Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Nini Inakusaidia Kukamata Maamuzi Yako?

Ni Nini Inakusaidia Kukamata Maamuzi Yako?

‘Muendelee kufahamu yale yaliyo mapenzi ya Yehova.’ WAEFESO 5:17.

NYIMBO: 69, 57

1. Taja sheria fulani za Biblia, na namna gani kutii sheria hizo kunatuletea faida?

KATIKA Biblia, Yehova ametupatia sheria zenye kutuonyesha waziwazi mambo yenye anapenda tufanye. Kwa mufano, anatuambia kama tunapaswa kuepuka kuabudu sanamu, kuiba, kulewa, ao kufanya mambo ya uasherati. (1 Wakorintho 6:9, 10) Na Yesu, Mwana wa Yehova, alipatia wanafunzi wake amri hii: ‘Muende mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, muwabatize katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi. Na, tazama! mimi nipo pamoja nanyi siku zote mupaka umalizio wa mufumo wa mambo.’ (Mathayo 28:19, 20) Mambo yote yenye Yehova na Yesu wanatuambia tufanye ni kwa faida yetu. Sheria za Yehova zinatufundisha namna ya kujihangaikia sisi wenyewe na kuhangaikia familia zetu, na zinatusaidia kuwa na afya ya muzuri na kuwa na furaha. Jambo la maana zaidi ni kwamba wakati tunatii sheria za Yehova na amri ya kuhubiri, hilo linamufurahisha na anatubariki.

2, 3. (a) Sababu gani Biblia haitupatie sheria juu ya kila hali katika maisha? (b) Tutazungumuzia maulizo gani katika habari hii? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

2 Lakini Biblia haitupatie sheria juu ya kila jambo lenye tunafanya katika maisha. Kwa mufano, Biblia haitoe maagizo yenye kuwa wazi juu ya muvalio. Hilo linaonyesha kama Yehova ni mwenye hekima sana. Kuko mitindo ao mivalio ya namna mbalimbali katika dunia yote, na mitindo hiyo inaendelea kubadilika, lakini mashauri ya Biblia hayabadilike hata kidogo. Pia, Biblia haitoe sheria nyingi juu ya kazi ao mambo ya kujifurahisha yenye tunapaswa kuchagua, ao juu ya mambo yenye tunapaswa kufanya kabisa ili tukuwe na afya ya muzuri. Yehova anaacha kila mutu na baba wa familia wakamate maamuzi juu ya mambo hayo.

3 Kwa hiyo, wakati tunapaswa kukamata uamuzi wa maana wenye utakuwa na matokeo juu ya maisha yetu na hakuna sheria fulani katika Biblia juu ya jambo hilo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Yehova anapendezwa na uamuzi wenye ninakamata? Hata kama sivunje sheria fulani ya Biblia, Yehova atafurahia uamuzi wowote wenye nitakamata? Namna gani ninaweza kuwa hakika kama atafurahia uamuzi wangu?’

MAAMUZI YENYE TUNAKAMATA YAKO NA MATOKEO JUU YETU NA JUU YA WENGINE

4, 5. Maamuzi yenye tunakamata yanaweza kuwa na matokeo gani juu yetu na juu ya wengine?

4 Watu fulani wanawaza kama wanaweza kufanya mambo yote yenye wanapenda kufanya. Lakini tunapenda kufanya mambo yenye kumufurahisha Yehova. Kwa hiyo, mbele ya kukamata uamuzi fulani, tunapaswa kufikiria mambo yenye Biblia inasema na kuyatii. Kwa mufano, Biblia inatuambia mawazo ya Mungu juu ya namna ya kutumia damu, kwa hiyo, tunatii mambo yenye Biblia inasema juu ya jambo hilo. (Mwanzo 9:4; Matendo 15:28, 29) Tunaweza kumuomba Yehova atusaidie tukamate maamuzi yenye kumupendeza.

5 Maamuzi yenye tunakamata yako na matokeo juu yetu. Uamuzi muzuri unaweza kutusaidia tumukaribie Yehova zaidi. Uamuzi wa mubaya unaweza kuharibu urafiki wetu pamoja naye. Pia, maamuzi yetu yanaweza kuwa na matokeo juu ya wengine. Hatupendi kufanya jambo fulani lenye linaweza kukwaza ndugu na dada zetu ao kuregeza imani yao. Pia, hatupendi kuharibu umoja kati ya ndugu na dada katika kutaniko. Kwa hiyo, ni jambo la maana tukamate maamuzi ya muzuri.—Soma Waroma 14:19; Wagalatia 6:7.

6. Tunapaswa kufikiria nini wakati tunakamata maamuzi yetu?

6 Namna gani tunaweza kukamata maamuzi ya muzuri wakati Biblia haituambie waziwazi mambo yenye tunapaswa kufanya? Kuliko kufanya tu mambo yenye tunapenda, tunapaswa kufikiria kwa uangalifu hali yetu wenyewe na kukamata maamuzi yenye kumupendeza Yehova. Kisha tunaweza kuwa hakika kama atatusaidia kupata matokeo ya muzuri.—Soma Zaburi 37:5.

YEHOVA ANATAKA NIFANYE NINI?

7. Wakati hakuna sheria ya Biblia, namna gani tunaweza kujua mambo yenye Yehova anataka tufanye katika hali fulani?

7 Lakini, namna gani tunaweza kujua mambo yenye kumupendeza Yehova? Andiko la Waefeso 5:17 linasema hivi: ‘Muendelee kufahamu yale yaliyo mapenzi ya Yehova.’ Wakati hakuna sheria fulani ya Biblia yenye kuwa wazi, tunapaswa kufahamu ao kuelewa, mambo yenye Yehova anataka tufanye katika hali yetu. Namna gani tunaweza kufanya hivyo? Tunapaswa kusali kwake na kuacha roho yake takatifu ituongoze.

8. Namna gani Yesu alijua mambo yenye Yehova alitaka afanye? Toa mufano.

8 Sikuzote, Yesu alielewa mambo yenye Yehova alitaka afanye. Kwa mufano, mara mbili wakati watu wengi walikuwa na njaa, Yesu alisali na kisha aliwapatia chakula kwa njia ya muujiza. (Mathayo 14:17-20; 15:34-37) Lakini, wakati alikuwa na njaa katika jangwa, Ibilisi alitaka ageuze majiwe yakuwe mukate, Yesu alikataa kufanya hivyo. (Soma Mathayo 4:2-4.) Alijua Baba yake muzuri sana; kwa hiyo, alijua kama Yehova hangetaka atumie roho takatifu kwa ajili ya mambo yake ya lazima. Kila mara alikuwa hakika kama Baba yake angemuongoza na kumupatia chakula chenye alikuwa nacho lazima.

9, 10. Ni nini itatusaidia tukamate maamuzi ya muzuri? Toa mufano.

9 Kama Yesu, tunaweza kukamata maamuzi ya muzuri ikiwa tunategemea muongozo wa Yehova. Biblia inasema hivi: ‘Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Umutambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako. Usikuwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe. Umuogope Yehova na ujiepushe na ubaya.’ (Methali 3:5-7) Wakati tunajifunza Biblia na kujua mawazo ya Yehova, tutaelewa mambo yenye anapenda tufanye katika hali fulani. Na ikiwa tunaendelea kujua zaidi mawazo ya Yehova, itakuwa vyepesi kwetu kukamata maamuzi yenye kumupendeza. Kwa kufanya hivyo, tutaendelea kuwa na “moyo wa nyama,” ni kusema, tutakuwa tayari kukubali muongozo wa Mungu.—Ezekieli 11:19.

10 Wazia kuwa mwanamuke fulani mwenye kuolewa anauza vitu katika soko na anaona viatu vya muzuri. Lakini ni vya bei sana. Hata kama bwana yake haiko pamoja naye, anajua bwana yake atawaza nini ikiwa anatumia feza nyingi ili kuuza viatu hivyo. Namna gani anajua mawazo ya bwana yake? Ameishi pamoja na bwana yake katika ndoa kwa miaka fulani, na anajua namna anapenda watumikishe feza zao. Vilevile, wakati tunajua mawazo ya Yehova na mambo yenye alifanya zamani, tutajua mambo yenye anapenda tufanye katika hali mbalimbali.

NAMNA GANI UNAWEZA KUJUA MAWAZO YA YEHOVA?

11. Ni maulizo gani yenye tunaweza kujiuliza wakati tunasoma ao kujifunza Biblia? (Soma kisanduku “Wakati Unajifunza Biblia, Ujiulize Hivi.”)

11 Namna gani tunaweza kujua mawazo ya Yehova? Jambo la maana zaidi lenye tunaweza kufanya ni kusoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida. Wakati tunafanya hivyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Habari hii inanifundisha nini juu ya Yehova? Sababu gani alitenda hivi?’ Na kama Daudi, tunapaswa pia kumuomba Yehova atusaidie tumujue muzuri zaidi. Daudi aliandika hivi: ‘Unijulishe njia zako, Ee Yehova; unifundishe mapito yako mwenyewe. Unitembeze katika kweli yako na kunifundisha, kwa maana wewe ni Mungu wangu wa wokovu. Nimekutumainia muchana kutwa [muchana wote].’ (Zaburi 25:4, 5) Wakati tunajifunza jambo fulani juu ya Yehova, tunaweza kufikiria hali fulani ambamo tunaweza kutumikisha habari hiyo. Je, tunaweza kutumikisha habari hiyo katika familia, kwenye kazi, kwenye masomo, ao katika kazi ya kuhubiri? Wakati tunafikiria hali fulani, itakuwa vyepesi kwetu kujua namna Yehova anapenda tutumikishe habari hiyo.

Ili tujue mawazo ya Yehova, tunapaswa kusoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida

12. Namna gani mikutano na vichapo vyetu vinatusaidia tufikie kujua mawazo ya Yehova juu ya mambo mbalimbali?

12 Njia ingine ya kujua mawazo ya Yehova ni kufuata kwa uangalifu sana mambo yenye tengenezo lake linatufundisha kutoka katika Biblia. Kwa mufano, wakati tunataka kukamata uamuzi fulani, tunaweza kutumikisha Index des Publications Watch Tower na kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova ili kujua mawazo ya Yehova. Tunaweza pia kupata faida kwenye mikutano yetu ya Kikristo wakati tunasikiliza kwa uangalifu na kutoa maelezo na wakati tunafikiri sana juu ya mambo yenye tunafundishwa. Kufanya hivyo kutatusaidia tujue mawazo ya Yehova. Kwa hiyo, tutaweza kukamata maamuzi yenye kumupendeza na yenye atabariki.

UFIKIRI SANA JUU YA MAWAZO YA YEHOVA MBELE YA KUKAMATA UAMUZI FULANI

13. Toa mufano wenye kuonyesha namna tunaweza kukamata uamuzi wa muzuri wakati tunafikiria mawazo ya Yehova.

13 Tuzungumuzie mufano fulani juu ya namna tunaweza kukamata uamuzi wa muzuri wakati tunafikiria mawazo ya Yehova. Pengine ungependa kuwa painia. Umefanya mabadiliko fulani katika maisha yako ili ukuwe na wakati mwingi wa kuhubiri. Lakini haujakuwa hakika kama utakuwa na furaha kabisa hata kama hautakuwa na feza nyingi na vitu vingi. Kwa kweli, Biblia haiseme kama tunapaswa kufanya kazi ya upainia ili kumutumikia Yehova. Tunaweza kubakia wahubiri na kuendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu. Lakini, Yesu alisema kama Yehova anabariki wale wenye kujinyima mambo fulani kwa ajili ya Ufalme. (Soma Luka 18:29, 30.) Biblia inasema pia kama Yehova anafurahi wakati tunafanya nguvu yetu yote ili kumusifu, na anapenda tumutumikie kwa furaha. (Zaburi 119:108; 2 Wakorintho 9:7) Wakati tunasali na kufikiri sana juu ya mambo hayo, tunaweza kukamata uamuzi wa muzuri katika hali fulani na wenye Yehova atabariki.

14. Namna gani unaweza kujua ikiwa muvalio fulani unafurahisha Yehova?

14 Ona mufano mwengine: Unapenda kabisa muvalio fulani, lakini unajua kama muvalio huo unaweza kukwaza ndugu ao dada fulani katika kutaniko. Biblia haiseme kitu juu ya namna hiyo ya kuvaa. Sasa, namna gani unaweza kujua mawazo ya Yehova? Biblia inatuambia hivi: ‘Wanawake wajipambe kwa mavazi yenye mupangilio muzuri, pamoja na kiasi na utimamu wa akili, si kwa mitindo ya kusuka nywele na zahabu ao lulu ao mavazi yaliyo gali sana [bei sana], bali kwa njia inayowafaa wanawake wanaodai kumuheshimu Mungu, yaani, kupitia matendo mema.’ (1 Timotheo 2:9, 10) Kwa kweli, watumishi wote wa Yehova, hata wanaume, wanaweza kujifunza jambo fulani kupitia maneno hayo. Ikiwa tuko wenye kiasi ao tunajua mipaka yetu, tunafikiria namna wengine wanaweza kujisikia ikiwa tunaamua kuvaa nguo fulani. Na kwa sababu tunapenda ndugu na dada zetu, tunaepuka kuwauzi ao kuwakwaza. (1 Wakorintho 10:23, 24; Wafilipi 3:17) Ikiwa tunafikiria mambo yenye Biblia inasema na mawazo ya Yehova, tunaweza kukamata maamuzi yenye kumupendeza.

15, 16. (a) Yehova anajisikia namna gani ikiwa tunaendelea kuwaza juu ya mambo ya uasherati (b) Wakati tunachagua mambo ya kujifurahisha, namna gani tunaweza kujua yale yenye kumupendeza Yehova? (c) Namna gani tunaweza kukamata maamuzi mazito?

15 Biblia inatuonyesha kama Yehova anaumia sana katika moyo wake na anahuzunika wakati watu wanafanya mambo ya mubaya na wakati wanafikiria mambo ya mubaya. (Soma Mwanzo 6:5, 6.) Ni wazi kama Yehova hapendi tuwazie-wazie mambo ya uasherati. Kwa kweli, ikiwa tunaendelea kuwaza juu ya mambo hayo, tunaweza kuyafanya kabisa. Lakini, Yehova anapenda tuwaze juu ya mambo ya muzuri na yenye kuwa safi. Mwanafunzi Yakobo aliandika kama hekima ya Yehova “kwanza kabisa ni safi kiadili, kisha yenye kufanya amani, yenye usawaziko, tayari kutii, yenye kujaa rehema na matunda mema, haifanyi tofauti zenye ubaguzi, si ya kinafiki.” (Yakobo 3:17) Kwa hiyo, Biblia inatufundisha kama tunapaswa kuepuka mambo yoyote ya kujifurahisha yenye yanaweza kutuchochea kuwazia-wazia mambo machafu ao ya mubaya ao kuwa na tamaa ya mambo hayo. Na ikiwa tunaelewa muzuri mambo anapenda na mambo anachukia, itakuwa vyepesi kwetu kujua ni vitabu gani tutasoma, filme gani tutaangalia, ao michezo gani tutacheza. Hatutakuwa na lazima ya kuuliza wengine mambo yenye tunapaswa kufanya.

16 Mara nyingi, kuna njia mbalimbali zenye kumufurahisha Yehova ili kutusaidia kukamata uamuzi fulani, na tunaweza kuchagua njia moja kati ya hizo. Lakini, wakati tunapaswa kukamata uamuzi muzito, inaweza kuwa muzuri kuomba mashauri kwa muzee ao ndugu ao dada fulani mwenye kukomaa kiroho. (Tito 2:3-5; Yakobo 5:13-15) Kwa kweli, hatupaswe kuomba mutu huyo atukamatie uamuzi. Lakini, tunapaswa kufikiria kwa uangalifu mambo yenye tumejifunza katika Biblia na kisha tukamate uamuzi sisi wenyewe. (Waebrania 5:14) Mutume Paulo alisema hivi: ‘Kila mumoja ataubeba muzigo wake mwenyewe.’—Wagalatia 6:5.

17. Tunapata faida gani wakati tunakamata maamuzi yenye kumupendeza Yehova?

17 Wakati tunakamata maamuzi yenye kumupendeza Yehova, tunamukaribia zaidi, anatukubali, na kutubariki. (Yakobo 4:8) Kisha imani yetu kwa Yehova itakuwa yenye nguvu zaidi. Kwa hiyo, tufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma katika Biblia ili tuelewe mawazo yake. Kwa kweli, sikuzote tutakuwa na jambo fulani mupya la kujifunza juu ya Yehova. (Ayubu 26:14) Lakini, ikiwa tunajikaza sana kujifunza juu yake leo, tutakuwa na hekima na tutaweza kukamata maamuzi ya muzuri. (Methali 2:1-5) Mawazo na mipango ya wanadamu inabadilika, lakini Yehova habadilike hata kidogo. Muandikaji mumoja wa zaburi alisema hivi: “Shauri la Yehova litasimama milele; mawazo ya moyo wake ni kwa kizazi kimoja baada ya kizazi kingine.” (Zaburi 33:11) Kwa kweli, tunaweza kukamata maamuzi ya muzuri zaidi ikiwa tunajua mawazo ya Yehova na kisha tunafanya mambo yenye kumupendeza.