Yona 4:1-11

  • Yona anakasirika na anatamani kufa (1-3)

  • Yehova anamufundisha Yona kuwa na rehema (4-11)

    • “Je, uko na sababu ya kukasirika vile?” (4)

    • Mumea wa mutango unatumiwa kufundisha somo (6-10)

4  Lakini jambo hilo halikumufurahisha Yona hata kidogo, na akakasirika sana. 2  Kwa hiyo akasali hivi kwa Yehova: “Aa, sasa, Yehova, je, haiko vile nilikuwa ninafikiri wakati nilikuwa katika inchi yangu mwenyewe? Ndiyo sababu nilijaribu kwanza kukimbilia Tarshishi;+ kwa sababu nilijua kama wewe ni Mungu mwenye huruma* na rehema, mwenye hakasirike haraka na mwenye upendo mwingi mushikamanifu,+ mwenye kusikitika juu ya musiba. 3  Sasa, Ee Yehova, tafazali ondoa uzima wangu,* kwa sababu afazali nikufe kuliko kuishi.”+ 4  Yehova akamuuliza: “Je, uko na sababu ya kukasirika vile?” 5  Kisha Yona akatoka katika muji na kuenda kukaa upande wa mashariki wa muji. Akajijengea kibanda kule na kukaa chini ya kivuli chake ili aone jambo lenye litapata muji.+ 6  Kisha Yehova Mungu akaotesha mumea wa mutango* juu ya Yona ili apate kivuli kwa ajili ya kichwa chake na ili taabu yake ipunguke. Basi Yona akafurahia sana mumea huo wa mutango. 7  Lakini siku yenye ilifuata, wakati kulipambazuka,* Mungu wa kweli akatuma kidudu na kikashambulia mumea huo wa mutango, na ukakauka. 8  Wakati jua lilianza kuwaka, Mungu akatuma pia upepo wa mashariki wenye joto kali, na jua likamuchoma Yona kwenye kichwa, na alikuwa karibu kuzimia. Akaendelea kuomba akufe,* na alikuwa anasema, “Afazali nikufe kuliko kuishi.”+ 9  Mungu akamuuliza Yona: “Je, uko na sababu ya kukasirika vile kwa sababu ya mumea huo wa mutango?”+ Na Yona akasema: “Niko na sababu ya kukasirika, kukasirika sana na ninatamani hata nikufe.” 10  Lakini Yehova akasema: “Ulisikilia huruma mumea wa mutango wenye wewe haukuufanyia kazi, wala kuukomalisha; uliota usiku mumoja na kukauka usiku mumoja. 11  Je, singepaswa pia kusikilia huruma Ninawi muji mukubwa,+ wenye kuwa na watu zaidi ya elfu mia moja makumi mbili (120 000) wenye hawajue hata kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa,* na pia wanyama wao wengi?”+

Maelezo ya Chini

Ao “neema.”
Ao “nafsi yangu.”
Ao pengine, “mbarika; mbono.”
Ni kusema, wakati mwangaza wa asubui ulianza kutokea.
Ao “nafsi yake ikufe.”
Ao “tofauti kati ya mukono wao wa kuume na wa kushoto.”