Muhubiri 8:1-17

  • Wakati mwanadamu mwenye hakamilike anatawala (1-17)

    • Tii maagizo ya mufalme (2-4)

    • Utawala wa mwanadamu ni wenye kuumiza (9)

    • Wakati azabu haitolewe haraka (11)

    • Kula, kunywa, na ufurahi (15)

8  Ni nani mwenye kuwa kama mutu mwenye hekima? Ni nani anajua kutatua tatizo?* Hekima ya mutu inafanya uso wake ungae na inatuliza uso wake wenye ukali. 2  Ninasema: “Tii maagizo ya mufalme+ kwa sababu ya kiapo kwa Mungu.+ 3  Usiondoke haraka mbele yake.+ Usiunge mukono jambo lolote la mubaya;+ kwa maana anaweza kufanya kile anapenda, 4  kwa sababu neno la mufalme liko na nguvu;+ ni nani anaweza kumuambia: ‘Unafanya nini?’” 5  Mwenye anashika amri hataumia,+ na moyo wenye hekima utajua wakati na utaratibu wenye kufaa.*+ 6  Kwa maana kila jambo liko na wakati na utaratibu wake,*+ kwa sababu matatizo ya wanadamu ni mengi sana. 7  Kwa kuwa hakuna mwenye anajua mambo yenye yatatokea, ni nani anaweza kumuambia namna yatatokea? 8  Kama vile hakuna mutu mwenye kuwa na uwezo juu ya roho* ao mwenye anaweza kuzuia roho, vilevile hakuna mwenye kuwa na uwezo juu ya siku ya kifo.+ Kama vile hakuna mwenye anaruhusiwa kuondoka wakati wa vita, vilevile uovu hautaruhusu wale wenye wanazoea kuutenda waponyoke.* 9  Nimeona mambo haya yote, na nilichunguza katika moyo wangu kila kazi yenye imefanywa chini ya jua, wakati mwanadamu ametawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.*+ 10  Na niliona waovu wakizikwa, watu wenye walizoea kuingia na kutoka mahali patakatifu, lakini walisahauliwa haraka katika muji kwenye walitenda vile.+ Jambo hili pia ni bure.* 11  Kwa sababu azabu haikutolewa haraka juu ya tendo la mubaya,+ moyo wa wanadamu hauogope kutenda mabaya.+ 12  Hata kama muovu anaweza kutenda mabaya mara mia moja (100) na kuendelea kuishi wakati murefu, lakini ninajua kwamba mambo yatawaendea muzuri wale wenye kumuogopa Mungu wa kweli, kwa sababu wanamuogopa.+ 13  Lakini mambo hayatamuendea muzuri muovu,+ wala hatarefusha siku zake zenye ziko kama kivuli,+ kwa sababu hamuogope Mungu. 14  Kuko jambo la bure* lenye linatendeka katika dunia: Kuko wenye haki wenye wanatendewa kama vile wamefanya mambo maovu,+ na kuko watu waovu wenye wanatendewa kama vile wametenda kwa haki.+ Ninasema kwamba jambo hili pia ni bure.* 15  Basi nikashauri watu wafurahi,+ kwa sababu chini ya jua hakuna jambo la muzuri zaidi kwa mwanadamu kuliko kula, kunywa, na kufurahi; anapaswa kufanya vile wakati anatumika sana sikuzote za maisha yake,+ zenye Mungu wa kweli amemupatia chini ya jua. 16  Nilijikaza sana katika moyo wangu ili kupata hekima na kuona kazi* yote yenye kufanywa katika dunia,+ hata nilikosa usingizi muchana na usiku.* 17  Basi nikafikiria kazi yote ya Mungu wa kweli, na nikavumbua kwamba wanadamu hawawezi kuelewa mambo yenye kufanyika chini ya jua.+ Hata kama watu wanajaribu kwa bidii namna gani, hawawezi kuyaelewa. Hata wakisema kwamba wako na hekima ya kutosha kuweza kujua, hawawezi kuyaelewa kabisa.+

Maelezo ya Chini

Ao “kufasiria maana ya jambo.”
Ao “wakati na hukumu yenye kufaa.”
Ao “hukumu yake.”
Ao “pumuzi, upepo.”
Ao pengine, “uovu wao hauwezi kuokoa waovu.”
Ao “kumutendea mubaya; kumutesa.”
Ao “ubatili.”
Ao “lenye kuvunja moyo.”
Ao “ubatili.”
Ao “shuguli.”
Ao pengine, “kwamba watu hawapate usingizi ikuwe muchana ao usiku.”