Sefania 1:1-18
1 Neno la Yehova lenye lilikuja kwa Sefania* mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana wa Hezekia katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni+ mufalme wa Yuda:
2 “Nitafagilia mbali kila kitu kutoka kwenye uso wa udongo,” ni vile Yehova anasema.+
3 “Nitafagilia mbali mwanadamu na munyama.
Nitafagilia mbali ndege wa mbinguni na samaki wa bahari,+Na vikwazo*+ pamoja na waovu;Na nitaondoa wanadamu kwenye uso wa udongo,” ni vile Yehova anasema.
4 “Nitanyoosha mukono wangu juu ya YudaNa juu ya wakaaji wote wa Yerusalemu,Na nitaondoa mahali hapa mabaki* yote ya Baali,+Jina la makuhani wa miungu ya kigeni na makuhani,+
5 Na wale wenye kuinamia jeshi la mbinguni juu ya sehemu za juu za nyumba,+Na wale wenye kumuinamia Yehova na kuapa kuwa washikamanifu kwake+Wakati huohuo wakiapa kuwa washikamanifu kwa Malkamu;+
6 Na wale wenye kuacha kumufuata Yehova+Na wenye hawamutafute Yehova wala kumuuliza.”+
7 Munyamaze mbele ya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, kwa maana siku ya Yehova iko karibu.+
Yehova ametayarisha zabihu; ametakasa wenye alialika.
8 “Katika siku ya zabihu ya Yehova nitaomba wakubwa watoe hesabu,Wana wa mufalme,+ na wote wenye kuvaa nguo za kigeni.
9 Nitaomba kila mutu mwenye kupanda kwenye jukwaa* siku hiyo atoe hesabu,Wale wenye kujaza nyumba ya bwana wao jeuri na udanganyifu.
10 Siku hiyo,” ni vile Yehova anasema,“Sauti ya kilio itasikika katika Mulango Mukubwa wa Samaki,+Makelele katika Eneo la Pili la muji,+Na kishindo kikubwa kutoka kwenye vilima.
11 Mulalamike, ninyi wakaaji wa Makteshi,*Kwa maana wafanyabiashara wote wameangamizwa;*Wale wote wenye kupima feza wameharibiwa.
12 Wakati huo nitatafuta-tafuta kabisa katika Yerusalemu kwa taa,Na nitaomba wale wenye hawajali* watoe hesabu, wale wenye kusema katika moyo wao,‘Yehova hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.’+
13 Mali yao itanyanganywa na nyumba zao zitaharibiwa.+
Watajenga nyumba, lakini hawataishi ndani;Na watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.+
14 Ile siku kubwa ya Yehova iko karibu!+
Iko karibu na inakuja haraka sana!*+
Sauti ya siku ya Yehova inaleta uchungu.+
Siku hiyo mupiganaji-vita atalia kwa sauti kubwa.+
15 Siku hiyo itakuwa siku ya kasirani kali,+Siku ya taabu na uchungu,+Siku ya zoruba na uharibifu,Siku ya giza na weusi,+Siku ya mawingu na giza nzito,+
16 Siku ya sauti ya baragumu na makelele ya vita,+Juu ya miji yenye ngome na juu ya minara mirefu ya pembe.+
17 Nitaletea wanadamu taabu,Na watatembea kama vipofu,+Kwa sababu wamemutendea Yehova zambi.+
Damu yao itamwangwa kama mavumbi,Na nyama* yao kama mavi.+
18 Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ya kasirani kali ya Yehova;+Kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa bidii yake,+Kwa sababu atafanya uharibifu, uharibifu wenye kuogopesha kwelikweli, wa wakaaji wote wa dunia.”+
Maelezo ya Chini
^ Maana yake “Yehova Ameficha (Ameweka Kama Hazina).”
^ Inaonekana ni vitu ao matendo yenye yanahusiana na ibada ya sanamu.
^ Ao “alama.”
^ Ao “kizingiti.” Pengine jukwaa la kiti cha mufalme.
^ Tnn., “wamenyamazishwa.”
^ Inaonekana lilikuwa eneo katika muji wa Yerusalemu karibu na Mulango Mukubwa wa Samaki.
^ Tnn., “wenye wanaganda juu ya machicha yao,” kama vile katika shimo la kukamulia divai. Machicha ni takataka za pombe zenye kubakia chini ya chombo.
^ Ao “inakuja mbio sana!”
^ Tnn., “matumbotumbo.”

