Ya Pili kwa Timoteo 3:1-17

  • Nyakati za hatari katika siku za mwisho (1-7)

  • Fuata mufano wa Paulo kwa ukaribu (8-13)

  • “Endelea kufuata mambo yenye ulijifunza” (14-17)

    • Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu (16)

3  Lakini ujue jambo hili, kwamba katika siku za mwisho+ kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia. 2  Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, wenye kujisifu, wenye kujivuna, wenye kumutukana Mungu, wenye hawatii wazazi, wenye hawana shukrani, wenye hawana ushikamanifu, 3  wenye hawana upendo wa asili, wenye hawataki makubaliano yoyote, wachongezi, wenye hawajizuie, wakali, wenye hawapendi wema, 4  wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi, wenye kupenda raha kuliko kumupenda Mungu, 5  wenye kwa inje wanaonekana kuwa na ushikamanifu kwa Mungu lakini wanakana nguvu za ushikamanifu huo;+ na wewe ujiepushe na watu wa namna hiyo. 6  Katikati ya hao kunainuka watu wenye kujiingiza kwa ujanja katika nyumba na kukamata mateka wanamuke wazaifu wenye kulemewa na mizigo ya zambi, wenye kuongozwa na tamaa mbalimbali, 7  wenye kujifunza sikuzote lakini hawawezi hata kidogo kupata ujuzi wenye hauna makosa* wa ile kweli. 8  Basi kwa namna yenye Yane na Yambre walipinga Musa, ni vile hawa pia wanaendelea kupinga kweli. Watu hao wameharibika kabisa katika akili, wakiwa wamekataliwa kuhusiana na imani. 9  Hata hivyo, hawatafanya maendeleo zaidi, kwa maana upumbavu* wao utaonekana na watu wote, kama vile ilikuwa kwa watu hao wawili.+ 10  Lakini wewe umefuata kwa ukaribu fundisho langu, mwendo wangu wa maisha,+ kusudi langu, imani yangu, subira yangu, upendo wangu, uvumilivu wangu, 11  mateso na shida kama zile zenye nilipata katika Antiokia,+ Ikoniamu,+ na Listra.+ Nilivumilia mateso hayo, na Bwana aliniokoa katika mambo hayo yote.+ 12  Kwa kweli, wale wote wenye wanapenda kuishi maisha ya ushikamanifu kwa Mungu katika umoja na Kristo Yesu watateswa pia.+ 13  Lakini watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi, wakipotosha watu na kupotoshwa wao wenyewe.+ 14  Hata hivyo, wewe endelea kufuata mambo yenye ulijifunza na yenye ulisadikishwa kuamini,+ ukijua ulijifunza mambo hayo kutoka kwa nani, 15  na kwamba tangu utoto wako+ umejua maandishi matakatifu,+ yenye yanaweza kukufanya ukuwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani katika Kristo Yesu.+ 16  Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu+ na liko na faida kwa kufundisha,+ kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo,* kwa kutia nizamu katika haki,+ 17  ili mutu wa Mungu akuwe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.

Maelezo ya Chini

Ao “ujuzi sahihi wa kweli.”
Ao “wazimu.”
Ao “kurekebisha.”