Ya Pili kwa Watesalonike 2:1-17
2 Lakini, ndugu, kwa habari ya kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo+ na kukusanywa kwetu pamoja kwake,+ tunawaomba ninyi kwamba
2 akili yenu isivurugwe haraka, wala musiogopeshwe na neno lenye liliongozwa na roho,*+ ao na ujumbe wa maneno, ao na barua yenye inaonekana kama vile imetoka kwetu, ya kwamba siku ya Yehova*+ iko hapa.
3 Musiache mutu yeyote awadanganye* ninyi kwa njia yoyote, kwa sababu siku hiyo haitakuja mupaka uasi-imani+ ukuje kwanza na ule mutu wa uvunjaji wa sheria+ afunuliwe, ule mwana wa uharibifu.+
4 Yeye anapinga na kujiinua mwenyewe juu ya kila mwenye kuitwa mungu ao kitu cha kuabudiwa,* na hivyo anakaa katika hekalu la Mungu, akijionyesha mwenyewe waziwazi kuwa mungu.
5 Je, hamukumbuke kama wakati nilikuwa ningali pamoja na ninyi, nilikuwa ninawaambia mambo haya?
6 Na sasa munajua kile chenye kutenda kama kizuizi, ili afunuliwe katika wakati wake mwenyewe wenye kufaa.
7 Ni kweli, fumbo la huu uvunjaji wa sheria tayari linafanya kazi,+ lakini ni mupaka tu ule mwenye kutenda sasa kama kizuizi atakuwa ameondolewa katika njia.
8 Kisha, kwa kweli, ule mwenye kuvunja sheria atafunuliwa, ule mwenye Bwana Yesu atamuharibu kwa roho ya kinywa chake,+ na kumufanya kuwa bure wakati kuwapo kwa Yesu kutaonekana wazi.+
9 Lakini kuwapo kwa ule mwenye kuvunja sheria ni kupitia utendaji wa Shetani+ pamoja na kila tendo lenye nguvu na alama za uongo, na maajabu+
10 na kila udanganyifu wenye hauko wa haki,+ kwa wale wenye kuangamia, ili kuwa malipo kwa sababu hawakukubali kupenda ile kweli ili waokolewe.
11 Ndiyo sababu Mungu anaacha wadanganywe ili wafikie kuamini uongo,+
12 ili wote wahukumiwe kwa sababu hawakuamini ile kweli, lakini walifurahia ukosefu wa haki.
13 Lakini, tunalazimika kumushukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu wenye kupendwa na Yehova,* kwa sababu tangu mwanzo Mungu aliwachagua ninyi+ kwa ajili ya wokovu kwa kuwatakasa+ kupitia roho yake na kwa imani yenu katika kweli.
14 Aliwaita ninyi kwenye wokovu kupitia habari njema yenye tunatangaza, ili mupate utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.+
15 Basi, ndugu, musimame imara+ na muendelee kushika mapokeo yenye mulifundishwa,+ ikuwe ni kupitia ujumbe wa maneno ao kupitia barua kutoka kwetu.
16 Zaidi ya hayo, Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu mwenye alitupenda+ na kutupatia faraja ya milele na tumaini la muzuri+ kupitia fazili zenye hazistahiliwe,
17 wafariji mioyo yenu na kuwafanya ninyi kuwa imara* katika kila tendo na neno la muzuri.
Maelezo ya Chini
^ Ao “kupitia kwa roho.” Angalia Maana ya Maneno, “Roho.”
^ Angalia Nyongeza A5.
^ Ao “awashawishi.”
^ Ao “kuheshimiwa.”
^ Angalia Nyongeza A5.
^ Ao “kuwatia nguvu.”