2 Samweli 14:1-33

14  Basi Yoabu+ mwana wa Seruya+ akapata kujua kwamba moyo wa mfalme ulimwelekea Absalomu.+  Kwa hiyo Yoabu akatuma ujumbe huko Tekoa,+ na kutoka huko akamchukua mwanamke mwenye hekima+ na kumwambia: “Tafadhali, omboleza, nawe tafadhali uvae mavazi ya maombolezo, na usijipake mafuta;+ nawe uwe kama mwanamke ambaye amekuwa akiomboleza siku nyingi kwa ajili ya mtu aliyekufa.+  Nawe uingie kwa mfalme, useme naye neno hili.” Basi Yoabu akatia maneno hayo kinywani mwake.+  Na yule mwanamke Mtekoa akaingia kwa mfalme, akaanguka kifudifudi,+ akasujudu na kusema: “Okoa,+ Ee mfalme!”  Kwa hiyo mfalme akamwambia: “Una jambo gani?” Naye akasema: “Mimi ni mwanamke mjane,+ kwa kuwa mume wangu amekufa.  Na mjakazi wako alikuwa na wana wawili, na hao wawili wakaanza kupambana shambani,+ na hapakuwa na mkombozi+ wa kuwatenganisha. Mwishowe mmoja akampiga mwenzake, akamuua.  Na tazama, familia yote wamesimama juu ya mjakazi wako, nao wanaendelea kusema, ‘Mtoe yule aliyempiga ndugu yake, ili tumuue kwa sababu ya nafsi ya ndugu+ yake aliyemuua,+ nasi tumwangamize hata mrithi!’ Nao hakika watazima mng’ao wa makaa yangu ambao umebaki, naye mume wangu hatakuwa na jina wala baki juu ya uso wa nchi.”+  Ndipo mfalme akamwambia yule mwanamke: “Nenda nyumbani kwako, nami nitatoa amri kukuhusu.”+  Basi yule mwanamke Mtekoa akamwambia mfalme: “Kosa liwe juu yangu, na pia juu ya nyumba ya baba yangu,+ Ee mfalme, lakini mfalme na kiti chake cha ufalme hawana hatia.” 10  Naye mfalme akaendelea kusema: “Yeyote akisema nawe, umlete kwangu, naye hatakudhuru tena kamwe.” 11  Lakini akasema: “Tafadhali, mfalme na amkumbuke Yehova Mungu wako,+ ili mlipiza-kisasi wa damu+ asilete uharibifu sikuzote, na kwamba wasimwangamize mwanangu.” Naye mfalme akasema: “Kama Yehova anavyoishi,+ hata unywele mmoja+ wa mwana wako hautaanguka chini.” 12  Basi yule mwanamke akasema: “Tafadhali, acha mjakazi+ wako aseme neno+ na bwana wangu mfalme.” Kwa hiyo mfalme akasema: “Sema!”+ 13  Na yule mwanamke akaendelea kusema: “Kwa nini basi, umewaza jinsi hii+ dhidi ya watu wa Mungu?+ Mfalme anaposema neno hili, yeye ni kama mtu aliye na hatia,+ kwa kuwa mfalme hamrudishi mtu wake aliyefukuzwa.+ 14  Kwa maana sisi tutakufa hakika,+ tutakuwa kama maji yanayomwagwa chini kwenye udongo, ambayo hayawezi kukusanywa. Lakini Mungu hataondolea mbali nafsi hata moja,+ naye amefikiria sababu zinazofanya yule aliyefukuzwa asifukuzwe kwake. 15  Na kwa vile sasa nimeingia ili kusema neno hili na mfalme bwana wangu, ni kwa sababu watu walinitia woga. Basi mjakazi wako akasema, ‘Tafadhali, acha niseme na mfalme. Labda mfalme atatenda kulingana na neno la kijakazi wake. 16  Kwa sababu mfalme alisikiliza ili kumkomboa kijakazi wake kutoka mkononi mwa mtu anayetafuta kuniangamiza mimi na mwanangu wa pekee kutoka katika urithi aliotoa Mungu,’+ 17  ndipo mjakazi wako akasema, ‘Tafadhali, acha neno la bwana wangu mfalme liwe la kutuliza.’ Kwa maana bwana wangu mfalme ni kama malaika+ wa Mungu wa kweli, ili kutofautisha mema na mabaya,+ na Yehova Mungu wako awe pamoja nawe.” 18  Mfalme akajibu na kumwambia yule mwanamke: “Tafadhali, usinifiche jambo ambalo ninakuuliza.”+ Na yule mwanamke akasema: “Tafadhali, bwana wangu mfalme na aseme.” 19  Na mfalme akaendelea kusema: “Je, mkono wa Yoabu+ upo pamoja nawe katika mambo haya yote?”+ Ndipo yule mwanamke akajibu na kusema: “Kama inavyoishi nafsi yako,+ Ee bwana wangu mfalme, hakuna mtu anayeweza kwenda upande wa kuume wala wa kushoto kutoka kwa yote ambayo bwana wangu mfalme amesema; kwa maana mtumishi wako Yoabu ndiye aliyeniamuru, naye ndiye aliyetia maneno haya yote katika kinywa cha mjakazi wako.+ 20  Mtumishi wako Yoabu amefanya jambo hili ili abadili sura ya jambo lile, lakini bwana wangu ana hekima kama hekima ya malaika+ wa Mungu wa kweli, hivi kwamba ajue yote yaliyo duniani.” 21  Basi mfalme akamwambia Yoabu: “Tazama, sasa, hakika nitafanya jambo hili.+ Basi nenda, mrudishe yule kijana Absalomu.”+ 22  Ndipo Yoabu akaanguka kifudifudi, akasujudu na kumbariki mfalme;+ kisha Yoabu akasema: “Leo mtumishi wako amejua kwamba nimepata kibali machoni pako,+ Ee bwana wangu mfalme, kwa maana mfalme ametenda kulingana na neno la mtumishi wake.” 23  Kisha Yoabu akaondoka, akaenda Geshuri,+ akamleta Absalomu Yerusalemu.+ 24  Hata hivyo, mfalme akasema: “Acha ageuke, aende katika nyumba yake, lakini hatauona uso wangu.”+ Basi Absalomu akageuka, akaenda nyumbani kwake, wala hakuuona uso wa mfalme. 25  Basi, kwa kulinganisha na Absalomu, hakuna mwanamume aliyekuwa na sura nzuri+ sana katika Israeli yote kuweza kusifiwa sana hivyo. Hakuwa na kasoro yoyote, kuanzia wayo wa mguu wake mpaka kipaji cha kichwa chake. 26  Na aliponyoa kichwa chake—naye alikuwa akikinyoa mwishoni mwa kila mwaka; kwa kuwa nywele zilikuwa nzito+ sana juu yake, alizinyoa—alipima uzito wa nywele za kichwa chake, shekeli mia mbili kulingana na jiwe la mizani la kifalme. 27  Na Absalomu akazaa wana watatu+ na binti mmoja ambaye jina lake lilikuwa Tamari. Alikuwa mwanamke mrembo zaidi.+ 28  Na Absalomu akaendelea kukaa Yerusalemu miaka miwili kamili, naye hakuuona uso wa mfalme.+ 29  Basi Absalomu akatuma ujumbe kumwita Yoabu ili amtume kwa mfalme, naye hakukubali kuja kwake. Ndipo akatuma ujumbe tena, mara ya pili, naye hakukubali kuja. 30  Mwishowe akawaambia watumishi wake: “Tazameni, sehemu ya shamba la Yoabu iliyo kando ya shamba langu, na hapo ana shayiri. Nendeni, mwiteketeze kwa moto.”+ Basi watumishi wa Absalomu wakaiteketeza kwa moto ile sehemu ya shamba.+ 31  Ndipo Yoabu akaondoka, akaja kwa Absalomu nyumbani na kumwambia: “Kwa nini watumishi wako waliiteketeza sehemu ya shamba langu?” 32  Kwa hiyo Absalomu akamwambia Yoabu: “Tazama! Nilituma ujumbe kwako, nikisema, ‘Njoo hapa nikutume kwa mfalme, kusema: “Kwa nini nimekuja kutoka Geshuri?+ Ingalikuwa afadhali kama bado ningalikuwa kule. Na sasa acha niuone uso wa mfalme, na ikiwa ndani yangu mna kosa lolote,+ basi na aniue.”’” 33  Kwa hiyo Yoabu akaingia kwa mfalme na kumwambia. Ndipo akamwita Absalomu, ambaye sasa aliingia kwa mfalme, akamsujudia, akaanguka kifudifudi mbele ya mfalme; kisha mfalme akambusu Absalomu.+

Maelezo ya Chini