Yona 1:1-17

  • Yona anajaribu kumukimbia Yehova (1-3)

  • Yehova analeta zoruba kali (4-6)

  • Taabu inatokea kwa sababu ya Yona (7-13)

  • Yona anatupwa katika bahari yenye zoruba (14-16)

  • Samaki mukubwa anamumeza Yona (17)

1  Neno la Yehova likakuja kwa Yona*+ mwana wa Amitai, na kusema:  “Simama, uende Ninawi+ ule muji mukubwa, na utangaze hukumu juu yake, kwa sababu nimeona uovu wao.”  Lakini Yona akasimama kuenda Tarshishi ili amukimbie Yehova; akashuka mupaka Yopa na akakuta mashua* ya kuenda Tarshishi. Basi akalipa malipo ya kusafiri na kuingia ndani ya mashua ili asafiri nao kuenda Tarshishi, mbali na Yehova.  Kisha Yehova akatokeza upepo mukali katika bahari, na kukakuwa zoruba kali sana mupaka mashua* ikakuwa karibu kuvunjika.  Wafanyakazi wa mashua* wakaogopa sana na kila mumoja wao akaanza kuitia mungu wake ili amusaidie. Na wakaanza kutupa katika bahari mizigo yenye ilikuwa ndani ya mashua ili kupunguza uzito wake.+ Lakini Yona alikuwa ameingia katika sehemu ya chini ya mashua, na kule alikuwa amelala na kusinzia kabisa.  Kapiteni wa mashua* akamukaribia na kumuambia: “Sababu gani unalala? Amuka, omba mungu wako! Pengine Mungu wa kweli atatufikiria, na hatutakufa.”+  Kisha wafanyakazi wa mashua* wakaambiana: “Mukuje, tupige kura+ ili tujue ni nani anatuletea taabu hii.” Basi wakapiga kura, na kura ikamuangukia Yona.+  Wakamuambia: “Tafazali utuambie, ni nani anatuletea taabu hii yenye imetupata? Unafanya kazi gani, na unatoka wapi? Unatoka inchi gani, na unatoka kwa watu gani?”  Akajibu: “Niko Mwebrania, na ninamuogopa* Yehova Mungu wa mbinguni, Mwenye aliumba bahari na inchi kavu.” 10  Kwa hiyo watu hao wakaogopa hata zaidi, na wakamuuliza: “Umefanya nini?” (Watu hao wakajua kwamba alikuwa anamukimbia Yehova, kwa sababu Yona alikuwa amewaambia.) 11  Basi wakamuambia: “Tukufanye nini ili bahari itulie?” Kwa sababu upepo mukali ulikuwa unaendelea kuongezeka katika bahari. 12  Akajibu: “Muninyangule na kunitupa katika bahari, na bahari itatulia kwa ajili yenu; kwa sababu ninajua kwamba zoruba hii kali imewapiga kwa sababu yangu.” 13  Lakini, watu hao wakajaribu kupiga makasia* kwa nguvu* ili kurudisha mashua* kwenye inchi kavu, hata hivyo hawakuweza kwa sababu upepo mukali uliendelea kuongezeka katika bahari pande zote. 14  Kisha wakamulilia Yehova na kusema: “Tafazali, Ee Yehova, tusikufe kwa sababu ya mutu huyu!* Usiweke juu yetu damu yenye haina kosa, kwa sababu umefanya kama vile ulipenda, Ee Yehova!” 15  Basi wakamunyangula Yona na kumutupa katika bahari; na bahari ikatulia. 16  Kisha watu hao wakamuogopa sana Yehova,+ na wakamutolea Yehova zabihu na kufanya naziri. 17  Sasa Yehova akatuma samaki mukubwa amumeze Yona, na Yona akakaa ndani ya tumbo la ule samaki siku tatu (3) muchana na usiku.+

Maelezo ya Chini

Maana yake “Njiwa.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “ninamuabudu.”
Kasia ni chombo chenye kufanana na mwiko chenye kinatumiwa kuendesha mashua.
Ao “wakajaribu kupasua njia.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “kwa sababu ya nafsi ya mutu huyu!”