Ya Pili kwa Watesalonike 3:1-18

  • Muendelee kusali (1-5)

  • Onyo juu ya kujiendesha bila utaratibu (6-15)

  • Salamu za mwisho (16-18)

3  Mwishowe, ndugu, muendelee kusali kwa ajili yetu,+ kwamba neno la Yehova* liendelee kuenea haraka+ na kutukuzwa, kama vile linafanya kwenu, 2  na kwamba Mungu atukomboe kutokana na watu wenye kuumiza na waovu,+ kwa maana imani haiko mali ya watu wote.+ 3  Lakini Bwana ni muaminifu, na atawatia ninyi nguvu na kuwalinda kutokana na ule muovu. 4  Zaidi ya hilo, tuko na uhakika katika Bwana juu yenu, kwamba munafanya na mutaendelea kufanya mambo yenye tunawaagiza. 5  Bwana aendelee kuongoza muzuri mioyo yenu ili mufikie upendo wa Mungu+ na mukuwe wavumilivu+ kwa ajili ya Kristo. 6  Sasa tunawapatia ninyi maagizo, ndugu, katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mujiepushe na kila ndugu mwenye anajiendesha bila utaratibu+ na hatembee kupatana na pokeo lenye* mulipata* kutoka kwetu.+ 7  Kwa maana ninyi wenyewe munajua namna munapaswa kutuiga,+ kwa sababu hatukujiendesha bila utaratibu kati yenu, 8  na hatukukula chakula cha mutu yeyote bure.*+ Lakini, kwa kazi ya jasho na ya taabu tulikuwa tunatumika usiku na muchana ili tusiwekee mutu yeyote kati yenu muzigo muzito.+ 9  Haimaanishe kama hatuna mamlaka,+ lakini tulitaka kuwawekea ninyi mufano ili mutuige.+ 10  Kwa kweli, wakati tulikuwa pamoja na ninyi, tulikuwa tunawapatia ninyi agizo hili: “Kama mutu yeyote hataki kufanya kazi, basi asikule pia chakula.”+ 11  Kwa maana tunasikia kama watu fulani wanajiendesha bila utaratibu kati yenu,+ hawafanye kazi yoyote, lakini wanajiingiza katika mambo yenye hayawaangalie.+ 12  Kwa watu wa namna hiyo tunatoa agizo na tunawatia moyo* katika jina la Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu na kula chakula chenye wao wenyewe walitumikia.+ 13  Kwa upande wenu, ndugu, musiache kutenda mema. 14  Lakini kama mutu yeyote hatii neno letu kupitia barua hii, mumutie mutu huyo alama na muache kushirikiana naye,+ ili apate haya. 15  Hata hivyo, musimuone mutu huyo kama adui, lakini muendelee kumuonya+ kama ndugu. 16  Sasa Bwana wa amani mwenyewe awapatie amani sikuzote katika kila njia.+ Bwana akuwe pamoja na ninyi wote. 17  Hii ni salamu yangu, mimi Paulo, yenye niliandika kwa mukono wangu mwenyewe.+ Na ni alama katika kila barua; hii ndiyo namna yangu ya kuandika. 18  Fazili zenye hazistahiliwe za Bwana wetu Yesu Kristo zikuwe pamoja na ninyi wote.

Maelezo ya Chini

Ao “agizo lenye.”
Ao pengine, “walipata.”
Ao “bila kulipa.”
Ao “tunawahimiza.”