Ya Kwanza ya Yohana 3:1-24

  • Sisi ni watoto wa Mungu (1-3)

  • Tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi (4-12)

    • Yesu atavunja kazi za Ibilisi (8)

  • Mupendane (13-18)

  • Mungu ni mukubwa kuliko mioyo yetu (19-24)

3  Muone namna ya upendo wenye Baba ametupatia sisi,+ kwamba tuitwe watoto wa Mungu!+ Na ni vile tuko. Ndiyo sababu ulimwengu hautujue,+ kwa sababu haumujue yeye.+ 2  Wapendwa, sasa sisi ni watoto wa Mungu,+ lakini bado haijafunuliwa namna tutakuwa.+ Tunajua kama wakati atafunuliwa tutakuwa kama yeye, kwa sababu tutamuona vile iko.* 3  Na kila mutu mwenye kuwa na tumaini hili ndani yake anajisafisha,+ kama vile huyo iko* safi. 4  Kila mutu mwenye anazoea kufanya zambi anaendelea pia kufanya uvunjaji wa sheria, na zambi ni uvunjaji wa sheria. 5  Munajua pia kama alifunuliwa ili kutosha zambi zetu,+ na hakuna zambi ndani yake. 6  Kila mutu mwenye anakaa katika umoja naye haendelee kufanya zambi;+ hakuna mutu mwenye anazoea kufanya zambi mwenye amemuona ao kumujua. 7  Watoto wadogo, mutu yeyote asiwapotoshe ninyi; mutu mwenye anazoea kutenda haki ni mwenye haki, kama vile huyo ni mwenye haki. 8  Mutu mwenye anazoea kufanya zambi anatokana na Ibilisi, kwa sababu Ibilisi amekuwa akifanya zambi tangu mwanzo.*+ Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alifunuliwa, ili avunje* kazi za Ibilisi.+ 9  Kila mutu mwenye amezaliwa kutokana na Mungu hazoee kufanya zambi,+ kwa sababu mbegu* Yake inakaa ndani ya mutu huyo, na hawezi kuwa na mazoea ya kufanya zambi, kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.+ 10  Watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi wanaonekana kupitia jambo hili: Mutu yeyote mwenye hazoee kutenda haki hatokane na Mungu, na pia ule mwenye hamupendi ndugu yake.+ 11  Kwa maana huu ndio ujumbe wenye mumesikia tangu mwanzo, kwamba tunapaswa kupendana;+ 12  hapana kama Kaini, mwenye alitokana na ule muovu na akamuua ndugu yake.+ Na sababu gani alimuua? Kwa sababu matendo yake mwenyewe yalikuwa maovu,+ lakini matendo ya ndugu yake yalikuwa ya haki.+ 13  Ndugu, musishangae kwamba ulimwengu unawachukia ninyi.+ 14  Tunajua kama tumevuka kutoka kifo mupaka uzima,+ kwa sababu tunapenda ndugu.+ Mutu mwenye hapendi anakaa katika kifo.+ 15  Kila mutu mwenye anamuchukia ndugu yake ni muuaji,+ na munajua kama hakuna muuaji mwenye uzima wa milele unakaa ndani yake.+ 16  Kupitia jambo hili, sisi tumejua upendo, kwa sababu huyo alitoa uzima wake* kwa ajili yetu,+ na sisi tunalazimika kutoa uzima wetu* kwa ajili ya ndugu zetu.+ 17  Lakini kama mutu yeyote iko* na vitu vya ulimwengu huu na anaona ndugu yake katika uhitaji lakini anakataa kumuonyesha huruma, namna gani upendo wa Mungu unakaa ndani yake?+ 18  Watoto wadogo, tunapaswa kupendana, hapana kwa neno ao kwa ulimi,+ lakini kwa tendo+ na kweli.+ 19  Kwa jambo hili tutajua kama tunatokana na kweli, na tutahakikishia* mioyo yetu mbele yake 20  juu ya jambo lolote lenye pengine mioyo yetu inaweza kutuhukumu, kwa sababu Mungu ni mukubwa kuliko mioyo yetu na anajua mambo yote.+ 21  Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tuko na uhuru wa kusema mbele ya Mungu;+ 22  na chochote chenye tunaomba tunakipokea kutoka kwake,+ kwa sababu tunashika amri zake na tunafanya mambo yenye kupendeza mbele ya macho yake. 23  Kwa kweli, hii ndiyo amri yake: kwamba tukuwe na imani katika jina la Mwana wake Yesu Kristo+ na tupendane,+ kama vile alitupatia amri. 24  Zaidi ya hayo, mutu mwenye anashika amri zake anakaa katika umoja naye, na yeye anakaa katika umoja na mutu huyo.+ Na kupitia roho yenye alitupatia, tunajua kama anakaa katika umoja na sisi.+

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “aharibu.”
Ao “tangu wakati alianza.”
Ni kusema, mbegu yenye inaweza kuzaa, ao kutoa matunda.
Ao “nafsi yake.”
Ao “nafsi yetu.”
Ao “eko.”
Ao “tutashawishi; tutasadikisha.”