+
30 Huyu ndiye nilisema juu yake: ‘Kuko mwanaume mwenye anakuja nyuma yangu mwenye ametangulia mbele yangu, kwa maana alikuwa mbele yangu.’+
31 Hata mimi sikumujua, lakini nilikuja kubatiza katika maji ili afunuliwe kwa Israeli.”+
32 Yohana pia alitoa ushahidi, kwa kusema: “Niliona roho ikishuka kama njiwa kutoka mbinguni, na ikakaa juu yake.+
33 Hata mimi sikumujua, lakini Ule mwenye alinituma nibatize katika maji aliniambia: ‘Mutu yeyote mwenye utaona roho inashuka na kukaa juu yake,+ huyo ndiye mwenye anabatiza katika roho takatifu.’+
34 Na mimi nimeona, na nimetoa ushahidi kwamba huyo ndiye Mwana wa Mungu.”+
35 Tena siku yenye ilifuata, Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili kati ya wanafunzi wake,
36 na wakati aliangalia Yesu anapita, akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu!”
37 Wakati wanafunzi hao wawili walisikia anasema vile, wakamufuata Yesu.
38 Kisha Yesu akageuka, na wakati aliona wanamufuata, akawauliza: “Munatafuta nini?” Wakamuambia: “Rabi (neno lenye wakati linatafsiriwa linamaanisha, “Mwalimu”), unakaa wapi?”
39 Akawaambia: “Mukuje na mutaona.” Basi wakaenda na kuona mahali alikuwa anakaa, na wakakaa pamoja naye siku hiyo; ilikuwa karibu saa ya kumi (10).*
40 Andrea,+ ndugu ya Simoni Petro, alikuwa mumoja wa wale wawili wenye walisikia mambo yenye Yohana alisema na akamufuata Yesu.
41 Kwanza alimupata Simoni ndugu yake na kumuambia: “Tumemupata Masiya”+ (neno lenye wakati linatafsiriwa linamaanisha, “Kristo”),
42 kisha akamupeleka kwa Yesu. Wakati Yesu alimuona, akasema: “Wewe ni Simoni,+ mwana wa Yohana; utaitwa Kefa” (jina lenye linatafsiriwa, “Petro”).+
43 Siku yenye ilifuata alitaka kutoka na kuenda Galilaya. Basi Yesu akamupata Filipo+ na kumuambia: “Kuwa mufuasi wangu.”
44 Sasa Filipo alikuwa wa Betsaida, muji wa Andrea na Petro.
45 Filipo akamukuta Natanaeli+ na kumuambia: “Tumemupata ule mwenye Musa, katika Sheria, na Manabii waliandika juu yake: Yesu, mwana wa Yosefu,+ kutoka Nazareti.”
46 Lakini Natanaeli akamuambia: “Je, kuko kitu kizuri chenye kinaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamuambia: “Kuja na uone.”
47 Yesu akamuona Natanaeli anakuja kwenye alikuwa, na akasema hivi juu yake: “Ona, Mwisraeli wa kweli mwenye hana udanganyifu ndani yake.”+
48 Natanaeli akamuuliza: “Umenijua namna gani?” Yesu akamujibu: “Mbele Filipo akuite, wakati ulikuwa chini ya muti wa tini, nilikuona.”
49 Natanaeli akamuambia: “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Israeli.”+
50 Yesu akamuambia: “Je, unaamini kwa sababu nimekuambia nilikuona chini ya muti wa tini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.”
51 Kisha akamuambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, mutaona mbingu imefunguliwa na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka kwenye Mwana wa binadamu iko.”*+
Maelezo ya Chini
^ Ao “alikuwa wa kimungu.”
^ Ao “alikuwa amejaa fazili zenye hazistahiliwe.”
^ Ao “katika kifua cha Baba.” Inamaanisha mahali pa pendeleo la pekee.
^ Angalia Nyongeza A5.
^ Ni kusema, karibu saa 10 kisha muchana-kati (16:00).
^ Ao “eko.”