Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 11

Juu ya Nini Kuko Mateso Mingi Sana?

Juu ya Nini Kuko Mateso Mingi Sana?

1, 2. Watu wengi wanajiulizaka ulizo gani?

MAJI mingi yanaharibu kijiji fulani. Mwanaume fulani mwenye kuwa na bunduki anapiga masasi watu wenye kuwa mu kanisa, anaumiza na kuua watu wengi. Ugonjwa wa kansere unaua mama mumoja, na anaacha watoto tano.

2 Wakati misiba ao magumu kama hayo yanatokea, watu wengi wanajiulizaka hivi: “Juu ya nini?” Watu wengi wanajiulizaka juu ya nini dunia inajaa chuki na mateso. Na wewe umekwisha kujiuliza ulizo hilo?

3, 4. (a) Habakuki aliuliza maulizo gani? (b) Yehova alimujibu namna gani?

3 Biblia inaonyesha kama watu wenye walikuwa na imani yenye nguvu katika Mungu waliuliza pia maulizo kama hayo. Kwa mufano, nabii Habakuki alimuuliza Yehova hivi: “Sababu gani unanifanya nione matendo mabaya? Na sababu gani unaachilia ukandamizaji? Sababu gani uharibifu na jeuri viko mbele yangu? Na sababu gani ugomvi na vita vinaongezeka?”​—Habakuki 1:3.

4 Andiko la Habakuki 2:2, 3, linaonyesha namna Mungu alijibu maulizo ya Habakuki, na alimupatia ahadi (malako) kama atamaliza hali hiyo. Yehova anapenda sana watu. Biblia inasema hivi: “Anawahangaikia ninyi.” (1 Petro 5:7) Mungu anachukia sana mateso kupita vile tunayachukia. (Isaya 55:8, 9) Kwa hiyo, tuzungumuzie ulizo hili: Juu ya nini kuko mateso mingi sana mu dunia?

JUU YA NINI KUKO MATESO MINGI SANA?

5. Walimu wengi wa dini wanafundisha nini juu ya mateso? (b) Biblia inafundisha nini juu ya jambo hilo?

5 Wakati mutu anateseka, mara nyingi wakubwa na walimu wa dini (religion) wanasema kama ni mapenzi ya Mungu. Wamoja wanaweza kusema kama Mungu amepanga mbele ya wakati mambo yote yenye kutokea mu maisha ya mutu, na hata magumu yenye kumupata. Tena, wanasema kama hatuwezi hata kidogo kuelewa ni juu ya nini. Wengine wanasema kama watu, hata watoto wadogo, wanakufa ili kuenda kuishi mbinguni pamoja na Mungu. Lakini hiyo haiko kweli. Yehova halete mambo ya mubaya hata kidogo. Biblia inasema hivi: “Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwamba Mungu wa kweli atende uovu, na Mweza-Yote afanye makosa!”​—Yobu 34:10.

6. Juu ya nini watu wengi wanasema kama Mungu njo analeta mateso yote yenye tunaona?

6 Watu wengi wanasema kama Mungu njo analeta mateso yote. Juu ya nini? Wanawaza kama yeye njo anatawala ulimwengu ao dunia. Lakini kama vile tulijifunza mu Sura ya 3, mwenye kutawala ulimwengu kabisa ni Shetani Ibilisi.

7, 8. Juu ya nini kuko mateso mingi sana mu dunia?

7 Biblia inasema kama “ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.” (1 Yohana 5:19) Shetani, mutawala wa ulimwengu huu ni muovu na hana huruma. “Anapotosha [ao, kudanganya] dunia yote yenye kuikaliwa na watu.” (Ufunuo 12:9) Watu wengi wanamuiga. Na hiyo ni sababu moja yenye kufanya dunia ijae uongo, chuki, na mambo ya kuumizana na kuuana.

8 Kuko sababu zingine zenye zinafanya kukuwe mateso mingi sana mu dunia. Kisha Adamu na Eva kumupinga Mungu, watoto wao waliriti zambi yao. Na juu ya zambi, watu wanaletea wengine mateso. Mara nyingi wanapenda kuwa wa maana zaidi kupita wengine. Wanakuwa na ugomvi kati yao, wanapigana vita, na wanaonea wengine. (Muhubiri 4:1; 8:9) Wakati fulani watu wanateseka juu ya “wakati na matukio yenye hayatazamiwe.” (Muhubiri 9:11) Wakati wako nafasi ya mubaya kwa wakati mubaya, wanaweza kupatwa na aksidenti na mambo ingine ya mubaya yanaweza kuwapata.

9. Juu ya nini tunaweza kuamini kabisa kama Yehova iko na sababu ya muzuri yenye inafanya aache mateso yaendelee?

9 Yehova haletee watu mateso hata kidogo. Hatuwezi kusema kama yeye njo analeta vita, jeuri na matendo ya kuonea wengine. Mungu halete misiba, kama vile matetemeko ya inchi, upepo mukali, na mafuriko (maji mingi yenye kuleta uharibifu). Lakini unaweza kujiuliza hivi: ‘Kama Yehova njo mwenye nguvu zaidi mu ulimwengu wote, juu ya nini hafanye mambo hayo yasitokee?’ Tunajua kama Mungu anatuhangaikia sana. Kwa hiyo, anapaswa kuwa na sababu ya muzuri yenye inamuchochea aache mateso yaendelee.​—1 Yohana 4:8.

JUU YA NINI MUNGU ANAACHA MATESO?

10. Namna gani Shetani alimupinga Yehova?

10 Mu bustani ao shamba la Edeni, Ibilisi alidanganya Adamu na Eva. Shetani alimushitaki Mungu kama iko Mutawala mubaya. Alisema kama Mungu aliwaima Adamu na Eva jambo fulani la muzuri. Shetani alipenda waamini kama yeye angekuwa mutawala muzuri sana kupita Yehova, na kama hawakukuwa na lazima ya kuongozwa na Mungu.​—Mwanzo 3:2-5; ona Mafasirio Ingine ya 27.

11. Tutajibu ulizo gani?

11 Adamu na Eva walikosa kumutii ao kumusikia Yehova na wakamupinga. Waliwaza kama walikuwa na haki ya kujiamulia mambo ya muzuri na mambo ya mubaya. Namna gani Yehova angeonyesha kama wapinzani hao walikosea na kama yeye njo anajua mambo yenye kuwa ya muzuri kwetu?

12, 13. (a) Juu ya nini Yehova hakuua Adamu na Eva palepale? (b) Juu ya nini Yehova ameacha Shetani akuwe mutawala wa ulimwengu huu? Na juu ya nini Yehova ameacha watu wajiongoze wao wenyewe?

12 Yehova hakuua Adamu na Eva palepale. Lakini, aliwaacha wakuwe na watoto. Kisha Yehova alipatia watoto wa Adamu na Eva nafasi ya kuchagua ni nani wanapenda akuwe mutawala wao. Yehova alikuwa na kusudi la kufanya dunia ijae watu wakamilifu, na jambo hilo lingetimia hata kama Shetani alimupinga.​—Mwanzo 1:28; Isaya 55:10, 11.

13 Shetani alimupinga Yehova mbele ya mamilioni ya malaika. (Yobu 38:7; Danieli 7:10) Kwa hiyo, Yehova alimupatia Shetani wakati wa kuonyesha ikiwa mambo yenye alimushitaki yalikuwa ya kweli. Na alipatia wanadamu wakati wa kuonyesha ikiwa wangeweza kujiongoza wao wenyewe bila musaada wake. Kwa hiyo, aliwaacha wafanye serikali ao guvernema zao wenyewe chini ya uongozi wa Shetani.

14. Mungu aliacha wakati upite, hilo limeonyesha nini?

14 Kwa maelfu ya miaka, wanadamu wamejaribu kujitawala wenyewe, lakini wameshindwa. Hilo limeonyesha kama Shetani ni musema-uongo. Wanadamu wako na lazima ya musaada wa Mungu. Nabii Yeremia alisema kweli wakati aliandika hivi: “Ninajua muzuri, Ee Yehova, kwamba njia ya mwanadamu haiko katika uwezo wake. Mwanadamu mwenye kutembea hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.”​—Yeremia 10:23.

JUU YA NINI YEHOVA AMEACHA MATESO YAENDELEE WAKATI MUREFU?

15, 16. (a) Juu ya nini Yehova ameacha mateso yaendelee wakati murefu? (b) Juu ya nini Yehova hajamaliza magumu yenye Shetani ameleta?

15 Juu ya nini Yehova ameacha mateso yaendelee wakati murefu? Juu ya nini hafanye mambo ya mubaya yasitokee? Imeomba wakati murefu juu ya kuonyesha kama utawala wa Shetani umeshindwa. Watu wamejaribu kila aina ya serikali, lakini zote zimeshindwa. Hata kama wamefanya maendeleo mu mambo ya sayansi na teknolojia, kuko ukosefu mingi wa haki, umaskini, jeuri, na vita kuliko zamani. Hatuwezi kujitawala muzuri sisi wenyewe bila musaada wa Mungu.

16 Lakini Yehova hajamaliza magumu yenye Shetani ameleta. Mungu angefanya vile, hilo lingeonyesha kama anaunga mukono utawala wa Shetani, na hawezi kufanya vile hata kidogo. Tena, watu wangewaza kama wanaweza kujitawala muzuri wao wenyewe. Lakini huo ni uongo, na Yehova hawezi kuunga mukono uongo huo. Hawezi kusema uongo.​—Waebrania 6:18.

17, 18. Yehova atafanya nini juu ya mambo yote ya mubaya yenye Shetani ameleta?

17 Je, Yehova iko na uwezo wa kumaliza mambo yote ya mubaya yenye yametokea juu ya upinzani wa Shetani na wanadamu? Ndiyo. Mungu anaweza mambo yote. Yehova anajua ni wakati gani mambo yote yenye Shetani alimushitaki yatakuwa yamejibiwa kabisa-kabisa. Kisha atafanya dunia kuwa paradiso, kama vile alikusudia. Wale wote wenye kuwa mu “makaburi ya ukumbusho” watafufuliwa. (Yohana 5:28, 29) Watu hawatagonjwa tena na hawatakufa tena. Yesu atatosha mambo yote ya mubaya yenye Shetani ameleta. Yehova atamutumia Yesu “ili avunje kazi za Ibilisi.” (1 Yohana 3:8) Tunafurahi sana kuona kama, mbele wakati huo ufike, Yehova ametuvumilia sana ili tufikie kumujua na kuamua ikiwa tunapenda yeye akuwe Mutawala wetu. (Soma 2 Petro 3:9, 10.) Hata wakati tunateseka, anatusaidia kuvumilia.​—Yohana 4:23; soma 1 Wakorinto 10:13.

18 Yehova hatukaze tumuchague yeye kuwa Mutawala wetu. Alipatia watu zawadi ya muzuri sana, ni kusema, uhuru wa kuchagua. Tuzungumuzie basi namna tunaweza kutumia zawadi hiyo ya maana sana.

NAMNA GANI UTATUMIA UHURU WAKO WA KUCHAGUA?

19. Yehova ametupatia zawadi gani ya muzuri sana? Juu ya nini tunapaswa kupendezwa na zawadi hiyo?

19 Zawadi ya muzuri sana ya uhuru wa kuchagua yenye Mungu ametupatia inatufanya tusikuwe sawa na wanyama. Mambo yenye wanafanya yanaongozwa na silika (uwezo fulani wenye unawafanya watende kwa njia fulani), lakini sisi tunaweza kuchagua namna tunapenda kuishi na kuamua ikiwa tunapenda kumupendeza Yehova. (Mezali 30:24) Tena, hatuko kama mashine zenye kufanya tu mambo yenye zimepangiwa kufanya. Tuko na uhuru wa kuchagua ikiwa tunapenda kuwa watu wa namna gani, watu wenye tunapenda wakuwe marafiki wetu, na mambo yenye tunapenda kufanya mu maisha yetu. Yehova anapenda tufurahie maisha.

20, 21. Ni uamuzi gani wa muzuri zaidi wenye unaweza kukamata leo?

20 Yehova anataka tumupende. (Matayo 22:37, 38) Ni kama baba mwenye anafurahia kusikia mutoto wake anamuambia kwa moyo wake “Ninakupenda” na haiko juu wanamukaza kusema vile. Yehova alitupatia uhuru wa kuchagua kama tutamutumikia ao hapana. Shetani, Adamu, na Eva walichagua kukataa kutumikia Yehova. Namna gani utatumia uhuru wako wa kuchagua?

21 Tumia uhuru wako wa kuchagua juu ya kumutumikia Yehova. Kuko mamilioni ya watu wengine wenye wameamua kumupendeza Mungu na kumupinga Shetani. (Mezali 27:11) Unaweza kufanya nini leo ili ukuwe mu dunia mupya ya Mungu wakati atatosha mateso yote? Habari yenye kufuata itazungumuzia ulizo hilo.