Esta 3:1-15

  • Mufalme anamuinua Hamani (1-4)

  • Hamani anafanya mupango wa kuharibu Wayahudi (5-15)

3  Kisha mambo hayo Mufalme Ahasuero akamupandisha cheo Hamani+ mwana wa Hamedata Mwagagi+ na akamuinua kwa kuweka kiti chake juu ya wakubwa wengine wote wenye walikuwa pamoja naye.+ 2  Na watumishi wote wa mufalme wenye walikuwa kwenye mulango mukubwa wa mufalme waliinama na kushusha uso chini mbele ya Hamani, kwa maana ni vile mufalme alikuwa ameagiza kuhusu Hamani. Lakini Mordekai alikataa kuinama ao kushusha uso chini. 3  Basi watumishi wa mufalme wenye walikuwa kwenye mulango mukubwa wa mufalme wakamuambia Mordekai: “Sababu gani unapuuza amri ya mufalme?” 4  Kila siku walikuwa wanamuuliza, lakini hakuwasikiliza. Kisha wakamujulisha Hamani ili kuona kama mwenendo wa Mordekai ungevumiliwa;+ kwa maana Mordekai alikuwa amewaambia kwamba yeye ni Muyahudi.+ 5  Sasa wakati Hamani aliona kwamba Mordekai alikataa kuinama na kushusha uso chini mbele yake, Hamani akakasirika sana.+ 6  Lakini alizarau wazo la kumuua* Mordekai peke yake, kwa maana walikuwa wamemuambia kuhusu watu wa Mordekai. Kwa hiyo, Hamani akaanza kutafuta namna ya kuangamiza Wayahudi wote wenye walikuwa katika utawala wote wa Ahasuero, watu wote wa Mordekai. 7  Katika mwezi wa kwanza, ni kusema, mwezi wa Nisani,* katika mwaka wa kumi na mbili (12)+ wa Mufalme Ahasuero, walipiga Puri+ (ni kusema, Kura) mbele ya Hamani ili kujua siku na mwezi, na ikaangukia mwezi wa kumi na mbili, ni kusema, Adari.*+ 8  Kisha Hamani akamuambia Mufalme Ahasuero: “Kuko watu fulani wenye wametawanyika na kusambaa kati ya vikundi vya watu+ katika majimbo yote ya* utawala wako,+ sheria zao ziko tofauti na za vikundi vingine vyote vya watu, na hawatii sheria za mufalme, na mufalme hatapata faida yoyote kwa kuwaacha waendelee kuishi. 9  Kama inamupendeza mufalme, acha amri iandikwe kwamba waharibiwe. Na mimi nitalipa maofisa talanta* elfu kumi (10 000) za feza ili waziweke katika hazina ya mufalme.”* 10  Basi mufalme akatosha kwenye mukono wake pete yake ya kutia muhuri+ na akaipatia Hamani+ mwana wa Hamedata Mwagagi,+ mwenye alikuwa adui ya Wayahudi. 11  Mufalme akamuambia Hamani: “Umepewa feza na watu hao, ili uwatendee kama vile unaona inafaa.” 12  Kisha waandishi wa mufalme+ wakaitwa siku ya kumi na tatu (13) ya mwezi wa kwanza. Wakaandika mambo yote+ yenye Hamani aliamuru maliwali wa mufalme, magavana wenye walikuwa wanasimamia majimbo,* na wakubwa wa vikundi mbalimbali vya watu, kila jimbo* kwa mwandiko wake* na kila kikundi cha watu kwa luga yao wenyewe. Mambo hayo yaliandikwa katika jina la Mufalme Ahasuero na kutiwa muhuri kwa pete ya mufalme.+ 13  Barua zilitumwa kupitia wajumbe katika majimbo yote ya* mufalme, zilitoa amri ya kuangamiza, kuua, na kuharibu Wayahudi wote, vijana pamoja na wazee, wanamuke na watoto, katika siku moja, siku ya kumi na tatu (13) ya mwezi wa kumi na mbili (12), ni kusema, mwezi wa Adari,+ na kunyanganya mali zao.+ 14  Kopi ya maandishi hayo ilipaswa kutolewa kuwa sheria katika kila jimbo* na kutangaziwa vikundi vyote vya watu, ili wajitayarishe kwa ajili ya siku hiyo. 15  Wajumbe wakaondoka haraka+ kulingana na amri ya mufalme; sheria hiyo ilitolewa katika ngome* ya Shushani.*+ Kisha mufalme na Hamani wakakaa ili kunywa, lakini muji wa Shushani* ulikuwa katika muvurugo.

Maelezo ya Chini

Tnn., “kuweka mukono juu ya.”
Ao “wilaya zote za.”
Talanta moja ilikuwa sawa na kilograme 34.2 (aunsi troi 1.101). Angalia Nyongeza B14.
Ao pengine, “Nitalipa talanta 10 000 kwenye hazina ya mufalme kwa ajili ya wale wenye watafanya kazi hiyo.”
Ao “wilaya za utawala.”
Ao “wilaya ya utawala.”
Ao “namna yake ya kuandika.”
Ao “wilaya zote za utawala wa.”
Ao “wilaya ya utawala.”
Ao “nyumba ya mufalme.”
Ao “Susa.”
Ao “Susa.”