Sefania 1:1-18

  • Siku ya hukumu ya Yehova iko karibu (1-18)

    • Siku ya Yehova inakuja haraka sana (14)

    • Feza na zahabu haviwezi kuokoa (18)

1  Neno la Yehova lenye lilikuja kwa Sefania* mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana wa Hezekia katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni+ mufalme wa Yuda:  2  “Nitafagilia mbali kila kitu kutoka kwenye uso wa udongo,” ni vile Yehova anasema.+  3  “Nitafagilia mbali mwanadamu na munyama. Nitafagilia mbali ndege wa mbinguni na samaki wa bahari,+Na vikwazo*+ pamoja na waovu;Na nitaondoa wanadamu kwenye uso wa udongo,” ni vile Yehova anasema.  4  “Nitanyoosha mukono wangu juu ya YudaNa juu ya wakaaji wote wa Yerusalemu,Na nitaondoa mahali hapa mabaki* yote ya Baali,+Jina la makuhani wa miungu ya kigeni na makuhani,+  5  Na wale wenye kuinamia jeshi la mbinguni juu ya sehemu za juu za nyumba,+Na wale wenye kumuinamia Yehova na kuapa kuwa washikamanifu kwake+Wakati huohuo wakiapa kuwa washikamanifu kwa Malkamu;+  6  Na wale wenye kuacha kumufuata Yehova+Na wenye hawamutafute Yehova wala kumuuliza.”+  7  Munyamaze mbele ya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, kwa maana siku ya Yehova iko karibu.+ Yehova ametayarisha zabihu; ametakasa wenye alialika.  8  “Katika siku ya zabihu ya Yehova nitaomba wakubwa watoe hesabu,Wana wa mufalme,+ na wote wenye kuvaa nguo za kigeni.  9  Nitaomba kila mutu mwenye kupanda kwenye jukwaa* siku hiyo atoe hesabu,Wale wenye kujaza nyumba ya bwana wao jeuri na udanganyifu. 10  Siku hiyo,” ni vile Yehova anasema,“Sauti ya kilio itasikika katika Mulango Mukubwa wa Samaki,+Makelele katika Eneo la Pili la muji,+Na kishindo kikubwa kutoka kwenye vilima. 11  Mulalamike, ninyi wakaaji wa Makteshi,*Kwa maana wafanyabiashara wote wameangamizwa;*Wale wote wenye kupima feza wameharibiwa. 12  Wakati huo nitatafuta-tafuta kabisa katika Yerusalemu kwa taa,Na nitaomba wale wenye hawajali* watoe hesabu, wale wenye kusema katika moyo wao,‘Yehova hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.’+ 13  Mali yao itanyanganywa na nyumba zao zitaharibiwa.+ Watajenga nyumba, lakini hawataishi ndani;Na watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.+ 14  Ile siku kubwa ya Yehova iko karibu!+ Iko karibu na inakuja haraka sana!*+ Sauti ya siku ya Yehova inaleta uchungu.+ Siku hiyo mupiganaji-vita atalia kwa sauti kubwa.+ 15  Siku hiyo itakuwa siku ya kasirani kali,+Siku ya taabu na uchungu,+Siku ya zoruba na uharibifu,Siku ya giza na weusi,+Siku ya mawingu na giza nzito,+ 16  Siku ya sauti ya baragumu na makelele ya vita,+Juu ya miji yenye ngome na juu ya minara mirefu ya pembe.+ 17  Nitaletea wanadamu taabu,Na watatembea kama vipofu,+Kwa sababu wamemutendea Yehova zambi.+ Damu yao itamwangwa kama mavumbi,Na nyama* yao kama mavi.+ 18  Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ya kasirani kali ya Yehova;+Kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa bidii yake,+Kwa sababu atafanya uharibifu, uharibifu wenye kuogopesha kwelikweli, wa wakaaji wote wa dunia.”+

Maelezo ya Chini

Maana yake “Yehova Ameficha (Ameweka Kama Hazina).”
Inaonekana ni vitu ao matendo yenye yanahusiana na ibada ya sanamu.
Ao “alama.”
Ao “kizingiti.” Pengine jukwaa la kiti cha mufalme.
Tnn., “wamenyamazishwa.”
Inaonekana lilikuwa eneo katika muji wa Yerusalemu karibu na Mulango Mukubwa wa Samaki.
Tnn., “wenye wanaganda juu ya machicha yao,” kama vile katika shimo la kukamulia divai. Machicha ni takataka za pombe zenye kubakia chini ya chombo.
Ao “inakuja mbio sana!”
Tnn., “matumbotumbo.”