Rutu 2:1-23

  • Rutu anaokota masalio katika shamba la Boazi (1-3)

  • Rutu na Boazi wanakutana (4-16)

  • Rutu anamuelezea Naomi juu ya fazili za Boazi (17-23)

2  Basi Naomi alikuwa na mutu mumoja wa jamaa ya upande wa bwana yake mwenye alikuwa tajiri sana; jina lake lilikuwa Boazi,+ na alikuwa wa familia ya Elimeleki. 2  Rutu Mumoabu akamuambia Naomi: “Tafazali, uniache niende katika mashamba ili niokote masalio+ kati ya masuke ya nafaka nyuma ya mutu yeyote mwenye atanikubali.” Basi Naomi akamuambia: “Uende, binti yangu.” 3  Kwa hiyo akaenda na kuanza kuokota masalio katika shamba nyuma ya wavunaji. Bila kujua akajikuta katika shamba la Boazi,+ mwenye alikuwa wa familia ya Elimeleki.+ 4  Kisha Boazi akafika kutoka Betlehemu na akasalimia wavunaji: “Yehova akuwe pamoja na ninyi.” Nao wakajibu: “Yehova akubariki.” 5  Kisha Boazi akamuuliza kijana mwanaume mwenye alikuwa musimamizi wa wavunaji: “Huyu kijana mwanamuke ni wa nani?” 6  Kijana huyo mwanaume mwenye alikuwa musimamizi wa wavunaji akamujibu: “Huyu kijana mwanamuke ni Mumoabu+ mwenye alikuja na Naomi kutoka katika maeneo ya mashamba ya Moabu.+ 7  Aliniuliza, ‘Tafazali, ninaweza kuokota+ na kukusanya masalio kati ya masuke* yenye kukatwa ya nafaka yenye wavunaji waliacha nyuma?’ Na hajakaa tangu wakati alifika asubui hii mupaka sasa, na ni sasa tu ndio amekaa katika kibanda ili kupumuzika kidogo.” 8  Kisha Boazi akamuambia Rutu: “Sikiliza, binti yangu. Usiende kuokota masalio katika shamba lingine, wala usiende mahali pengine popote; bakia karibu na vijana wangu wanamuke.+ 9  Endelea kuangalia shamba lenye wanavuna, na uwafuate. Nimeamuru vijana wanaume wasikuguse.* Ukisikia kiu, uende kwenye mitungi ukunywe maji yenye vijana hao wanaume wameshota.” 10  Kwa hiyo akaanguka uso chini na kuinama mupaka chini na kumuambia: “Namna gani nimekubaliwa mbele ya macho yako, na sababu gani umenitambua, ijapokuwa mimi ni mugeni?”+ 11  Boazi akamujibu: “Wameniambia mambo yote yenye ulimufanyia mama-mukwe wako kisha bwana yako kufa na namna uliacha baba yako na mama yako na inchi ya watu wa jamaa yako na ukakuja kwa watu wenye haukukuwa unajua zamani.+ 12  Yehova akupatie zawabu kwa sababu ya mambo yenye ulifanya,+ na upate malipo kamili* kutoka kwa Yehova Mungu wa Israeli, mwenye umekuja kutafuta ulinzi chini ya mabawa yake.”+ 13  Basi Rutu akasema: “Acha nikubaliwe mbele ya macho yako, bwana wangu. Umenifariji na kusema na mutumishi wako kwa njia yenye kutuliza,* ijapokuwa mimi siko mumoja wa watumishi wako.” 14  Basi wakati wa kula, Boazi akamuambia: “Kuja hapa, ukule mukate na kuutia katika siki.”* Basi akakaa pembeni ya wavunaji. Boazi akamupatia nafaka yenye kukaangwa. Akakula, akashiba, na akaacha zingine. 15  Wakati alisimama ili aokote masalio,+ Boazi akaamuru vijana wake wanaume: “Mumuache aokote pia kati ya masalio ya masuke* yenye kukatwa ya nafaka, na musimutendee mubaya.+ 16  Pia, muhakikishe kwamba mumeondoa masuke fulani ya nafaka katika mafungu-mafungu na muyaache nyuma ili ayaokote, na musiseme jambo lolote ili kumukataza.” 17  Basi akaendelea kuokota masalio katika shamba mupaka mangaribi.+ Kisha kupiga-piga masalio yenye alikuwa ameokota, akapata karibu efa* moja ya shayiri. 18  Halafu akayakamata na kuenda katika muji, na mama-mukwe wake akaona masalio yenye alikuwa ameokota. Na Rutu akakamata chakula chenye aliacha+ kisha kushiba, akamupatia mama-mukwe wake. 19  Basi mama-mukwe wake akamuuliza: “Leo uliokota masalio wapi? Ulifanya kazi wapi? Abarikiwe mutu mwenye alikuona.”+ Kwa hiyo akamuelezea mama-mukwe wake kuhusu mutu mwenye alitumika naye, akasema: “Mwanaume mwenye nilitumika naye leo jina lake Boazi.” 20  Basi Naomi akamuambia binti-mukwe wake: “Mutu huyo abarikiwe na Yehova, mwenye hajakosa kuonyesha upendo mushikamanifu kwa wazima na wafu.”+ Naomi akaendelea kusema: “Mwanaume huyo ni mutu wa jamaa yetu.+ Ni mumoja wa wakombozi wetu.”*+ 21  Kwa hiyo Rutu Mumoabu akasema: “Aliniambia pia, ‘Ubakie karibu na vijana wangu mupaka wakati watamaliza mavuno yangu yote.’”+ 22  Basi Naomi akamuambia Rutu binti-mukwe wake: “Binti yangu, ni muzuri zaidi ufuatane na vijana wake wanamuke kuliko kusumbuliwa katika shamba lingine.” 23  Kwa hiyo akabakia karibu na vijana wanamuke wa Boazi na akaokota masalio+ mupaka mwisho wa mavuno ya shayiri na ya ngano. Na akaendelea kuishi pamoja na mama-mukwe wake.+

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “mafungu ya nafaka.”
Ao “wasikusumbue.”
Ao “zawabu kamili.”
Tnn., “umesema na moyo wa mutumishi wako.”
Ao “vinaigre.”
Ao pengine, “mafungu ya nafaka.”
Karibu litre 22 (vibaba 20). Angalia Nyongeza B14.
Ao “mutu wetu wa ukoo mwenye kuwa na haki ya kukomboa.”