Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Tupendane . . . kwa Tendo na Kweli”

“Tupendane . . . kwa Tendo na Kweli”

“Acheni tupendane, si kwa neno wala kwa ulimi, bali [lakini] kwa tendo na kweli.”​—1 YOH. 3:18.

NYIMBO: 72, 124

1. Ni upendo wa aina gani wenye kuwa mukubwa zaidi, na sababu gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

UPENDO wenye kutegemea kanuni zenye kufaa (a·gaʹpe) ni zawadi kutoka kwa Yehova. Yeye ndiye Chanzo cha upendo huo. (1 Yoh. 4:7) Upendo wa aina hiyo ndio upendo mukubwa zaidi. Hata kama upendo huo unaweza kutia ndani, kuhangaikia wengine na kuwachangamukia, unaonekana zaidi kwa matendo mazuri yenye tunafanyia wengine bila uchoyo. Kitabu kimoja kinasema kuwa a·gaʹpe “inaweza kuonekana tu kupitia matendo yenye kufanywa.” Wakati tunaonyesha ao tunaonyeshwa upendo wenye hauna uchoyo, maisha yetu yanakuwa mazuri, yanajaa furaha na yanakuwa yenye maana.

2, 3. Namna gani Yehova ameonyesha wanadamu upendo wenye hauna uchoyo?

2 Yehova alionyesha wanadamu upendo hata mbele ya kuumba Adamu na Eva. Aliumba dunia ili ikuwe makao ya milele ya mwanadamu. Zaidi ya hilo, aliiumba kwa njia yenye kufanya tufurahie kabisa maisha. Yehova alifanya hivyo kwa faida yetu, haiko kwa faida yake mwenyewe. Alionyesha pia upendo wenye hauna uchoyo wakati alibariki watoto wake duniani kwa kuwapatia tumaini la kuishi milele katika Paradiso yenye alikuwa amewatayarishia.

3 Kisha Adamu na Eva kuasi, Yehova alionyesha upendo wake mukubwa zaidi wenye hauna uchoyo. Alifanya mupango wa kukomboa wazao wa waasi hao wawili, alikuwa hakika kuwa wamoja kati yao wangekubali upendo wake. (Mwa. 3:15; 1 Yoh. 4:10) Kwa kweli, tangu wakati Yehova aliahidi kuja kwa Mukombozi, aliona kama vile zabihu hiyo ilikuwa imekwisha kutolewa. Kisha miaka 4000 hivi, Yehova alijinyima sana kwa kumutoa Mwana wake muzaliwa wa pekee kwa ajili ya wanadamu. (Yoh. 3:16) Tuko wenye shukrani sana kwa upendo wa Yehova wenye hauna uchoyo!

4. Ni nini inaonyesha kuwa wanadamu wenye hawakamilike wanaweza kuonyesha upendo wenye hauna uchoyo?

4 Tuko na uwezo wa kuonyesha upendo wenye hauna uchoyo kwa sababu Mungu alituumba kwa mufano wake. Zambi yenye tuliriti imefanya ikuwe vigumu kwetu kuonyesha upendo, lakini haijaondoa uwezo wetu wa kufanya hivyo. Abeli alionyesha upendo kwa Mungu kwa kumutolea bila uchoyo jambo la muzuri zaidi lenye alikuwa nalo. (Mwa. 4:3, 4) Noa alionyesha upendo wenye hauna uchoyo kwa wanadamu wenzake kwa kuwahubiria ujumbe wa Mungu kwa miaka mingi hata kama hawakukubali ujumbe huo. (2 Pet. 2:5) Abrahamu alitia upendo wake kwa Mungu pa nafasi ya kwanza kuliko namna alikuwa anajisikia katika moyo wake wakati aliombwa atoe mwana wake Isaka. (Yak. 2:21) Kama wanaume hao waaminifu, tunapenda kuonyesha upendo, hata kama tunapatwa na magumu.

TOFAUTI KATI YA UPENDO WA KWELI NA UPENDO WA UWONGO

5. Tunaweza kuonyesha upendo wa kweli katika njia gani?

5 Biblia inaeleza kuwa upendo wa kweli unaonyeshwa, “si kwa neno wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli.” (1 Yoh. 3:18) Hilo linamaanisha kuwa hatuwezi kuonyesha upendo kupitia maneno yetu? Hapana kabisa! (1 Tes. 4:18) Lakini, linamaanisha kuwa upendo wetu haupaswe kuonekana kwa maneno tu, zaidi sana wakati hali zinaomba kutenda kabisa. Kwa mufano, wakati Mukristo mwenzetu anakosa mambo ya lazima katika maisha, tunapaswa kufanya mengi zaidi ya kumuambia maneno yenye kutia moyo. (Yak. 2:15, 16) Vilevile, upendo wetu kwa Yehova na kwa jirani yetu unatuchochea tusiombe tu Mungu “awatume wafanyakazi katika mavuno” lakini tunapaswa pia kufanya kazi ya kuhubiri kwa bidii.​—Mt. 9:38.

6, 7. (a) “Upendo usio na unafiki” ni nini? (b) Toa mifano ya watu fulani wenye walionyesha upendo wa uwongo.

6 Mutume Yohana aliandika kuwa tunapaswa kupenda “kwa tendo na kweli.” Kwa hiyo, upendo wetu unapaswa kuwa “bila unafiki,” ao “usio na unafiki.” (Rom. 12:9; 2 Kor. 6:6) Wakati fulani mutu anaweza kufanya ionekane kuwa anaonyesha upendo. Lakini upendo wake ni wa kweli na wenye kutoka moyoni kabisa?’ Iko na nia gani? Upendo wa kweli hauwezi kuwa na unafiki. Upendo wa uwongo hauna maana.

7 Fikiria mifano fulani ya watu wenye walionyesha upendo wa uwongo. Katika shamba la Edeni, Shetani alifanya ionekane kuwa alikuwa anatafuta kabisa faida ya Eva, lakini kwa kweli matendo yake yalikuwa ya uchoyo na ya unafiki. (Mwa. 3:4, 5) Wakati Daudi alikuwa Mufalme, Ahithofeli alionyesha kuwa urafiki wake pamoja na Daudi haukukuwa wa kweli. Ahithofeli aligeuka na kuwa musaliti wakati alifikiri kuwa atapata faida fulani. (2 Sam. 15:31) Leo pia, waasi-imani na wengine wenye wanaleta migawanyiko katika kutaniko, wanatumia “maneno laini [matamu] na maneno ya kusifusifu” ili waonekane kuwa wenye upendo, lakini nia yao ya kweli ni ya uchoyo.​—Rom. 16:17, 18.

8. Tunapaswa kujiuliza ulizo gani?

8 Upendo wenye kuwa na unafiki ni wa mubaya kwa sababu ni kinyume cha upendo wa kweli. Unafiki kama huo unaweza kudanganya wanadamu, lakini hapana Yehova. Kwa kweli, Yesu alisema kama wale wenye kuwa wanafiki watapewa malipizi ‘makubwa zaidi.’ (Mt. 24:51) Bila shaka, watu wa Yehova wanaepuka kabisa kuonyesha upendo wa unafiki. Lakini, ni muzuri tujiulize hivi: ‘Upendo wangu ni wa kweli sikuzote, hauna uchoyo ao uwongo?’ Tuzungumuzie njia kenda ambamo tunaweza kujikaza kuonyesha upendo “usio na unafiki.”

NAMNA YA KUONYESHA UPENDO “KWA TENDO NA KWELI”

9. Upendo wa kweli utatuchochea kufanya nini?

9 Ufurahie kutumika hata kama wengine hawaone mambo yenye unafanya. Tunapaswa kuwa tayari kufanyia ndugu zetu matendo ya upendo “katika siri,” ao bila kuonekana na watu, wakati hilo linawezekana. (Soma Mathayo 6:1-4.) Anania na Safira walishindwa kufanya hivyo. Kuliko kufurahia kutoa bila kuonekana na watu, walidanganya juu ya kiasi cha feza zenye walitoa na walipatwa na matokeo ya mubaya kwa sababu ya unafiki wao. (Mdo. 5:1-10) Lakini, upendo wa kweli unatuchochea tufurahie kutumikia ndugu zetu bila kutangaza kwa wengine mambo yenye tulifanya. Kwa mufano, ndugu wenye kusaidia ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza kutayarisha chakula cha kiroho, wanafanya hivyo bila kujulisha majina yao, hawatafute kujulikana ao kusema mambo yenye walifanya.

10. Namna gani tunaweza kuwa wa kwanza kuonyesha wengine heshima?

10 Ukuwe wa kwanza kuonyesha wengine heshima. (Soma Waroma 12:10.) Yesu alituwekea mufano wa kuheshimia wengine kwa kufanya kazi za hali ya chini zaidi. (Yoh. 13:3-5, 12-15) Tunapaswa kujikaza sana ili kukomalisha unyenyekevu wenye tuko nao lazima ili kuonyesha wengine heshima kwa njia hiyo. Hata mitume walielewa namna ya kuiga mufano wa Yesu kisha kupokea roho takatifu. (Yoh. 13:7) Tunaweza kuonyesha wengine heshima kwa kuepuka kujiona kuwa wa maana sana kwa sababu ya masomo yetu, vitu vyetu vya kimwili, ao mapendeleo yetu katika kazi ya Yehova. (Rom. 12:3) Pia, hatupaswe kusikilia wivu wale wenye kusifiwa, lakini tunafurahi pamoja nao hata kama tunaona kuwa sisi pia tunapaswa kusifiwa kama wao ao sisi pia tulichangia ili kutimiza jambo fulani.

11. Sababu gani tunapaswa kupongeza wengine kwa moyo wote?

11 Upongeze ndugu zako kwa moyo wote. Tunapaswa kutafuta nafasi za kupongeza wengine kwa sababu kufanya hivyo ni muzuri kwa “ajili ya kujenga.” (Efe. 4:29) Lakini, tunapaswa kufanya hivyo kwa moyo wetu wote. Kama hatufanye hivyo kwa moyo wote, tutakuwa tunasifusifu mutu ao kuepuka daraka letu la kumutolea mashauri ikiwa inaomba kufanya hivyo. (Met. 29:5) Ikiwa tunapongeza mutu fulani na kisha tunaanza kumusema mubaya kwa wengine, tunatenda kwa unafiki. Mutume Paulo aliepuka mutego huo na alituwekea mufano muzuri wa kuonyesha upendo wa kweli katika njia yenye alipongeza wengine. Kwa mufano, alipongeza kwa moyo wote Wakristo wa Korintho juu ya mwenendo wao fulani. (1 Kor. 11:2) Lakini wakati matendo yao hayakustahili pongezi, aliwafasiria sababu gani kwa upole na waziwazi.​—1 Kor. 11:20-22.

Kusaidia ndugu zetu wenye kuwa katika uhitaji ni njia moja ya kuonyesha upendo na ukaribishaji-wageni (Picha hizi zinapatana na fungu la 12)

12. Namna gani tunaweza kuonyesha upendo wa kweli wakati tunaonyesha ukaribishaji-wageni?

12 Ukuwe mukaribishaji-wageni. Yehova anatuomba tuonyeshe ndugu na dada zetu ukarimu. (Soma 1 Yohana 3:17.) Lakini, tunapaswa kufanya hivyo kwa nia ya muzuri na kwa moyo wote. Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ninaonyesha kwanza ukaribishaji-wageni kwa marafiki wangu wa sana, wale wenye ninaona kuwa wa maana katika kutaniko, ao wale wenye wanaweza kunirudishia kwa njia fulani? Ao ninatafuta njia za kuonyesha ukarimu kwa ndugu na dada wenye sijue muzuri ao wale wenye hawana kitu cha kunirudishia?’ (Lu. 14:12-14) Wazia kuwa ndugu iko na lazima ya musaada kwa sababu alikamata maamuzi yenye kukosa hekima, ao anashindwa kutushukuru kwa sababu ya ukaribishaji-wageni wenye tulimuonyesha. Katika hali kama hizo, tunapaswa kutumikisha shauri hili: ‘Mukaribishane bila kunungunika.’ (1 Pet. 4:9) Ikiwa unafuata shauri hilo, utapata furaha yenye mutu anapata wakati anatoa na nia ya muzuri.​—Mdo. 20:35.

13. (a) Ni wakati gani inaweza kuwa vigumu zaidi kusaidia wale wenye kuwa zaifu? (b) Tunaweza kufanya nini ili kutegemeza wale wenye kuwa zaifu?

13 Utegemeze wale wenye kuwa zaifu. Amri hii ya Biblia inaweza kuonyesha ikiwa upendo wetu ni wa kweli: ‘Mutegemeze walio zaifu, mukuwe wenye ustahimilivu [uvumilivu] kuelekea wote.’ (1 Tes. 5:14) Hata kama wengi wenye kuwa zaifu wanafikia kuwa na imani yenye nguvu, wengine wako na lazima tuwaonyeshe uvumilivu, na tuendelee kuwategemeza. Tunaweza kufanya hivyo kwa kuzungumuza nao juu ya mawazo ya Maandiko yenye kujenga, kuwaalika ili tuhubiri pamoja nao, ao kuchukua tu nafasi ya kuwasikiliza. Pia, kuliko tu kufikiri kuwa ndugu ao dada fulani iko “nguvu” kiroho ao “zaifu,” tunapaswa kukumbuka kuwa kila mumoja wetu iko na sifa za muzuri na uzaifu wake. Hata mutume Paulo alikubali kwamba alikuwa na uzaifu. (2 Kor. 12:9, 10) Kwa hiyo, sisi wote tuko na lazima ya kutegemezwa na Wakristo wenzetu.

14. Tunapaswa kuwa tayari kufanya nini ili kuendeleza amani pamoja na ndugu zetu?

14 Ufanye amani. Tunapaswa kufanya yetu yote ili kuendelea kuwa na amani pamoja na ndugu zetu, hata wakati tunafikiri kuwa wengine wanatuelewa mubaya ao tumetendewa bila haki. (Soma Waroma 12:17, 18.) Kuomba musamaha kunaweza kusaidia mutu mwenye tulikosea ajisikie muzuri, lakini tunapaswa kufanya hivyo kwa moyo wote. Kwa mufano, kuliko kusema, “Unisamehe juu unajisikia mubaya,” unaweza kukubali kosa lako na kusema, “Unisamehe juu mambo yenye nilisema yalikuumiza.” Amani ni ya maana sana katika ndoa. Wakati bibi na bwana wako mbele ya watu hawapaswe kufanya ionekane kuwa wanapendana, lakini wakati wako wao wenyewe hawasemeshane, ao wanatumia maneno makali ao kutendeana kwa jeuri ili kuumizana.

15. Namna gani tunaweza kuonyesha kuwa tumesamehe kwa moyo wote?

15 Ukuwe tayari kusamehe. Tunasamehe wakati tunahurumia mutu mwenye alitukosea na kuepuka kumuwekea kinyongo. Kwa ‘kuvumiliana katika upendo, kujitahidi [kujikaza] sana kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani,’ tunaweza kuwa tayari kusamehe wale wenye wanaweza kukosa kujua kuwa wametukosea. (Efe. 4:2, 3) Ili musamaha wetu ukuwe wa kweli, tunapaswa kuzuia mawazo yetu ili ‘tusiweke hesabu ya ubaya.’ (1 Kor. 13:4, 5) Ikiwa tunawekea wengine kinyongo ao kasirani, tunaweza kuharibu urafiki wetu pamoja na ndugu na dada zetu, lakini pia urafiki wetu pamoja na Yehova. (Mt. 6:14, 15) Tunaweza pia kuonyesha kuwa tumesamehe kwa moyo wote kwa kusali kwa ajili ya wale wenye kutukosea.​—Lu. 6:27, 28.

16. Namna gani tunapaswa kuona migawo yetu katika kazi ya Yehova?

16 Usitafute faida zako mwenyewe. Ikiwa tunapata mapendeleo katika kazi ya Yehova, tunapaswa kuona mapendeleo hayo kuwa nafasi ya kuonyesha kuwa upendo wetu ni wa kweli kwa ‘kutafuta, si faida [yetu] wenyewe, bali ile ya yule mutu mwingine.’ (1 Kor. 10:24) Kwa mufano, kwenye mikusanyiko yetu, wakaribishaji wanafika nafasi ya kufanyia mukusanyiko mbele ya wengine. Kuliko kuona kuwa mugawo wao unawatolea nafasi ya kupata viti vya muzuri zaidi kwa ajili yao na watu wa familia zao, wengi kati ya ndugu hao wanachagua kukaa kwenye viti vya hali ya chini vyenye kuwa mahali penye wanatumikia. Kwa kutafuta faida ya wengine katika njia hiyo, wanaonyesha upendo wenye hauna uchoyo hata kidogo. Namna gani unaweza kuiga mufano wao muzuri?

17. Ikiwa mutu amefanya zambi nzito, upendo wa kweli utamuchochea kufanya nini?

17 Utubu na uache kufanya zambi kwa siri. Wakristo fulani wenye wamefanya zambi nzito wanajaribu kuificha ili kuepuka kujipatisha haya ao kuvunja wengine moyo. (Met. 28:13) Lakini, kufanya hivyo ni kukosa upendo kwa sababu kunaumiza mutenda zambi na wengine pia. Hilo linaweza kufanya roho ya Mungu isitende juu ya kutaniko na linaweza kuvuruga amani ya kutaniko lote. (Efe. 4:30) Upendo wa kweli unachochea Wakristo wenye wamefanya zambi nzito wazungumuze na wazee ili wawapatie musaada wenye wako nao lazima.​—Yak. 5:14, 15.

18. Sababu gani upendo wa kweli ni wa maana sana?

18 Kati ya sifa zote, upendo ndio sifa kubwa zaidi. (1 Kor. 13:13) Ni alama yenye kuonyesha kuwa tuko wanafunzi wa Yesu na waigaji wa Yehova, Chanzo cha upendo. (Efe. 5:1, 2) Paulo aliandika hivi: “Ikiwa . . . sina upendo, mimi si kitu.” (1 Kor. 13:2) Tuendelee basi kuonyesha upendo hapana “kwa neno” tu lakini pia “kwa tendo na kweli.”