2 Samweli 5:1-25
5 Baada ya muda makabila yote ya Israeli yakaja kwa Daudi+ katika Hebroni+ na kusema: “Tazama! Sisi ni mfupa wako na nyama yako.+
2 Jana na juzi vilevile,+ Sauli alipokuwa mfalme juu yetu, ni wewe uliyeongoza Israeli katika kuwatoa na kuwaingiza.+ Na Yehova alikuambia, ‘Wewe utawachunga+ watu wangu Israeli, nawe utakuwa kiongozi+ juu ya Israeli.’”
3 Basi wanaume wote wazee+ wa Israeli wakaja kwa mfalme katika Hebroni, na Mfalme Daudi akafanya agano+ nao katika Hebroni mbele za Yehova; kisha wakamtia mafuta+ Daudi awe mfalme juu ya Israeli.+
4 Daudi alikuwa na umri wa miaka 30 alipoanza kuwa mfalme. Akatawala kwa miaka 40+ akiwa mfalme.
5 Katika Hebroni alitawala akiwa mfalme juu ya Yuda kwa miaka 7 na miezi 6;+ na katika Yerusalemu+ akatawala akiwa mfalme kwa miaka 33 juu ya Israeli yote na Yuda.
6 Basi mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu kupigana na Wayebusi+ wanaokaa katika nchi, nao wakaanza kumwambia Daudi: “Wewe hutaingia humu, lakini bila shaka vipofu na vilema watakufukuza,”+ wao walikuwa wakifikiri: “Daudi hataingia humu.”
7 Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni,+ yaani, Jiji la Daudi.+
8 Hivyo Daudi akasema siku hiyo: “Yeyote atakayewapiga Wayebusi,+ basi, kwa kutumia mfereji wa chini kwa chini wa maji,+ na akutane na vilema pamoja na vipofu, wenye kuchukiza nafsi ya Daudi!” Ndiyo sababu wao husema: “Kipofu na kilema hawataingia katika nyumba.”
9 Na Daudi akaanza kukaa katika ngome hiyo, nayo ikaitwa Jiji la Daudi; na Daudi akaanza kujenga kuzunguka pande zote kuanzia Kilima+ na kuelekea ndani.
10 Kwa hiyo Daudi akaendelea kuwa mkuu zaidi na zaidi,+ na Yehova Mungu wa majeshi+ alikuwa pamoja naye.+
11 Na Hiramu+ mfalme wa Tiro akatuma wajumbe+ kwa Daudi, na pia mierezi+ na wafanyakazi wa miti na wafanyakazi wa mawe ya kuta, nao wakaanza kumjengea Daudi nyumba.+
12 Na Daudi akajua kwamba Yehova alikuwa amemfanya imara kuwa mfalme juu ya Israeli+ na kwamba alikuwa ameuinua+ ufalme wake kwa ajili ya watu wake Israeli.+
13 Wakati huo Daudi akaendelea kuchukua masuria+ na wake+ zaidi kutoka katika Yerusalemu baada ya kutoka Hebroni; naye Daudi akaendelea kuzaa wana na mabinti zaidi.
14 Na haya ndiyo majina ya wale ambao alizaa katika Yerusalemu: Shamua+ na Shobabu+ na Nathani+ na Sulemani,+
15 na Ibhari na Elishua+ na Nefegi+ na Yafia,+
16 na Elishama+ na Eliada na Elifeleti.+
17 Na Wafilisti wakasikia kwamba walikuwa wamemtia mafuta Daudi awe mfalme juu ya Israeli.+ Ndipo Wafilisti wote wakaja kumtafuta Daudi. Daudi aliposikia habari hizo, akashuka, akatoka na kwenda mahali palipo pagumu kufikiwa.+
18 Nao Wafilisti wakaingia na kuendelea kutembea huku na huku katika nchi tambarare ya chini ya Refaimu.+
19 Naye Daudi akaanza kumuuliza+ Yehova, akisema: “Je, nipande kwenda kupigana na Wafilisti? Je, utawatia mkononi mwangu?” Ndipo Yehova akamwambia Daudi: “Panda uende, kwa maana bila shaka nitawatia Wafilisti mikononi mwako.”+
20 Kwa hiyo Daudi akaja Baal-perasimu,+ na Daudi akawapiga na kuwaua huko. Ndipo akasema: “Yehova amepenya katikati ya adui+ zangu mbele yangu, kama pengo lililofanyizwa na maji.” Ndiyo sababu alipaita mahali hapo jina Baal-perasimu.+
21 Basi wakaziacha sanamu+ zao huko, kwa hiyo Daudi na watu wake wakazichukua.+
22 Baadaye Wafilisti wakaja tena+ na kutembea huku na huku katika nchi tambarare ya chini ya Refaimu.+
23 Ndipo Daudi akamuuliza+ Yehova, lakini yeye akasema: “Usipande kwenda. Zunguka uende nyuma yao, nawe uje juu yao mbele ya miti ya mibaka.+
24 Na iwe kwamba, utakaposikia sauti ya mwendo juu ya miti ya mibaka, ndipo utende bila kusita,+ kwa sababu wakati huo Yehova atakuwa ametoka kwenda mbele yako kuipiga kambi ya Wafilisti.”+
25 Basi Daudi akafanya hivyo, kama Yehova alivyokuwa amemwamuru,+ naye akawapiga+ Wafilisti kutoka Geba+ mpaka Gezeri.+