HABARI JUU YA MAISHA YA WATU
Kufanya Mambo Yenye Yehova Anaomba Kunaleta Baraka
“Tutafanya vile!” Ni vile mimi na bwana yangu pamoja na kaka yangu na bibi yake tulijibia wakati tulisikia mualiko wa kutimiza mugawo fulani. Sababu gani tulikubali mugawo huo, na namna gani Yehova alitubariki? Acha kwanza niwaelezee namna nilikomaa.
NILIZALIWA katika mwaka wa 1923 katika Hemsworth, muji wenye kuwa katika Yorkshire, Uingereza. Nilikuwa na kaka yangu mumoja mukubwa, Bob. Wakati nilikuwa na miaka kenda hivi, baba yetu mwenye alichukia unafiki wa dini, alipata vitabu fulani vyenye kufunua mafundisho ya uongo ya dini. Aliguswa sana na mambo yenye alisoma. Kisha miaka fulani, Bob Atkinson alitutembelea na akatuwekea kwenye fono hotuba moja ya Ndugu Rutherford yenye kurekodiwa ili tuisikilize. Tulitambua kuwa mafundisho hayo yalitoka kwa watu walewale wenye walichapisha vitabu hivyo! Wazazi wangu walimuomba Ndugu Atkinson akule pamoja na sisi chakula cha mangaribi kila siku na kujibia maulizo mengi ya Biblia yenye tulikuwa nayo. Tulialikwa kuhuzuria mikutano katika nyumba ya ndugu mumoja kwenye umbali wa kilometre fulani. Tulikubali mara moja na kutaniko ndogo lilianzishwa katika Hemsworth. Bila kukawia tulikuwa tunapangisha watumishi wa kanda (leo wanaitwa waangalizi wa muzunguko) na kualika mapainia wenye kuwa katika maeneo ya karibu-karibu ili wakule chakula pamoja na sisi. Kupitisha wakati pamoja nao kulikuwa na matokeo makubwa juu yangu.
Tulikuwa tumeanza kufanya biashara, lakini baba yangu aliambia kaka yangu hivi: “Ikiwa unapenda kuenda kufanya kazi ya upainia, tutaachana na biashara hii.” Bob alikubali, na aliondoka nyumbani na kuenda kufanya kazi ya upainia wakati alikuwa na miaka 21. Kisha miaka mbili, wakati nilikuwa na miaka 16 nikakuwa painia. Katika mwisho wa juma nilihubiri pamoja na wengine, lakini mara nyingi katikati ya juma, nilihubiri peke yangu kwa kutumia karte ya kutoa ushahidi na fono. Hata hivyo, Yehova alinibariki kwa kunisaidia kupata mwanafunzi wa Biblia mwenye alifanya maendeleo ya muzuri sana. Watu wengi wa familia ya mwanafunzi huyo walifikia kuwa Mashahidi. Mwaka wenye ulifuata, niliwekwa kuwa painia wa pekee pamoja na Mary Henshall. Tulitumwa katika eneo la Cheshire lenye lilikuwa halijahubiriwa.
Ilikuwa katikati ya Vita ya Pili ya Ulimwengu na wanawake waliombwa kuunga mukono vita. Kwa sababu tulikuwa watumishi wa wakati wote, sisi mapainia wa pekee tulifikiri kuwa hatutaombwa kufanya hivyo kama vile watumishi wa dini zingine. Lakini tribinali Isa. 41:10, 13.
haikukubali; kwa hiyo, nilihukumiwa kufungwa katika gereza kwa siku 31. Mwaka wenye ulifuata, wakati nilieneza miaka 19, nilijiandikisha kuwa mutu mwenye kukataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri yangu. Nilipelekwa kwenye tribinali mbili, lakini mashitaka yangu yalifutwa. Hata kama nilipatwa na magumu hayo, nilijua kuwa roho takatifu ilikuwa inanisaidia na kuwa Yehova alikuwa anakamata mukono wangu, na kunifanya nikuwe imara na mwenye nguvu.—NINAPATA MUTU MWINGINE WA KUTUMIKA NAYE
Mimi na Arthur Matthews tulikutana katika mwaka wa 1946. Kisha tu kufungwa katika gereza kwa miezi tatu kwa sababu zamiri yake haikumuruhu kuingia katika jeshi, alijiunga na mudogo yake Dennis, mwenye alikuwa painia wa pekee katika Hemsworth. Tangu wakati walikuwa watoto, baba yao alikuwa amewafundisha juu ya Yehova na walibatizwa wakati walikuwa vijana. Bila kukawia Dennis alipewa mugawo wa kutumikia katika Irelandi; kwa hiyo, alimuacha Arthur bila mutu wa kutumika naye. Wazazi wangu walipendezwa na tabia ya Arthur, mwenye alikuwa kijana painia mwenye bidii; kwa hiyo, walimuomba akuje kuishi kwetu. Wakati nilikuwa ninakuja kuwatembelea, mimi na Arthur tulikuwa tunajitolea kusafisha masahani kisha kula. Mwishowe, tukaanza kuandikiana. Katika mwaka wa 1948, Arthur alifungwa tena kwa miezi tatu. Tulifunga ndoa katika Mwezi wa 1, 1949, na tulikuwa na muradi wa kubakia katika utumishi wa wakati wote kadiri ingewezekana. Kwa baraka ya Yehova na kujipanga muzuri, tulitumia kipindi cha mapumuziko ili kutumika katika shamba la mavuno ya matunda, ili tupate feza za kutusaidia kuendelea kufanya kazi ya upainia.
Katika Hemsworth muda mufupi kisha ndoa yetu katika mwaka wa 1949
Kisha zaidi ya mwaka mumoja, tuliombwa tuende katika Irelandi ya Kaskazini, kwanza katika Armagh na kisha katika Newry, watu wengi wa miji hiyo mbili walikuwa wa dini ya Katoliki. Watu walituchukia sana katika eneo hilo, na tulipaswa kuwa waangalifu wakati tulikuwa tunazungumuza na watu. Mikutano ilikuwa inafanywa katika nyumba ya ndugu fulani na bibi yake yenye ilikuwa kwenye umbali wa kilometre 16 kutoka mahali penye tulikuwa tunaishi. Watu munane hivi walikuwa wanahuzuria. Wakati tuliombwa tulale kwao, tulikuwa tunalala chini na kesho asubuhi tulikuwa tunakula chakula kizuri. Ninafurahi sana kujua kuwa sasa kuko Mashahidi wengi katika eneo hilo.
“TUTAFANYA VILE!”
Kaka yangu na bibi yake Lottie, walikuwa tayari mapainia wa pekee katika Irelandi ya Kaskazini, na katika mwaka wa 1952 sisi waine tulihuzuria mukusanyiko wa wilaya katika Belfast. Ndugu fulani alitupangisha pamoja na Pryce Hughes, mwenye alikuwa mutumishi wa tawi ya Uingereza wakati huo. Usiku mumoja, tulizungumuzia kutolewa kwa kijitabu La voie de Dieu est une voie d’amour, chenye kilitolewa zaidi sana kwa ajili ya watu wa Irelandi. Ndugu Hughes alizungumuzia magumu ya kuhubiria Wakatoliki katika inchi ya Irelandi. Ndugu walikuwa wanafukuzwa katika nyumba zao na kutendewa kwa jeuri na vikundi vya watu wenye walichochewa na mapadri. Pryce alisema hivi: “Tuko na lazima ya bibi na bwana wenye kuwa na motokari ili wafanye kampanye ya pekee ya kugawia watu kijitabu hicho katika inchi yote.” * Mara moja tulijibia, “Tutafanya vile!” Hayo ndiyo maneno nilisema kwenye mwanzo wa habari hii.
Pamoja na mapainia wenzetu kwenye pikipiki yenye kuwa na motokari ya kukokotwa pembeni
Mahali moja kwenye mapainia wangeweza kubakia katika Dublin ilikuwa katika nyumba ya Ma Rutland, dada mwaminifu wa muda murefu. Kisha kupita hapo na kisha kuuzisha vitu vyetu fulani, sisi wote tuliingia kwenye pikipiki (moto) ya Bob yenye ilikuwa na motokari ya pembeni ya kukokotwa. Tulipata motokari ya muzuri yenye ilikuwa imekwisha kutumiwa na tukaomba mutu mwenye tuliuzia atuletee motokari hiyo kwa sababu sisi wote hatukujua kutembeza. Usiku huo wote Arthur alikuwa anakaa kwenye kitanda na kufanya kama vile alikuwa anabadilisha mwendo wa motokari. Asubuhi yenye ilifuata wakati alikuwa anajaribu kutosha motokari hiyo mahali pa kuwekea motokari, dada misionere Mildred Willett (mwenye alifikia kuwa bibi ya John Barr) alikuja. Alikuwa anajua kutembeza motokari! Alitusaidia kufanya mazoezi ya kutembeza motokari, na kisha hapo tulikuwa tayari kuenda!
Motokari yetu na nyumba yetu ya kukokotwa
Kisha, tulikuwa na lazima ya mahali pa kuishi. Tulikuwa tumeambiwa kuwa tuepuke kuishi katika nyumba ya kukokotwa kwa sababu maadui zetu wangeiunguza, kwa hiyo, tulitafuta nyumba lakini hatukupata. Usiku huo, sisi waine tulilala katika motokari. Siku yenye ilifuata, tuliweza tu kupata nyumba fulani ya kukokotwa yenye ilikuwa imetengenezwa nyumbani na yenye ilikuwa na vitanda viwili vidogo-vidogo vyenye kubebana. Hiyo ikakuwa nyumba yetu. Jambo la kushangaza ni kwamba, hatukukuwa na matatizo ya kuacha nyumba hiyo katika mashamba ya watu wenye moyo muzuri. Tulihubiria eneo lenye lilikuwa kwenye umbali wa kati ya kilometre 16 na 24. Na kisha kuhubiri huko, tulikuwa tunarudia ili kuhubiria wale wenye kuwa katika eneo ambamo tulikuwa tumeacha nyumba yetu.
Tulitembelea maeneo yote yenye kuwa katika sehemu ya kusini-mashariki mwa inchi hiyo bila magumu mengi, na tuligawia watu zaidi ya vijitabu 20000 na tukapatia tawi ya Uingereza majina ya watu wenye walikuwa wamependezwa. Ni baraka kubwa sana kuona kuwa leo kuko mamia ya Mashahidi katika eneo hilo!
KURUDIA UINGEREZA KISHA KUENDA ÉCOSSE
Kisha, tulipewa mugawo wa kutumikia tena kusini mwa muji wa Londres. Kisha majuma kidogo, biro ya tawi ya Uingereza iliita Arthur na kumuomba aanze kufanya kazi ya muzunguko siku yenye ilifuata! Kisha kuzoezwa kwa juma moja, tulisafiri na kuenda katika muzunguko wetu katika Écosse. Arthur hakukuwa na wakati wa kutayarisha hotuba zake, lakini roho yake ya kuwa tayari kupambana na magumu katika kazi ya Yehova ilinitia moyo sana. Tulifurahia sana mugawo wetu katika kazi ya muzunguko. Tulikuwa tumetumikia kwa miaka fulani katika eneo lenye halikukuwa limehubiriwa, na sasa ilikuwa baraka kubwa sana kuwa kati ya ndugu na dada wengi.
Wakati Arthur alipata mualiko wa kusoma Masomo ya Gileadi kwa miezi kumi katika mwaka wa 1962, tulipaswa kukamata uamuzi muzito. Mwishowe tuliamua kuwa hata kama ningebakia, ilikuwa muzuri Arthur akubali pendeleo hilo. Kwa sababu ningebakia peke yangu, nilitumwa tena kuwa painia wa pekee katika Hemsworth. Kisha mwaka mumoja, wakati Arthur alirudia tulipewa mugawo wa kufanya kazi ya wilaya yenye ilichukua eneo la Écosse, kaskazini mwa Uingereza, na Irelandi ya Kaskazini.
MUGAWO MUPYA KATIKA IRELANDI
Katika mwaka wa 1964, Arthur alipewa mugawo mupya wa kuwa mutumishi wa tawi katika inchi ya Irelandi. Tulifurahia sana kazi ya kusafiri, kwa hiyo, mwanzoni nilikuwa na wasiwasi juu ya mabadiliko hayo. Wakati ninakumbuka, niko mwenye shukrani kwa sababu nilipewa pendeleo la kutumika kwenye Beteli. Ninaamini kuwa ikiwa unakubali mugawo fulani hata kama hauufurahie, kwa kweli, utabarikiwa sikuzote na Yehova. Katika Beteli nilifanya kazi ya kutumika katika biro, kupakiza vitabu, kupika, na kufanya usafi. Wakati fulani, tulikuwa tunafanya pia kazi ya wilaya na tuliweza kukutana na ndugu katika inchi yote. Jambo hilo, na pia kuona wanafunzi wetu wa Biblia wanafanya maendeleo, kulifanya tuungane kabisa pamoja na familia yetu ya kiroho katika Irelandi. Hiyo ni baraka kubwa sana!
TUKIO LA MAANA KATIKA HISTORIA YA KITEOKRASI YA IRELANDI
Mukusanyiko wa kwanza wa kimataifa katika Irelandi ulifanywa Dublin katika mwaka wa 1965. * Hata kama tulipingwa sana katika kila njia, mukusanyiko huo ulikuwa na matokeo ya muzuri sana. Watu 3948 walihuzuria, na watu 65 walibatizwa. Wale wote wenye walipangisha watu 3500 wenye walitoka katika inchi zingine ili kuja kwenye mukusanyiko huo, walipokea barua ya shukrani. Wenye waliwapangisha wao pia walisifu mwenendo wa wale wenye walikuja kwenye mukusanyiko huyo. Kwa kweli, hilo lilikuwa tukio la maana katika Irelandi.
Arthur anasalimia Ndugu Nathan Knorr wakati anafika kwa ajili ya mukusanyiko wa mwaka wa 1965
Arthur anatangaza kutolewa kwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia katika luga ya Kiselti katika mwaka wa 1983
Katika mwaka wa 1966 Irelandi ya kaskazini na kusini zilianza kuongozwa na biro ya tawi ya Dublin; hiyo ilikuwa tofauti kabisa na migawanyiko ya politike na ya dini katika kisiwa hicho. Tulifurahi sana kuona Wakatoliki wengi wanakuwa Mashahidi na wanatumika pamoja na ndugu wenye zamani walikuwa Waprotestanti.
MUGAWO WETU UNABALIKA KABISA
Katika mwaka wa 2011 maisha yetu yalibadilika kabisa wakati tawi ya Uingereza na ya Irelandi zilitiwa pamoja na tukapewa mugawo wa kutumikia kwenye Beteli ya Londres. Habari hiyo ilikuja katika kipindi chenye nilikuwa nimeanza kuwa na wasiwasi juu ya afya ya Arthur. Wanganga walivumbua kuwa alikuwa na ugonjwa wa kutetemeka (Parkinson). Tarehe 20 Mwezi wa 5, 2015, bwana yangu wa miaka 66 alikufa.
Katika miaka fulani yenye imepita, nimevunjika moyo, nimeshuka moyo, na nimekuwa na huzuni. Zamani, sikuzote Arthur alikuwa ananisaidia. Ninamukumbuka sana! Lakini wakati unapatwa na hali kama hizo, unamukaribia Yehova zaidi. Nimetiwa pia moyo sana kujua kuwa Arthur alikuwa anapendwa sana. Nimepata barua kutoka kwa marafiki katika Irelandi, Uingereza, na hata kutoka Amerika. Barua hizo, na vitia moyo kutoka kwa Dennis mudogo ya Arthur, na bibi yake, Mavis, na Ruth na Judy, watoto wa kaka yangu, vimenisaidia sana.
Andiko lenye limenitia sana moyo ni Isaya 30:18. Linasema hivi: ‘Yehova ataendelea kutarajia kuwaonyesha ninyi kibali, na kwa hiyo atasimama ili kuwaonyesha ninyi rehema. Kwa maana Yehova ni Mungu wa hukumu. Wenye furaha ni wale wote wanaoendelea kumutarajia [kumungojea].’ Nimefarijiwa sana kujua kuwa Yehova anangojea kwa hamu ili kutengeneza mambo na kutupatia migawo yenye kufurahisha katika dunia mupya.
Wakati ninakumbuka maisha yetu, ninaona namna Yehova ameongoza na kubariki kazi katika Irelandi! Ninajisikia kuwa nilikuwa na pendeleo kubwa sana la kutoa muchango mudogo katika maendeleo hayo ya kiroho. Bila shaka, kufanya mambo yenye Yehova anatuomba kunaleta baraka sikuzote.