Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Mungu, Anazungumuza na Watu Wake

Yehova Mungu, Anazungumuza na Watu Wake

Sikia, tafazali, na mimi mwenyewe nitasema.’—AYUBU 42:4.

NYIMBO: 113, 114

1-3. (a) Sababu gani mawazo ya Mungu na namna yake ya kuzungumuza ni ya hali ya juu kuliko ya wanadamu? (b) Tutajifunza nini katika habari hii?

YEHOVA alipenda wengine wakuwe na uzima na wafurahie maisha, ndiyo sababu aliumba malaika na kisha wanadamu. (Zaburi 36:9; 1 Timotheo 1:11) Yehova aliumba kwanza kiumbe mwenye mutume Yohana anaita “Neno.” (Yohana 1:1; Ufunuo 3:14) Kiumbe huyo ni Yesu. Yehova alikuwa anazungumuza naye kwa kumuelezea mawazo yake na namna anajisikia. (Yohana 1:14, 17; Wakolosai 1:15) Mutume Paulo anasema kwamba malaika wanazungumuza pia na kwamba wako na luga, lakini luga yao ni tofauti kabisa na luga za wanadamu.—1 Wakorintho 13:1.

2 Yehova anajua mambo yote juu ya mamiliare ya malaika na wanadamu wenye aliumba. Ana uwezo wa kusikiliza sala za mamilioni ya watu kwa wakati uleule, na anaelewa sala zao hata kama wanatumia luga mbalimbali. Na wakati huohuo, anaendelea pia kuzungumuza na malaika na kuwaongoza. Mawazo ya Yehova na namna yake ya kuzungumuza ni ya hali ya juu kuliko ya wanadamu; ndiyo sababu ana uwezo wa kufanya mambo hayo yote. (Soma Isaya 55:8, 9.) Kwa hiyo, wakati anazungumuza na wanadamu, anatumia maneno mepesi ili tuelewe ujumbe wake.

3 Katika habari hii, tutajifunza namna Yehova anatumia njia yenye kuwa wazi ili kuzungumuza na wanadamu. Tutajifunza pia namna anabadilisha njia ya kuzungumuza kulingana na hali.

MUNGU ANAZUNGUMUZA NA WANADAMU

4. (a) Yehova alitumia luga gani ili kuzungumuza na Musa, Samweli, na Daudi? (b) Ni habari gani zenye kupatikana katika Biblia?

4 Pengine Yehova alitumia Kiebrania cha zamani wakati alizungumuza na mwanadamu wa kwanza, Adamu, katika shamba la Edeni. Kisha, Yehova alizungumuza na wanadamu kama vile Musa, Samweli, na Daudi. Hata kama walitumia maneno yao wenyewe ya Kiebrania na namna yao ya kuandika, kwa kweli waliandika mawazo ya Mungu. Waliandika maneno kutoka moja kwa moja kwa Yehova, na waliandika pia habari juu ya urafiki wa Mungu pamoja na watu wake. Kwa mufano, Biblia inazungumuzia imani yao, namna walimupenda Mungu, inazungumuzia pia makosa yao na namna walikosa uaminifu. Habari hizo zote ziliandikwa kwa faida yetu.—Waroma 15:4.

Waandikaji wa Biblia waliandika maneno kutoka moja kwa moja kwa Yehova, na waliandika pia habari juu ya urafiki wa Mungu pamoja na watu wake

5. Mungu alitumia tu luga ya Kiebrania ili kuzungumuza na watu? Eleza.

5 Yehova hakutumia kila mara Kiebrania ili kuzungumuza na watu. Kisha, wakati walikombolewa kutoka Babiloni, Waisraeli fulani walianza kuzungumuza Kiharamu. Pengine ndiyo sababu nabii Danieli, Yeremia, na Ezra waliandika sehemu fulani za Biblia katika Kiharamu. * (Soma maelezo ya chini.)

6. Sababu gani Maandiko ya Kiebrania ilitafsiriwa katika Kigiriki?

6 Wakati Alexandre Mukubwa alipata ushindi juu ya sehemu kubwa ya ulimwengu, watu katika inchi nyingi walianza kuzungumuza Koine ao Kigiriki cha kawaida. Wayahudi wengi walianza kuzungumuza Kigiriki, na kisha Maandiko ya Kiebrania ilitafsiriwa katika Kigiriki. Tafsiri hiyo inaitwa Septante. Hiyo ilikuwa tafsiri ya kwanza ya Biblia na iko kati ya tafsiri za maana zaidi. Watu wenye elimu ya Biblia wanaamini kwamba Septante ilitafsiriwa na watu 72. * (Soma maelezo ya chini.) Wamoja kati yao walitafsiri Maandiko ya Kiebrania neno kwa neno, lakini wengine hawakufanya hivyo. Lakini, Wayahudi wenye kuzungumuza Kigiriki na Wakristo waliamini kwamba tafsiri ya Septante ilikuwa Neno la Mungu.

7. Yesu alitumia luga gani ili kufundisha wanafunzi wake?

7 Pengine Yesu alikuwa anazungumuza Kiebrania wakati alikuwa hapa duniani. (Yohana 19:20; 20:16; Matendo 26:14) Pengine alitumia pia maneno fulani ya Kiharamu yenye ilitumiwa sana wakati huo. Lakini, alijua pia Kiebrania cha zamani chenye Musa na manabii wengine walitumia, kwa sababu maandishi hayo ilisomwa katika sinagogi kila juma. (Luka 4:17-19; 24:44, 45; Matendo 15:21) Pia, watu walikuwa wanazungumuza Kigiriki na Kilatini wakati wa Yesu; lakini Biblia haiseme ikiwa Yesu alizungumuza luga hizo ao hapana.

8, 9. Sababu gani Wakristo wengi walizungumuza Kigiriki, na hilo linatufundisha nini juu ya Yehova?

8 Wafuasi wa kwanza wa Yesu walizungumuza Kiebrania, lakini kisha kifo chake, wanafunzi wake walianza kuzungumuza luga zingine. (Soma Matendo 6:1.) Wakati habari njema iliendelea kuhubiriwa, Wakristo wengi walizungumuza Kigiriki kuliko Kiebrania. Kwa sababu Kigiriki ndiyo luga yenye ilijulikana sana, kitabu cha Mathayo, Marko, Luka, na Yohana viliandikwa katika Kigiriki. * (Soma maelezo ya chini.) Pia, barua za mutume Paulo na vitabu vingine vya Biblia viliandikwa katika Kigiriki.

9 Inafurahisha kujua kwamba, wakati waandikaji wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo walitaja Maandiko ya Kiebrania, walitumia mara nyingi tafsiri ya Septante. Wakati fulani, maandiko yenye walitaja ilikuwa tofauti kidogo na maandishi ya Kiebrania. Kwa hiyo, kazi hiyo ya watafsiri hao wasiokamilika ilikuja kuwa sehemu ya Biblia yenye tuko nayo leo. Jambo hilo linatufundisha kwamba Yehova haone luga ao desturi fulani kuwa ya maana sana kuliko ingine.—Soma Matendo 10:34.

Mungu hatuombe tujifunze kusema luga fulani ya pekee ili tufikie kumujua na mambo yenye amepanga kufanya

10. Njia yenye Yehova anatumia ili kuzungumuza na wanadamu imetufundisha nini?

10 Tumejifunza kwamba Yehova anazungumuza na wanadamu kulingana na hali. Hatuombe tujifunze kusema luga fulani ya pekee ili tufikie kumujua na mambo yenye amepanga kufanya. (Soma Zekaria 8:23; Ufunuo 7:9, 10.) Tumejifunza pia kwamba Yehova alitumia roho yake ili kuongoza waandikaji wa Biblia, lakini aliwaruhusu watumie maneno yao wenyewe ili kuandika mawazo yake.

MUNGU AMELINDA UJUMBE WAKE

11. Sababu gani Yehova anazungumuza na wanadamu hata kama wanasema luga mbalimbali?

11 Wanadamu wanazungumuza luga mbalimbali, lakini hilo halimuzuie Yehova kuzungumuza nao. Namna gani tunajua hilo? Biblia iko tu na maneno kidogo ya luga ya zamani yenye Yesu alitumia. (Mathayo 27:46; Marko 5:41; 7:34; 14:36) Lakini Yehova alihakikisha kwamba ujumbe wa Yesu uandikwe na kutafsiriwa katika Kigiriki na kisha katika luga zingine. Pia, kwa sababu Wayahudi na Wakristo walifanya mara nyingi kopi za Neno la Mungu, hilo lilisaidia kulinda ujumbe wa Mungu. Kisha, kopi hizo zilitafsiriwa katika luga nyingi zaidi. Miaka 400 hivi kisha kuzaliwa kwa Kristo, John Chrysostom alisema kwamba mafundisho ya Yesu ilikuwa imetafsiriwa katika luga ya Wasiria, Wamisri, Wahindi, Waperse, Waethiopia, na katika luga za watu wengine wengi.

12. Namna gani Biblia imeshambuliwa?

12 Katika historia, watu wameshambulia sana Biblia na wale wenye waliitafsiri na kuigawanya. Miaka 300 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, Dioclétien, Mutawala wa Roma, alitoa amri ili kopi zote za Biblia ziharibiwe. Kisha miaka 1200 hivi, William Tyndale alianza kutafsiri Biblia katika Kiingereza. Alisema kwamba ikiwa Mungu anamusaidia aendelee kuishi, atafanya yake yote ili hata kijana mwanaume mulimaji aelewe muzuri zaidi Biblia kuliko padiri. Kwa sababu Tyndale aliteswa, alitoka Angleterre na kukimbilia katika inchi ingine ya Ulaya ili atafsiri na kuchapisha Biblia yake. Viongozi wa kanisa walijaribu kulunguza kopi zote za Biblia zenye walipata; lakini watu wengi walikuwa wamepata tafsiri ya Tyndale. Kisha, Tyndale alifungwa kwenye muti na kulunguzwa. Lakini, viongozi wa dini hawakuweza kuharibu tafsiri hiyo, na ilitumiwa ili kutayarisha tafsiri ya Biblia yenye kuitwa King James Version.Soma 2 Timotheo 2:9.

13. Watu wenye elimu ya Biblia wametambua nini kisha kujifunza maandishi ya zamani ya Biblia?

13 Ni kweli kwamba kopi fulani za zamani za Biblia zinatofautiana kidogo na ziko na makosa fulani. Lakini, watu wenye elimu ya Biblia walijifunza kwa uangalifu maelfu ya maandishi, vipande vya maandishi ya zamani, na tafsiri za zamani za Biblia. Kisha kuzilinganisha na zingine, walitambua kwamba ni maandiko machache tu ndiyo ilikuwa tofauti kidogo na mengine. Lakini ujumbe wa Biblia haukubadilika. Mambo hayo yote inahakikishia wanafunzi wa Biblia kwamba Biblia yenye wako nayo leo iliongozwa na roho ya Yehova.—Isaya 40:8. * (Soma maelezo ya chini.)

14. Biblia inapatikana kwa kiasi gani leo?

14 Biblia ilishambuliwa sana, lakini imetafsiriwa katika luga zaidi ya 2800. Ndiyo kitabu chenye kupatikana sana kuliko vitabu vingine vyote. Watu wengi hawamuamini Mungu, lakini Neno lake Biblia ndiyo kitabu chenye kinaendelea kugawanywa sana. Tafsiri fulani za Biblia haziko mwepesi kusoma ao ziko na makosa, lakini tafsiri hizo zote zinapatia watu ujumbe mwepesi wa tumaini na uzima wa milele.

TULIKUWA NA LAZIMA YA TAFSIRI MUPYA YA BIBLIA

15. (a) Tangu mwaka wa 1919, kumekuwa badiliko gani kuhusu vichapo vyetu? (b) Sababu gani vichapo vyetu vinaandikwa kwanza katika Kiingereza?

15 Katika mwaka wa 1919, kikundi kidogo cha wanafunzi wa Biblia kiliwekwa kuwa ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara.’ Wakati huo, mutumwa mwaminifu alitumia zaidi sana Kiingereza ili kuzungumuza na watu wa Mungu. (Mathayo 24:45) Lakini leo, vitabu vyenye kutusaidia kuelewa Biblia vinapatikana katika luga zaidi ya 700. Kama vile Kigiriki cha zamani, leo luga ya Kiingereza inatumiwa katika biashara, kwenye masomo na inatumiwa sana na watu wengi. Kwa hiyo, vichapo vyetu vinaandikwa kwanza katika Kiingereza kisha vinatafsiriwa katika luga zingine.

16, 17. (a) Watu wa Mungu walikuwa na lazima ya nini? (b) Walifanya nini? (c) Ndugu Knorr alikuwa na kusudi gani?

16 Vichapo vyetu vyote vinategemea Biblia. Zamani, watu wa Mungu walitumia tafsiri ya King James Version, ya mwaka wa 1611. Lakini, tafsiri hiyo ilitumia maneno ya zamani na yenye haikuwa mwepesi kueleweka. Jina la Mungu lilipatikana sana katika maandishi ya zamani sana, lakini tafsiri hiyo ilitumia jina hilo mara chache tu. Tafsiri hiyo ilikuwa na makosa na ilikuwa pia na maandiko mengine yenye haikupatikana katika maandishi ya zamani. Tafsiri zingine za Biblia za Kiingereza zilikuwa pia na mambo hayo.

17 Ni wazi kwamba watu wa Mungu walikuwa na lazima ya tafsiri ya kweli kabisa ya Biblia na yenye kuwa mwepesi kueleweka. Kwa hiyo, Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mpya ilifanywa, na ndugu wa halmashauri hiyo walitangaza kutolewa kwa buku sita za tafsiri hiyo, kuanzia mwaka wa 1950 mupaka 1960. Buku la kwanza lilitolewa kwenye mukusanyiko mumoja wa tarehe 2 Mwezi wa 8, 1950. Kwenye mukusanyiko huo, Ndugu Knorr alisema kwamba watu wa Mungu walikuwa na lazima ya tafsiri ya sasa, yenye kuwa mwepesi kueleweka, ya kweli kabisa, na yenye ingewasaidia sana kuelewa kweli. Walikuwa na lazima ya tafsiri yenye kuwa mwepesi kusoma na kueleweka kama vile maandishi ya zamani yenye wanafunzi wa Yesu walitumia. Ndugu Knorr alipenda Tafsiri ya Ulimwengu Mpya isaidie watu wengi sana wafikie kumujua Yehova.

18. Ni mupango gani wenye ulichukuliwa ili kusaidia kazi ya kutafsiri Biblia?

18 Katika mwaka wa 1963, Ndugu Knorr alitimiza kusudi lake. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilitolewa katika Kiholanzi, Kifaransa, Kijerumani, Kiitaliano, Kiportige, na Kihispania. Katika mwaka wa 1989, Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova lilifanya idara mupya kwenye makao makubwa yetu ili kusaidia watafsiri wa Biblia. Kisha, katika mwaka wa 2005, watafsiri walipewa ruhusa ya kutafsiri Biblia katika luga zenye zilikuwa tayari zinatafsiri gazeti Munara wa Mulinzi. Kwa hiyo, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inapatikana leo ikiwa nzima ao sehemu katika luga zaidi ya 130.

19. Kulikuwa tukio gani la maana sana katika mwaka wa 2013, na tutajifunza nini katika habari yenye kufuata?

19 Luga ya Kiingereza imebadilika tangu kutolewa kwa Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya kwanza; kwa hiyo, ilikuwa lazima kutumia maneno ya sasa. Siku ya Posho tarehe 5, na Siku ya Yenga tarehe 6 Mwezi wa 10, 2013, watu 1413676 katika inchi 31 walihuzuria mukusanyiko wa pekee wa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Wamoja kati yao walikuwa kwenye mukusanyiko huo, na wengine waliufuata kwa njia ya telefone ao Internete. Ndugu mumoja wa Baraza Lenye Kuongoza alitangaza kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya sasa ya Kiingereza. Ndugu na dada walifurahi sana, na wengi kati yao walilia wakati walipokea Biblia hiyo mupya. Wakati wasemaji walikuwa wanasoma maandiko katika tafsiri hiyo, wote walitambua kwamba tafsiri hiyo mupya ni mwepesi sana kusoma na kueleweka. Katika habari yenye kufuata, tutajifunza mambo mengi zaidi juu ya tafsiri hiyo ya sasa, na namna inaendelea kutafsiriwa katika luga zingine.

^ fu. 6 Septante inamaanisha “Makumi Saba.” Inaonekana kwamba kazi ya kutafsiri Biblia hiyo ilianza miaka 300 hivi mbele ya kuzaliwa kwa Kristo na ilimalizika miaka 150 kisha. Tafsiri hiyo ingali ya lazima leo kwa sababu inasaidia watu wenye elimu ya Biblia waelewe maneno magumu ya Kiebrania ao maandiko fulani.

^ fu. 8 Watu fulani wanafikiri kwamba Mathayo aliandika kwanza kitabu chake katika Kiebrania, kisha pengine yeye mwenyewe alikitafsiri katika Kigiriki.

^ fu. 13 Soma Nyongeza A3 katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya sasa ya Kiingereza; soma pia habari “Hicho Kitabu Kiliokokaje?”, katika broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, ukurasa wa 7-9.