Muhubiri 9:1-18

  • Wote wanapatwa na jambo lilelile (1-3)

  • Furahia maisha hata kama utakufa (4-12)

    • Wafu hawajue kitu chochote (5)

    • Hakuna kazi yoyote katika Kaburi (10)

    • Wakati na mambo yenye hayatazamiwe (11)

  • Hekima haifurahiwe kila mara (13-18)

9  Kwa hiyo nilitia mambo yote haya katika moyo wangu na kuona kwamba wenye haki na wenye hekima, na pia kazi zao, wako katika mikono ya Mungu wa kweli.+ Watu hawajue upendo ao chuki yenye ilifanywa mbele wakuwe.  Wote wanapatwa na jambo lilelile,*+ wenye haki na pia waovu,+ watu wazuri na safi na wale wenye hawako safi, wale wenye kutoa zabihu na wale wenye hawatoe zabihu. Mutu muzuri ni sawa na mutenda-zambi; mutu mwenye anaapa kiapo ni sawa na ule mwenye kuwa muangalifu kuhusu kuapa kiapo.  Hili ni jambo lenye kuhuzunisha lenye linatendeka chini ya jua: Kwa sababu wote wanapatwa na jambo lilelile,*+ moyo wa wanadamu umejaa ubaya; na kuko wazimu katika moyo wao wakati wa maisha yao, na kisha wanakufa!*  Kuko tumaini kwa mutu yeyote mwenye kuwa kati ya wazima, kwa sababu imbwa mwenye kuwa muzima anashindia simba mwenye amekufa.+  Kwa maana wazima wanajua* kwamba watakufa,+ lakini wafu hawajue kitu chochote,+ wala hawana zawabu* tena, kwa sababu mambo yote yenye yanaweza kukumbukwa juu yao yamesahauliwa.+  Tena, upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari vimepotea, na hawawezi tena kushiriki katika mambo yenye kufanywa chini ya jua.+  Uende, ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo muchangamufu,+ kwa sababu tayari Mungu wa kweli amefurahia kazi zako.+  Nguo zako zikuwe nyeupe,* na usikose kutia mafuta kwenye kichwa chako.+  Furahia maisha pamoja na bibi yako mupendwa+ siku zote za maisha yako ya bure, zenye Yeye amekupatia chini ya jua, siku zako zote za maisha yako yenye kuwa bure,* kwa maana hilo ndilo fungu lako* katika maisha na katika kazi yako ya nguvu yenye unafanya kwa jasho chini ya jua.+ 10  Kila jambo lenye mukono wako unapata kufanya, ulifanye kwa nguvu zako zote, kwa sababu hakuna kazi wala mipango wala ujuzi wala hekima katika Kaburi,*+ mahali unaenda. 11  Nimeona jambo lingine chini ya jua, kwamba haiko wenye mbio ndio wanashinda kila mara katika mbio, wala haiko wenye nguvu ndio wanashinda katika vita,+ wala haiko wenye hekima ndio wanapata kila mara chakula, wala haiko wenye akili ndio wanakuwa kila mara na utajiri,+ wala haiko wenye ujuzi ndio wanafanikiwa kila mara,+ kwa sababu wakati na matukio yenye hayatazamiwe* yanafikia wote. 12  Kwa maana mwanadamu hajue wakati wake.+ Kama vile samaki wanakamatwa katika wavu* hatari na kama vile ndege wanakamatwa katika mutego, ni vile pia wana wa binadamu wananaswa wakati wa taabu,* wakati inawafikia bila kutazamia. 13  Niliona pia jambo hili kuhusu hekima chini ya jua—​na lilinivutia: 14  Kulikuwa muji mudogo wenye watu kidogo; na mufalme mwenye nguvu alikuja kupigana nao na aliuzunguka na kutengeneza vitu vikubwa vya kutumia ili kuuzunguka kwa ajili ya vita. 15  Katika muji huo kulikuwa mutu fulani maskini lakini mwenye hekima, naye akaokoa muji huo kupitia hekima yake. Lakini hakuna mwenye alimukumbuka mutu huyo maskini.+ 16  Na nikasema katika moyo wangu: ‘Hekima inashindia nguvu;+ lakini hekima ya maskini inazarauliwa, na maneno yake hayasikilizwe.’+ 17  Ni muzuri zaidi kusikiliza maneno ya utulivu ya mwenye hekima kuliko makelele ya mutu mwenye kutawala kati ya wapumbavu. 18  Hekima inashindia silaha za vita, lakini mutenda-zambi mumoja tu anaweza kuharibu mambo mengi ya muzuri.+

Maelezo ya Chini

Ao “mwisho uleule.”
Ao “mwisho uleule.”
Tnn., “na kisha hilo—wanaenda kwa wafu!”
Ao “wanatambua.”
Ao “mushahara.”
Ni kusema, nguo zenye kungaa ambazo zinaonyesha hali ya furaha, hapana nguo za maombolezo.
Ao “siku zako za ubatili.”
Ao “sehemu yako.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “matukio yenye hayakuwaziwa.”
Ao “makila.”
Ao “musiba.”