Ya Pili kwa Watesalonike 2:1-17

  • Ule mutu wa uvunjaji wa sheria (1-12)

  • Wanaombwa wakuwe imara (13-17)

2  Lakini, ndugu, kwa habari ya kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo+ na kukusanywa kwetu pamoja kwake,+ tunawaomba ninyi kwamba 2  akili yenu isivurugwe haraka, wala musiogopeshwe na neno lenye liliongozwa na roho,*+ ao na ujumbe wa maneno, ao na barua yenye inaonekana kama vile imetoka kwetu, ya kwamba siku ya Yehova*+ iko hapa. 3  Musiache mutu yeyote awadanganye* ninyi kwa njia yoyote, kwa sababu siku hiyo haitakuja mupaka uasi-imani+ ukuje kwanza na ule mutu wa uvunjaji wa sheria+ afunuliwe, ule mwana wa uharibifu.+ 4  Yeye anapinga na kujiinua mwenyewe juu ya kila mwenye kuitwa mungu ao kitu cha kuabudiwa,* na hivyo anakaa katika hekalu la Mungu, akijionyesha mwenyewe waziwazi kuwa mungu. 5  Je, hamukumbuke kama wakati nilikuwa ningali pamoja na ninyi, nilikuwa ninawaambia mambo haya? 6  Na sasa munajua kile chenye kutenda kama kizuizi, ili afunuliwe katika wakati wake mwenyewe wenye kufaa. 7  Ni kweli, fumbo la huu uvunjaji wa sheria tayari linafanya kazi,+ lakini ni mupaka tu ule mwenye kutenda sasa kama kizuizi atakuwa ameondolewa katika njia. 8  Kisha, kwa kweli, ule mwenye kuvunja sheria atafunuliwa, ule mwenye Bwana Yesu atamuharibu kwa roho ya kinywa chake,+ na kumufanya kuwa bure wakati kuwapo kwa Yesu kutaonekana wazi.+ 9  Lakini kuwapo kwa ule mwenye kuvunja sheria ni kupitia utendaji wa Shetani+ pamoja na kila tendo lenye nguvu na alama za uongo, na maajabu+ 10  na kila udanganyifu wenye hauko wa haki,+ kwa wale wenye kuangamia, ili kuwa malipo kwa sababu hawakukubali kupenda ile kweli ili waokolewe. 11  Ndiyo sababu Mungu anaacha wadanganywe ili wafikie kuamini uongo,+ 12  ili wote wahukumiwe kwa sababu hawakuamini ile kweli, lakini walifurahia ukosefu wa haki. 13  Lakini, tunalazimika kumushukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu wenye kupendwa na Yehova,* kwa sababu tangu mwanzo Mungu aliwachagua ninyi+ kwa ajili ya wokovu kwa kuwatakasa+ kupitia roho yake na kwa imani yenu katika kweli. 14  Aliwaita ninyi kwenye wokovu kupitia habari njema yenye tunatangaza, ili mupate utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.+ 15  Basi, ndugu, musimame imara+ na muendelee kushika mapokeo yenye mulifundishwa,+ ikuwe ni kupitia ujumbe wa maneno ao kupitia barua kutoka kwetu. 16  Zaidi ya hayo, Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu mwenye alitupenda+ na kutupatia faraja ya milele na tumaini la muzuri+ kupitia fazili zenye hazistahiliwe, 17  wafariji mioyo yenu na kuwafanya ninyi kuwa imara* katika kila tendo na neno la muzuri.

Maelezo ya Chini

Ao “kupitia kwa roho.” Angalia Maana ya Maneno, “Roho.”
Ao “awashawishi.”
Ao “kuheshimiwa.”
Ao “kuwatia nguvu.”