2 Samweli 22:1-51
22 Na Daudi akamwambia Yehova maneno ya wimbo+ huu siku ambayo Yehova alikuwa amemkomboa kutoka katika mkono wa adui+ zake wote na kutoka katika mkono wa Sauli;+
2 naye akasema:“Yehova ni mwamba+ wangu na ngome+ yangu na Mwokoaji wangu.+
3 Mungu wangu ni mwamba+ wangu. Nitamkimbilia,Ngao+ yangu na pembe+ yangu ya wokovu, kilele+ changu salama,Na mahali pangu pa kukimbilia,+ Mwokozi+ wangu; unaniokoa kutoka katika jeuri.+
4 Nitamwita, Yehova, Yule anayestahili kusifiwa,+Nami nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.+
5 Kwa maana mashuu yanayosababisha kifo yalinizunguka;+Kulikuwa na mafuriko ya ghafula ya watu wasiofaa kitu yaliyoendelea kuniogopesha.+
6 Kamba za Kaburi* zilinizunguka;+Mitego ya kifo ilinikabili.+
7 Katika taabu yangu niliendelea kumwita Yehova,+Nami niliendelea kumwita Mungu wangu.+Ndipo kutoka katika hekalu lake akaisikia sauti yangu,+Kilio changu cha kuomba msaada kikaingia masikioni mwake.+
8 Nayo dunia ikaanza kutikisika na kutetemeka;+Misingi ya mbingu ikasukasuka,+Nayo ikatikisika-tikisika kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
9 Moshi ukapanda katika mianzi ya pua yake, na moto kutoka kinywani mwake ukaendelea kuteketeza;+Makaa yakawaka moto kutoka kwake.+
10 Naye akaziinamisha mbingu, akashuka;+Na giza zito lilikuwa chini ya miguu yake.+
11 Naye akaja akiwa amepanda juu ya kerubi,+ akaja akiwa anaruka;Naye akaonekana juu ya mabawa ya roho.+
12 Ndipo akaweka giza kumzunguka kama vibanda,+Maji yenye giza, mawingu mazito.+
13 Kutoka katika mwangaza mbele yake yakawaka makaa yanayowaka ya moto.+
14 Yehova akaanza kunguruma+ kutoka mbinguni,Na Aliye Juu Zaidi akaanza kutoa sauti yake.+
15 Naye akaendelea kuitupa mishale, ili awatawanye;+Umeme, ili awavuruge.+
16 Na sakafu za vijito vya bahari zikaonekana,+Misingi ya nchi yenye kuzaa+ ikafunuliwa,Kwa kemeo la Yehova, kwa mlipuko wa pumzi ya pua yake.+
17 Alikuwa akituma mkono kutoka juu, alikuwa akinichukua,+Alikuwa akinitoa ndani ya maji makuu.+
18 Alikuwa akinikomboa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+Kutoka kwa wale wanaonichukia; kwa sababu walikuwa na nguvu kuliko mimi.+
19 Waliendelea kunikabili katika siku ya msiba wangu,+Lakini Yehova akawa tegemeo langu.+
20 Naye akanitoa nje mpaka mahali penye nafasi tele;+Alikuwa akiniokoa, kwa sababu alikuwa amependezwa nami.+
21 Yehova hunipa thawabu kulingana na uadilifu wangu;+Hunilipa kulingana na usafi wa mikono yangu.+
22 Kwa maana nimezishika njia za Yehova,+Wala kwa uovu sikuondoka kwa Mungu wangu.+
23 Kwa maana maamuzi yake yote ya hukumu+ yako mbele yangu;Na kwa habari ya sheria zake, sitageuka kando kuziacha.+
24 Nami nitajiendesha bila kosa+ mbele zake,Nami nitajiepusha na kosa.+
25 Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+Kulingana na usafi wangu mbele za macho yake.+
26 Kwa mtu mshikamanifu utatenda kwa ushikamanifu;+Kwa mtu asiye na kosa, mwenye nguvu, utatenda kwa njia isiyo na kosa;+
27 Kwa mtu anayebaki safi utakuwa safi,+Na kwa mpotovu utatenda kama mpumbavu.+
28 Nawe utawaokoa watu wanyenyekevu;+Bali macho yako, yako dhidi ya wenye majivuno, ili uwashushe.+
29 Kwa maana wewe ni taa yangu, Ee Yehova,+Na Yehova ndiye anayefanya giza langu liangaze.+
30 Kwa maana kwa msaada wako ninaweza kukimbiza kikundi cha waporaji;+Kwa msaada wa Mungu wangu ninaweza kuupanda ukuta.+
31 Mungu wa kweli, njia yake ni kamilifu;+Neno la Yehova limetakaswa.+Yeye ni ngao kwa wale wote wanaomkimbilia.+
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu ila Yehova,+Na ni nani aliye mwamba ila Mungu wetu?+
33 Mungu wa kweli ni ngome yangu yenye nguvu,+Naye ataifanya njia yangu iwe kamilifu,+
34 Anaifanya miguu yangu iwe kama ile ya paa;+Na kwenye mahali palipo juu kwa ajili yangu yeye huendelea kunisimamisha.+
35 Anaifundisha mikono yangu kupigana vita;+Nayo mikono yangu imepinda upinde wa shaba.+
36 Nawe utanipa ngao yako ya wokovu,+Na unyenyekevu wako ndio hunifanya niwe mkuu.+
37 Utafanyiza nafasi kubwa ya kutosha kwa ajili ya hatua zangu zilizo chini yangu;+Navyo vifundo vya miguu yangu hakika havitatetemeka.+
38 Nitawafuatilia adui zangu, ili niwamalize,Nami sitarudi mpaka waangamizwe.+
39 Nami nitawaangamiza na kuwavunja vipande-vipande,+ ili wasisimame;+Nao wataanguka chini ya miguu yangu.+
40 Nawe utanifunga mshipi wa nguvu kwa ajili ya vita;+Utawaangusha chini yangu wale wanaoniinukia.+
41 Nao adui zangu, utanipa upande wa nyuma wa shingo yao;+Wale wanaonichukia vikali—nitawanyamazisha pia.+
42 Wanalia wapate msaada, lakini hakuna mwokozi;+Kwa Yehova, lakini yeye hawajibu.+
43 Nami nitawatwanga wawe laini kama mavumbi ya udongo;Nitawaponda kama matope ya barabarani;+Nitawapiga niwalaze.
44 Nawe utanifanya niponyoke lawama ya watu wangu.+Utanilinda niwe kiongozi wa mataifa;+Watu ambao sikujua—watanitumikia.+
45 Wageni watanijia wakitetemeka;+Masikio yatatii ili kunisikia.+
46 Wageni watakuwa dhaifu,Nao watakuja wakitetemeka kutoka katika maboma yao.+
47 Yehova anaishi;+ na abarikiwe Mwamba wangu;+Na Mungu wa mwamba wa wokovu wangu atukuzwe.+
48 Mungu wa kweli ndiye Mpaji wa matendo ya kisasi kwangu+Na ndiye anayeshusha vikundi vya watu chini yangu,+
49 Na ndiye anayeniondoa kwa adui zangu.+Nawe utaniinua juu ya wale wanaosimama dhidi yangu;+Utanikomboa kutoka kwa mtu mwenye vitendo vya jeuri.+
50 Ndiyo sababu nitakushukuru wewe, Ee Yehova, kati ya mataifa;+Nami nitalipigia jina lako muziki:+
51 Yule anayefanya matendo makuu ya wokovu kwa ajili ya mfalme wake+Na kuonyesha fadhili zenye upendo kwa mtiwa-mafuta wake,+Kwa Daudi na kwa uzao wake mpaka wakati usio na kipimo.”+
Maelezo ya Chini
^ Sheoli. Tazama Nyongeza 4.