Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Miujiza Ambayo Itatukia Hivi Karibuni

Miujiza Ambayo Itatukia Hivi Karibuni

Miujiza Ambayo Itatukia Hivi Karibuni

UNGEHISIJE ikiwa ungetambua kwamba daktari ambaye alikuwa amepangiwa kukufanyia upasuaji mkubwa hajawahi kufanya upasuaji kama huo? Ni wazi kwamba ungekuwa na wasiwasi mwingi. Lakini kwa upande mwingine, ungehisije ikiwa ungetambua kwamba daktari huyo alikuwa stadi katika kazi yake na alikuwa amewahi kufanya mamia ya upasuaji kama huo na akafaulu? Bila shaka, ungekuwa na uhakika kwelikweli kwamba anaweza kukusaidia.

Ulimwengu huu mwovu unahitaji kufanyiwa “upasuaji” mkubwa sana. Kupitia Neno lake Biblia, Yehova Mungu ameahidi kwamba atarudisha dunia hii kuwa Paradiso. (2 Petro 3:13) Lakini ili iwe hivyo, kwanza lazima uovu uondolewe, ukatiliwe mbali kabisa. (Zaburi 37:9-11; Methali 2:21, 22) Mambo yote yenye kuhuzunisha tunayoona leo, lazima yaondolewe kabla ya paradiso kurudishwa duniani. Muujiza utahitajika ili jambo hilo litukie!​—Ufunuo 21:4, 5.

Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba mabadiliko hayo makubwa yatatukia hivi karibuni. Kwa nini? Kwa sababu miujiza ambayo tayari Yehova Mungu amefanya inathibitisha kwamba ana nguvu za kutimiza ahadi zake. Linganisha miujiza sita tu kati ya mingi inayotajwa katika Biblia na ahadi za wakati ujao ambazo inatoa.

Endelea kujifunza kuhusu ahadi za wakati wetu ujao zinazotajwa katika Biblia. Kadiri imani yako inavyoimarika ndivyo tumaini lako litakavyoongezeka—tumaini la kuishi wakati ambao wewe mwenyewe utafaidika kutokana na miujiza ambayo Yehova anafanya.

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 9, 10]

MUUJIZA:

YESU ALILISHA MAELFU YA WATU KWA MIKATE NA SAMAKI WACHACHE.​—MATHAYO 14:13-21; MARKO 8:1-9; YOHANA 6:1-14.

AHADI:

“Hakika dunia itatoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, atatubariki.”​ZABURI 67:6.

INAMAANISHA NINI?

HAKUNA MTU ATAKAYETESEKA TENA KWA SABABU YA NJAA.

MUUJIZA:

YESU ALIWAPONYA VIPOFU.​—MATHAYO 9:27-31; MARKO 8:22-26.

AHADI:

Macho ya vipofu yatafunguliwa.”​—ISAYA 35:5.

INAMAANISHA NINI?

VIPOFU WOTE WATAKUWA NA UWEZO WA KUONA.

MUUJIZA:

YESU ALIPONYA VILEMA.​—MATHAYO 11:5, 6; YOHANA 5:3-9.

AHADI:

“Kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya.”​ISAYA 35:6.

INAMAANISHA NINI?

VILEMA WOTE WATAPONYWA.

MUUJIZA

YESU ALIPONYA MAGONJWA MBALIMBALI.​—MARKO 1:32-34; LUKA 4:40.

AHADI:

“Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’”​ISAYA 33:24.

INAMAANISHA NINI?

MAGONJWA YOTE YENYE KUDHOOFISHA YATAONDOLEWA. TUTAFURAHIA AFYA KAMILI.

MUUJIZA:

YESU ALIDHIBITI NGUVU ZA ASILI.​—MATHAYO 8:23-27; LUKA 8:22-25.

AHADI:

“Hakika wao watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatafanya kazi ya bure.”​ISAYA 65:21, 23.

“Utakuwa mbali sana na ukandamizaji—kwa maana hutaogopa yeyote—na jambo lolote lenye kutia hofu, kwa maana halitakuja karibu nawe.”​ISAYA 54:14.

INAMAANISHA NINI?

MISIBA YA ASILI HAITAKUWAPO TENA.

MUUJIZA:

YESU ALIFUFUA WAFU.​—MATHAYO 9:18-26; LUKA 7:11-17.

AHADI:

‘Wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho watatoka.’ YOHANA 5:28, 29.

“Bahari ikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi vikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake.”UFUNUO 20:13.

INAMAANISHA NINI?

WAPENDWA WETU WALIOKUFA WATAFUFULIWA.