Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kumaliza Kukosana Katika Roho ya Upendo

Namna ya Kumaliza Kukosana Katika Roho ya Upendo

‘Mudumishe [muendeleze] amani kati ya mutu na mwenzake.’MARKO 9:50.

NYIMBO: 39, 77

1, 2. Ni mifano gani ya watu wenye walikosana wenye kuzungumuziwa katika kitabu cha Mwanzo, na sababu gani mifano hiyo inaweza kutusaidia?

UMEKWISHA kuwaza juu ya mifano ya watu wenye walikosana wenye kuzungumuziwa katika Biblia? Sura za kwanza-kwanza za kitabu cha Mwanzo zinatuonyesha kama Kaini alimuua Abeli (Mwanzo 4:3-8); Lameki alimuua kijana fulani mwanaume kwa sababu kijana huyo alimupiga (Mwanzo 4:23); wachungaji wa Abrahamu walibishana na wachungaji wa Loti (Mwanzo 13:5-7); Hagari alijiona kuwa wa maana kuliko Sara, na hilo lilifanya Sara amukasirikie Abrahamu (Mwanzo 16:3-6); Ishmaeli alikuwa adui ya kila mutu na kila alikuwa adui yake.—Mwanzo 16:12.

2 Sababu gani mifano hiyo inazungumuziwa katika Biblia? Kwa sababu mifano hiyo ya watu wenye hawakamilike wenye walikosana inaweza kutufundisha jambo fulani. Sisi pia hatukamilike, na wakati tunapata magumu kama hayo katika maisha yetu, tunaweza kuiga mifano ya muzuri yenye kupatikana katika Biblia na kuepuka mifano ya mubaya. (Waroma 15:4) Hilo linaweza kutusaidia tujue namna ya kufanya amani pamoja na wengine.

3. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Katika habari hii, tutajifunza sababu gani tunapaswa kumaliza kukosana ao kukosa kuelewana na wengine, na namna tunaweza kufanya hivyo. Tena, tutajifunza kanuni fulani za maana za Biblia zenye zinaweza kutusaidia tumalize kukosana na tuendeleze urafiki pamoja na Yehova na pamoja na watu wengine.

SABABU GANI WATUMISHI WA MUNGU WANAPASWA KUMALIZA KUKOSANA?

4. Ni mawazo gani yameenea katika dunia yote, na yamekuwa na matokeo gani?

4 Shetani ndiye anachochea sana watu wakuwe na migawanyiko na waendelee kukosana. Sababu gani tunasema hivyo? Katika shamba la Edeni, Shetani alisema kwamba kila mutu anaweza na anapaswa kuamua yeye mwenyewe mema na mabaya bila kuongozwa na Mungu. (Mwanzo 3:1-5) Lakini wakati tunaona mambo yenye kufanyika katika dunia leo, tunaona kama mawazo hayo yanaleta tu magumu. Watu wengi wanafikiri kama wako na haki ya kujiamulia wao wenyewe mema na mabaya. Wako na majivuno, wanajipenda wenyewe, na wako na roho ya mashindano, na hawahangaike ikiwa maamuzi yao yanaumiza wengine ao hapana. Mambo hayo yanafanya watu wakose kuelewana. Biblia inatukumbusha kwamba ikiwa tuko wenye kukasirika haraka, tutakosana sana na wengine na tutafanya zambi nyingi.—Methali 29:22.

5. Namna gani Yesu alifundisha watu wamalize kukosana na wengine?

5 Katika Mahubiri yake ya Mulimani, Yesu alifundisha wanafunzi wake namna ya kufanya amani na kuepuka kukosana na wengine, hata kama wangepoteza kitu fulani kwa kufanya hivyo. Kwa mufano, aliwaambia wakuwe wapole, wenye kufanya amani, waepuke kuwa na hasira, wamalize haraka kukosana, na wapende maadui wao.—Mathayo 5:5, 9, 22, 25, 44.

6, 7. (a) Sababu gani ni jambo la maana kumaliza kukosana bila kukawia? (b) Watumishi wote wa Yehova wanapaswa kujiuliza maulizo gani?

6 Leo, tunaabudu Yehova wakati tunasali, tunahubiri, na kuenda kwenye mikutano. Kama hatufanye amani pamoja na ndugu na dada, Yehova hatakubali ibada yetu. (Marko 11:25) Ili tukuwe marafiki wa Yehova, tunapaswa kusamehe wengine wakati wanatukosea.—Soma Luka 11:4; Waefeso 4:32.

Unasamehe haraka ndugu na dada zako?

7 Yehova anaomba watumishi wake wote wakuwe wenye kusamehe na waishi kwa amani pamoja na wengine. Unaweza kujiuliza hivi: ‘Ninasamehe haraka ndugu na dada zangu? Ninafurahia kuwa pamoja nao?’ Ikiwa unaona kama uko na lazima ya kuwa mwenye kusamehe zaidi, umuombe Yehova akusaidie. Baba yetu wa mbinguni atasikia sala zako zenye unatoa kwa unyenyekevu na kuzijibia.—1 Yohana 5:14, 15.

UNAWEZA KUSAHAU KOSA?

8, 9. Tunapaswa kufanya nini ikiwa mutu fulani anatukwaza?

8 Sisi wote hatukamilike; kwa hiyo, tunapaswa kujua kama watu wanaweza kusema ao kufanya mambo yenye yanaweza kutukwaza. (Mhubiri 7:20; Mathayo 18:7) Utatenda namna gani? Mufano wenye kufuata unaweza kutufundisha jambo la maana: Dada mumoja alisalimia ndugu wawili wenye alikutana nao nafasi fulani. Lakini ndugu mumoja alikwazika juu ya namna dada huyo alimusalimia. Wakati ndugu hao wawili walibakia wao wenyewe, ndugu mwenye alikwazika alianza kusema mubaya juu ya dada huyo. Lakini, ndugu mwengine alimukumbusha kama dada huyo amemutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka 40 hata kama amepata magumu mengi. Alihakikishia mwenzake kama dada huyo hakupenda kumukwaza. Ndugu mwenye alikwazika alitenda namna gani? Alisema hivi: “Unasema kweli.” Kisha aliamua kusahau jambo lenye lilitokea.

9 Mufano huo unatufundisha nini? Wakati mutu fulani anatukwaza, tunaweza kuamua tutatenda namna gani. Mutu mwenye kuwa na upendo anasemehe wengine. (Soma Methali 10:12; 1 Petro 4:8.) Wakati ‘tunapita [kusamehe] kosa’, jambo hilo linamufurahisha sana Yehova. (Methali 19:11; Mhubiri 7:9) Kwa hiyo, wakati mutu fulani anasema ao kufanya jambo lenye kukukwaza, ujiulize hivi: ‘Ninaweza kusahau kosa hili? Ni lazima kabisa niendelee kuwaza juu ya kosa hili?’

10. (a) Dada mumoja alitenda namna gani kwanza wakati wengine walisema mubaya juu yake? (b) Ni andiko gani lilimusaidia dada huyo aendelee kuwa na amani?

10 Wakati wengine wanasema maneno fulani ya mubaya juu yetu, inaweza kuwa vigumu kusahau maneno hayo. Fikiria jambo lenye lilimufikia dada mumoja painia mwenye tunaweza kuita Lucy. Wengine katika kutaniko walisema mubaya juu ya kazi yake ya kuhubiri na namna anatumia wakati wake. Alikwazika sana na aliomba mashauri kwa ndugu fulani wenye kukomaa kiroho. Hilo lilikuwa na matokeo gani? Dada huyo anasema kama walitumia Biblia ili kumusaidia aache kuwaza sana juu ya mambo ya mubaya yenye wengine walisema, na walimusaidia aanze kuwaza sana juu ya Yehova. Alitiwa moyo wakati alisoma andiko la Mathayo 6:1-4. (Soma.) Andiko hilo lilimukumbusha kama jambo la maana zaidi ni kumufurahisha Yehova. Kwa hiyo, aliamua kusahau maneno hayo ya mubaya. Leo, hata kama wengine wanasema mubaya juu ya kazi yake ya kuhubiri, anafurahi kwa sababu anajua kuwa anafanya yake yote ili kumufurahisha Yehova.

WAKATI UNAONA KUWA NI VIGUMU KUSAHAU KOSA

11, 12. (a) Mukristo anapaswa kufanya nini wakati anaona kama ndugu yake “ana jambo fulani juu” yake? (b) Namna Abrahamu alimaliza kukosana inaweza kutufundisha nini? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

11 ‘Sisi wote tunajikwaa mara nyingi.’ (Yakobo 3:2) Wazia unatambua kama ndugu ao dada fulani alikwazika kwa sababu ya jambo fulani lenye ulifanya ao kusema. Unapaswa kufanya nini? Yesu alisema kama ikiwa ‘unaleta zawadi yako kwenye mazabahu na hapo ukumbuke kwamba ndugu yako ana jambo fulani juu yako, acha zawadi yako hapo mbele ya mazabahu na uende zako; kwanza fanya amani yako pamoja na ndugu yako, na ndipo, ukiisha kurudi, itoe zawadi yako.’ (Mathayo 5:23, 24) Kwa hiyo, uzungumuze na ndugu ao dada yako. Wakati unazungumuza naye, kusudi lako linapaswa kuwa kufanya amani pamoja naye. Unapaswa kukubali kosa lako na usitafute kuonyesha kama yeye ndiye alikosea. Kufanya amani pamoja na ndugu ao dada zetu ni jambo la maana zaidi.

Kusudi letu linapaswa kuwa kufanya amani pamoja na ndugu na dada zetu

12 Biblia inaonyesha namna gani watumishi wa Mungu wanaweza kufanya amani wakati wanakosana. Kwa mufano, Abrahamu na Loti, mutoto wa ndugu yake, wote wawili walikuwa na wanyama wengi, na wachungaji wao walianza kukosana kwa sababu hawakukuwa na eneo la kutosha ili kulisha wanyama wao. Kwa sababu Abrahamu alipenda wakuwe na amani, alimuacha Loti achague eneo la muzuri zaidi. (Mwanzo 13:1, 2, 5-9) Abrahamu alituachia mufano wa muzuri sana! Je, Abrahamu aliendelea kujisikia kuwa alipoteza kitu fulani kwa sababu alionyesha ukarimu? Hapana kabisa. Kisha tu Abrahamu kufanya hivyo, Yehova alimuahidi kama atamubariki kwa kumupatia zaidi ya mambo yenye alipoteza. (Mwanzo 13:14-17) Hilo linatufundisha nini? Hata kama tunajisikia kuwa tumepoteza kitu fulani, Yehova atatubariki wakati tunamaliza kukosana katika roho ya upendo. [1]—Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.

13. Musimamizi mumoja alitenda namna gani wakati ndugu mwengine alimuambia maneno makali, na mufano huo unaweza kutufundisha nini?

13 Fikiria mufano wa siku zetu. Musimamizi wa mupya wa biro yenye kuangalia kazi fulani kwenye mukusanyiko alimuita ndugu mumoja ili kumuuliza ikiwa anaweza kutumika pamoja naye katika biro hiyo. Ndugu huyo alisema maneno mengi ya mubaya na kukata telefone kwa sababu alikuwa angali anamukasirikia musimamizi wa zamani wa biro hiyo. Musimamizi wa mupya hakukwazika, lakini hakuachilia jambo hilo lenye lilikuwa limetokea. Kisha saa moja, alimuita ndugu huyo tena na kumuomba waonane. Juma lenye lilifuata, ndugu hao walikutana kwenye Jumba la Ufalme, walisali kwa Yehova, na kisha wakazungumuza kwa saa moja. Ndugu huyo alimuelezea mwenzake tatizo lenye alipata na musimamizi wa zamani. Musimamizi huyo wa mupya alimusikiliza ndugu huyo kwa upole na wakazungumuzia maandiko fulani. Kwa hiyo, ndugu hao wawili walifanya amani na wakatumika pamoja kwenye mukusanyiko. Ndugu huyo ni mwenye shukrani kwa sababu musimamizi huyo alizungumuza naye kwa upole.

WAKATI WA KUOMBA MUSAADA KWA WAZEE

14, 15. (a) Ni wakati gani tunapaswa kutumikisha shauri la Mathayo 18:15-17? (b) Ni hatua gani tatu zenye Yesu alionyesha, na tunapaswa kuwa na kusudi gani wakati tunatumikisha hatua hizo?

14 Matatizo mengi kati ya Wakristo wawili yanaweza kumalizwa kati yao wenyewe. Lakini, wakati fulani ni vigumu kufanya hivyo. Katika hali fulani, ni muzuri kuomba musaada kwa ndugu wengine, kulingana na Mathayo 18:15-17. (Soma.) ‘Zambi’ yenye Yesu alitaja katika andiko hilo haiko kukosana kidogo kati ya Wakristo. Namna gani tunajua hivyo? Yesu alisema kama ikiwa mukosaji anakataa kutubu kisha kuzungumuza pamoja na ndugu ao dada yake, pamoja na mashahidi, ao pamoja na ndugu wengine wenye madaraka, tunapaswa kutendea ndugu ao dada huyo ‘kama mutu wa mataifa na kama mukusanya-kodi.’ Leo, hilo linamaanisha kama anapaswa kutengwa na kutaniko. ‘Zambi’ hiyo ni zambi kama vile kuiba mwengine kwa kutumikisha udanganyifu ao kusingizia mutu mwengine, lakini haiwezi kuwa uasherati, mwanaume kulala na mwanaume ao mwanamuke kulala na mwanamuke, uasi-imani, ao kuabudu sanamu. Zambi kama hizo zinapaswa kabisa kushugulikiwa na wazee.

Inaweza kuwa lazima kuzungumuza na ndugu ao dada yako mara nyingi ili kufanya amani naye (Picha hizi zinapatana na fungu la 15)

15 Wakati Yesu alitoa shauri hilo, alikuwa anapenda kutuonyesha namna ya kusaidia ndugu ao dada kwa sababu tunamupenda. (Mathayo 18:12-14) Namna gani tunaweza kutumikisha shauri hilo? (1) Tunapaswa kujikaza kufanya amani pamoja na ndugu ao dada yetu bila kuingiza watu wengine katika mambo yetu. Inaweza kuwa lazima tuzungumuze naye mara nyingi. Lakini, tunapaswa kufanya nini kama hatujakuwa na amani? (2) Tunapaswa kuzungumuza na ndugu ao dada yetu pamoja na mutu mwengine mwenye kujua jambo hilo ao mwenye anaweza kuona ikiwa kosa fulani limefanywa. Ikiwa munamaliza tatizo lenu, utakuwa ‘umemupata ndugu yako.’ Lakini ikiwa umezungumuza na ndugu na dada yako mara nyingi na hamukuweza kufanya amani pamoja naye (3) ambia wazee juu ya tatizo lenu.

16. Ni nini inaonyesha kama kufuata shauri la Yesu ni njia yenye kufaa na yenye upendo?

16 Katika hali nyingi, haiko lazima kufuata hatua zote tatu zenye kuonyeshwa katika Mathayo 18:15-17. Ni muzuri kujua hivyo. Sababu gani? Kwa sababu katika hali nyingi, mukosaji anatambua kosa lake na anatubu, kwa hiyo hawezi tena kutengwa na kutaniko. Kisha, ndugu ao dada mwenye alikwazika anapaswa kusamehe ndugu yake ili wapate amani. Kwa hiyo, shauri la Yesu linaonyesha wazi kama hatupaswe kuenda kuona wazee mbiombio. Tunapaswa tu kuambia wazee kisha kufuata hatua mbili za kwanza na kuko ushuhuda wenye kuonyesha kwamba ndugu ao dada amefanya kosa fulani.

17. Tutapata baraka gani wakati ‘tunatafuta amani’ pamoja na wengine?

17 Kwa sababu hatukamilike, tutaendelea kukosea wengine. Mwanafunzi Yakobo aliandika hivi: “Mutu asiyejikwaa katika kusema, huyu ni mutu mukamilifu, anayeweza kuongoza hata mwili wake wote.” (Yakobo 3:2; La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo) Ili kumaliza kukosana, tunapaswa kujikaza sana ‘kutafuta amani, na kuifuatia.’ (Zaburi 34:14) Wakati tunaendelea kufanya amani pamoja na wengine, tutafanya urafiki wa sana pamoja na ndugu na dada zetu, na hilo litafanya tuendelee kuwa na umoja. (Zaburi 133:1-3) Jambo la maana zaidi ni hili: tutakuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova, “Mungu anayetoa amani.” (Waroma 15:33) Tutapata baraka hizo zote ikiwa tunajikaza kumaliza kukosana katika roho ya upendo.

^ [1] (fungu la 12) Watu wengine wenye walimaliza kukosana katika roho ya amani ni Yakobo, pamoja na Esau (Mwanzo 27:41-45; 33:1-11); Yosefu, pamoja na ndugu zake (Mwanzo 45:1-15); na Gideoni, pamoja na watu wa kabila la Efraimu (Waamuzi 8:1-3). Pengine unaweza kufikiria mifano mingine kama hiyo katika Biblia.