Sefania 3:1-20
3 Ole wake muji wenye uasi,+ wenye kuchafuliwa, na wenye kukandamiza!
2 Haukutii sauti yoyote;+ haukukubali nizamu yoyote.+
Haukumutegemea Yehova;+ haukumukaribia Mungu wake.+
3 Wakubwa wake katikati yake ni simba wenye kunguruma.+
Waamuzi wake ni imbwa wa pori wakati wa usiku;Hawaache mufupa wowote wa kutafuna mupaka asubui.
4 Manabii wake ni wenye zarau, watu wenye udanganyifu.+
Makuhani wake wanachafua vitu vitakatifu;+Wanatendea sheria kwa jeuri.+
5 Yehova ni mwenye haki katikati ya muji huo;+ hafanye jambo lolote la mubaya.
Kila asubui anatangaza hukumu zake,+Hazikosekane kama vile mapambazuko.*
Lakini mwenye haiko mwenye haki hasikie haya.+
6 “Niliharibu mataifa; minara yao ya pembe iliachwa ukiwa.
Niliharibu barabara zao, na hivyo hakuna mutu yeyote mwenye alipita ndani.
Miji yao ilibakia mabomoko, bila mutu wala mukaaji yeyote.+
7 Nilisema, ‘Hakika utaniogopa na kukubali nizamu,’*+Ili makao yake yasiharibiwe+—Nitaomba muji huo utoe hesabu* kwa sababu ya mambo hayo yote.
Lakini walitamani sana kutenda kwa upotovu.+
8 ‘Kwa hiyo muendelee kuningojea kwa uvumilivu,’+ ni vile Yehova anasema,‘Mupaka siku nitasimama ili kukamata vitu vyenye vinanyanganywa katika vita,*Kwa maana uamuzi wangu wa hukumu ni kukusanya mataifa, kukusanya falme,Ili niwamwangie kasirani yangu kali, kasirani yangu yote yenye kuwaka;+Kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa bidii yangu.+
9 Kwa maana wakati huo nitabadilisha luga ya vikundi vya watu kuwa luga safi,Ili wote waitie jina la Yehova,Wamutumikie bega kwa bega.’*+
10 Kutoka eneo la mito ya Etiopia,Wale wenye kunililia, binti ya watu wangu wenye walisambazwa, wataniletea zawadi.+
11 Siku hiyo hamutapatishwa hayaKwa sababu ya matendo yenu yote ya uasi yenye mulinitendea,+Kwa maana wakati huo nitaondoa kati yenu watu wenye kujivuna kwa kiburi;Na hamutakuwa tena na majivuno katika mulima wangu mutakatifu.+
12 Nitaacha wanyenyekevu na watu wa hali ya chini wabakie katikati yenu,+Na watapata kimbilio katika jina la Yehova.
13 Watu wa Israeli wenye watabakia+ hawatatenda ukosefu wowote wa haki;+Hawatasema uongo, wala ulimi wa udanganyifu hautakuwa katika vinywa vyao;Watakula* na kulala, na hakuna mutu mwenye atawaogopesha.”+
14 Piga vigelegele vya shangwe, Ee binti ya Sayuni!
Piga vigelegele vya ushindi, Ee Israeli!+
Shangilia na kufurahi kwa moyo wako wote, Ee binti ya Yerusalemu!+
15 Yehova ameondoa hukumu juu yako.+
Ameelekeza adui yako mahali pengine.+
Yehova, Mufalme wa Israeli, iko* katikati yako.+
Hautaogopa tena musiba.+
16 Siku hiyo muji wa Yerusalemu utaambiwa:
“Usiogope, Ee Sayuni.+
Usiache mikono yako iregee.
17 Yehova Mungu wako iko* katikati yako.+
Atakuokoa kwa kuwa ni Mwenye nguvu.
Atakufurahia kwa shangwe kubwa.+
Atanyamaza* katika upendo wake.
Atashangilia kwa sababu yako kwa sauti za furaha.
18 Nitakusanya wale wenye kuhuzunika kwa sababu ya kukosa sikukuu zako;+Hawakukuwa kwako kwa sababu ya kubeba lawama kwa ajili ya muji huo.+
19 Angalia! Wakati huo nitapatia azabu wale wote wenye kukukandamiza;+Na nitamuokoa ule mwenye kutembea kwa kukokota muguu,*+Na nitakusanya wenye kutawanyika.+
Nitawafanya kuwa kitu cha kusifiwa na chenye kujulikana sana*Katika inchi yote ya haya yao.
20 Wakati huo nitawaingiza ndani,Wakati nitawakusanya pamoja.
Kwa maana nitawafanya kuwa kitu chenye kujulikana sana* na cha kusifiwa+ kati ya vikundi vyote vya watu wa dunia,Wakati nitarudisha mbele ya macho yenu watu wenu wenye walikamatwa mateka,” ni vile Yehova anasema.+
Maelezo ya Chini
^ Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
^ Ao “Nitapatia muji huo azabu.”
^ Ao “rekebisho.”
^ Ao pengine, “nitasimama nikiwa shahidi.”
^ Ao “Wamuabudu kwa umoja.”
^ Ao “Watajikulisha katika malisho.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “Atakaa kimya; Atatulia; Atatosheka.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “mwenye kuchechemea.”
^ Tnn., “jina.”
^ Tnn., “jina.”

