Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Na Atimize Mipango Yako Yote

Na Atimize Mipango Yako Yote

“Upate furaha tele katika Yehova,naye atakupa maombi ya moyo wako.”​—ZAB. 37:4.

NYIMBO: 89, 140

1. Kijana anapaswa kuamua nini juu ya wakati unaokuja, lakini sababu gani hapaswe kuhangaika sana? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

VIJANA, pengine mutakubali kuwa mbele ya kuanza safari, ni jambo la hekima mutu afanye mipango juu ya mahali kwenye ataenda. Maisha ni kama safari, na wakati ungali kijana ndio wakati wa kufanya mipango juu ya mahali kwenye unapenda kuenda. Kwa kweli, inaweza kuwa vigumu kufanya mipango. Kijana mumoja mwanamuke mwenye kuitwa Heather alisema hivi: “Ni jambo la kuogopesha. Unapaswa kuamua namna utatumia maisha yako yote.” Lakini usiogope. Yehova anaambia watu wake hivi: ‘Usitazame huku na huku [usihangaike], kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu. Nitakusaidia.’​—Isa. 41:10.

2. Namna gani unajua kuwa Yehova anapenda ufanye mipango yenye itakusaidia ukuwe na wakati unaokuja wenye furaha?

2 Yehova anakuomba upange kwa hekima wakati wako unaokuja. (Mhu. 12:1; Mt. 6:20) Anapenda ukuwe na furaha. Hilo linaonekana wazi wakati unaona, unasikia, na kuonja vitu mbalimbali vyenye aliumba. Fikiria pia namna anatuhangaikia na kutufundisha namna ya kuwa na maisha ya muzuri zaidi. Yehova anaambia hivi wale wenye kukataa mashauri yake: ‘Mulichagua jambo ambalo halikunipendeza. . . . Tazama! Watumishi wangu watashangilia, lakini ninyi mutaona aibu [haya]. Tazama! Watumishi wangu watapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya hali nzuri ya moyo.’ (Isa. 65:12-14) Yehova anatukuzwa wakati watumishi wake wanakamata maamuzi yenye hekima katika maisha yao.​—Met. 27:11.

MIPANGO YENYE ITAKULETEA FURAHA

3. Yehova anakuomba ufanye nini?

3 Yehova anakuomba ufanye mipango gani? Ili tukuwe na furaha tunapaswa kumujua na kumutumikia Mungu kwa uaminifu. Ni hivyo Mungu alituumba. (Zab. 128:1; Mt. 5:3) Hiyo ni tofauti kubwa na wanyama wenye aliumba, wenye wanatosheka tu na kula, kunywa, na kuzaa watoto. Mungu anapenda ukuwe na furaha kwa kufanya mipango juu ya mambo mengine zaidi ya yale yenye wanyama wanatosheka nayo. Muumbaji wako ni “Mungu wa upendo,” “Mungu mwenye furaha,” mwenye aliumba wanadamu ‘kwa mufano wake.’ (2 Kor. 13:11; 1 Tim. 1: 11; Mwa. 1:27) Utakuwa na furaha ikiwa unamuiga Mungu wetu mwenye upendo. Umekwisha kujionea ukweli wa andiko hili: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea”? (Mdo. 20:35) Hiyo ni kweli ya musingi katika maisha ya mwanadamu. Kwa hiyo, Yehova anapenda ufanye mipango yenye kuonyesha kuwa unamupenda yeye na kupenda wengine.​—Soma Mathayo 22:36-39.

4, 5. Ni nini ilimuletea Yesu furaha?

4 Yesu Kristo aliwaachia ninyi vijana mufano mukamilifu. Wakati alikuwa mutoto, yeye pia alikuwa anacheza na kujifurahisha. Neno la Mungu linasema kuwa kuko “wakati wa kucheka. . . na wakati wa kurukaruka [kucheza].” (Mhu. 3:4) Pia, Yesu alimukaribia Yehova kwa kujifunza Maandiko. Wakati alikuwa na miaka 12, walimu kwenye hekalu walishangazwa na “uelewaji wake na majibu yake” juu ya mambo ya kiroho.​—Lu. 2:42, 46, 47.

5 Yesu alikomaa na kuwa mutu muzima mwenye furaha. Ni nini ilimuletea furaha? Alijua kuwa, kati ya mambo mengine, Mungu alipenda ‘awatangazie masikini habari njema . . . na kupata kuona tena kwa vipofu.’ (Lu. 4:18) Yesu alipata furaha kwa sababu alifanya mambo yenye Mungu alimuomba afanye. Zaburi 40:8 inaonyesha namna alijisikia; inasema hivi: “Ee Mungu wangu, nimependezwa na kufanya mapenzi yako.” Yesu alifurahia kufundisha watu juu ya Baba yake wa mbinguni. (Soma Luka 10:21.) Kisha kufundisha mwanamuke mumoja juu ya ibada ya kweli, Yesu aliambia hivi wanafunzi wake: “Chakula changu ni mimi kufanya mapenzi yake aliyenituma na kuimaliza kazi yake.” (Yoh. 4:31-34) Kumupenda Mungu na wengine kulifanya Yesu akuwe na furaha. Kunaweza kukuletea furaha wewe pia.

6. Sababu gani ni muzuri uzungumuzie mipango yako ya wakati unaokuja pamoja na Wakristo wenye kuwa na uzoefu?

6 Wakristo wengi walipata furaha katika ujana wao kwa sababu walifanya kazi ya upainia. Unaweza kuzungumuzia mipango yako pamoja nao. ‘Mipango inavunjika mahali ambapo hapana mazungumuzo ya siri, lakini katika wingi wa washauri mambo yanatimizwa.’ (Met. 15:22) Watu hao wenye kukomaa kiroho wanaweza kukuambia kuwa utumishi wa wakati wote utakufundisha mambo yenye yatakusaidia katika maisha yako yote. Kisha kufundishwa na Baba yake huko mbinguni, Yesu aliendelea kujifunza mambo mengine wakati wa utumishi wake hapa duniani. Kwa mufano, alijionea furaha ya kugusa mioyo ya watu kwa kuwahubiria habari njema na pia furaha ya kubakia muaminifu wakati wa majaribu. (Soma Isaya 50:4; Ebr. 5:8; 12:2) Tuzungumuzie basi aina fulani za utumishi wa wakati wote zenye zinaweza kukuletea furaha sana.

SABABU GANI WALE WENYE KUFANYA WANAFUNZI WANAPATA MATOKEO YA MUZURI?

7. Sababu gani vijana wengi wanafurahia kazi ya kufanya wanafunzi?

7 Yesu alisema hivi: ‘Muende . . . mufanye wanafunzi kutoka kwa watu. . . na kuwafundisha.’ (Mt. 28:19, 20) Ikiwa unapanga kufanya kazi ya kufanya wanafunzi, utakuwa umechagua kazi ya maana zaidi, kazi yenye kumutukuza Mungu. Kama kazi zingine zote, inaomba wakati upite ili ukuwe na uzoefu. Hivi karibuni, ndugu mumoja mwenye kuitwa Timothy mwenye alianza kufanya kazi ya upainia wakati alikuwa angali kijana, alisema hivi: “Ninapenda kumutumikia Yehova kwa wakati wote kwa sababu hiyo ndiyo njia ya kuonyesha kuwa ninamupenda. Mwanzoni, sikuweza kuanzisha hata funzo moja la Biblia, lakini kisha kuhamia katika eneo lingine, nilianzisha mafunzo fulani ya Biblia katika mwezi mumoja. Mwanafunzi mumoja alianza kuja kwenye Jumba la Ufalme. Kisha kusoma kwa miezi mbili Masomo kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Bibi, * nilipewa mugawo mupya na huko nimeanzisha mafunzo ine. Ninapenda kufundisha watu kwa sababu ninaona namna roho takatifu inawasaidia kufanya mabadiliko.”​—1 Tes. 2:19.

8. Namna gani vijana fulani Wakristo wamefanya mengi zaidi katika kazi ya kufanya wanafunzi?

8 Vijana fulani wamejifunza luga ingine. Kwa mufano, Jacob, wa Amerika ya Kaskazini, anaandika hivi: “Wakati nilikuwa na miaka saba, wengi kati ya wanafunzi wenzangu walikuwa Wavietnamu. Nilipenda kuzungumuza nao juu ya Yehova, kwa hiyo, kisha muda fulani nilifanya mipango ili kujifunza luga yao. Nilijifunza mambo mengi kwa kulinganisha magazeti ya Munara wa Mulinzi ya luga ya Kiingereza na ya Kivietnamu. Pia nilitafuta marafiki katika kutaniko la luga ya Kivietnamu lenye lilikuwa karibu. Wakati nilikuwa na miaka 18, nilianza kufanya kazi ya upainia. Kisha, nilisoma Masomo kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Bibi. Kujifunza luga hiyo kulinisaidia katika mugawo wangu wa sasa wa kazi ya upainia, kwenye mimi peke yangu ndiye muzee katika kikundi cha luga ya Kivietnamu. Wavietnamu wengi wanashangaa kuona kuwa nimejifunza luga yao. Wananikaribisha katika nyumba zao, na mara nyingi ninajifunza Biblia pamoja nao. Wamoja kati yao wamefanya maendeleo mupaka kubatizwa.”​—Linganisha na Matendo 2:7, 8.

9. Namna gani kazi ya kufanya wanafunzi inatufundisha mambo ya muzuri?

9 Kazi ya kufanya wanafunzi inakufundisha namna ya kufanya kazi muzuri, ufundi wa kuzungumuza, namna ya kuwa na uhakika, na kutenda kwa hekima. (Met. 21:5; 2 Tim. 2:24) Lakini zaidi sana, kazi ya kufanya wanafunzi inaleta furaha kwa sababu inakusaidia kujua muzuri zaidi Maandiko yenye kuwa musingi wa imani yako. Pia, unajifunza namna ya kutumika pamoja na Yehova.​—1 Kor. 3:9.

10. Namna gani unaweza kupata furaha katika kazi ya kufanya wanafunzi hata katika eneo kwenye watu hawapendezwe na habari njema?

10 Unaweza kufurahia kazi ya kufanya wanafunzi hata kama katika eneo lenu ni hesabu kidogo ya watu ndio wanapendezwa na habari njema. Tunasaidiana katika kazi ya kufanya wanafunzi. Kutaniko lote linatafuta wale wenye kuwa na mioyo ya muzuri. Hata kama ni ndugu ao dada mumoja tu ndiye anaweza kupata mutu mwenye anaweza kufikia kuwa mwanafunzi, wote walisaidia kutafuta na wote wanaweza kuwa na furaha. Kwa mufano, Brandon alifanya kazi ya upainia kwa miaka kenda katika eneo moja kwenye watu hawapendezwe na kweli. Anasema hivi: “Ninapenda kuhubiri habari njema kwa sababu Yehova ndiye ametuomba tufanye kazi hiyo. Nilianza kufanya kazi ya upainia kisha tu kumaliza masomo. Ninafurahia kutia moyo ndugu vijana katika kutaniko letu na kuona namna wanafanya maendeleo ya kiroho. Kisha kusoma Masomo kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Bibi, nilipewa mugawo mupya kwenye nilifanya kazi ya upainia. Ni kweli kwamba sijapata katika eneo hata mutu mumoja mwenye amefanya maendeleo na kufikia kubatizwa, lakini wengine wamepata. Ninafurahi kwa sababu nilifanya mipango ya kutumika kwa wakati wote katika kazi ya kufanya wanafunzi.”​—Mhu. 11:6.

MIPANGO YAKO INAWEZA KUKUONGOZA WAPI?

11. Vijana wengi wamefurahia aina gani ya utumishi mutakatifu?

11 Kuko nafasi nyingi za kumutumikia Yehova. Kwa mufano, vijana wengi wanajitolea katika kazi ya ujenzi. Kuko lazima ya mamia ya Majumba ya Ufalme. Kazi ya kujenga majumba hayo ni utumishi mutakatifu wenye kumutukuza Mungu na inaweza kukuletea furaha. Kama katika aina zingine za utumishi mutakatifu, kutumika pamoja na wafanyakazi wenzako kunaleta furaha. Kazi ya ujenzi ya kiteokrasi inakufundisha kuhangaikia usalama, kuwa mufanyakazi mwenye bidii, na kutii wale wenye kuongoza.

Wale wenye kuanza utumishi wa wakati wote watapata baraka nyingi (Picha hii inapatana na fungu la 11-13)

12. Namna gani kazi ya upainia inaweza kukuongoza kwenye aina zingine za utumishi?

12 Ndugu mumoja mwenye kuitwa Kevin, anasema hivi: “Tangu wakati nilikuwa kijana mudogo, nilipenda kumutumikia Yehova kwa wakati wote siku fulani. Mwishowe, nilianza kufanya kazi ya upainia wakati nilikuwa na miaka 19. Nilijitegemeza mimi mwenyewe kwa kutumika wakati fulani pamoja na ndugu mumoja mwenye alikuwa anafanya kazi ya ujenzi. Nilijifunza kuweka paa (sehemu ya juu ya nyumba), madirisha, na milango. Kisha, nilipitisha miaka mbili pamoja na kikundi cha kutoa musaada kisha upepo mukali kutokea, nilikuwa ninasaidia kujenga Majumba ya Ufalme na nyumba za ndugu na dada. Wakati nilisikia kuwa katika Afrika ya Kusini kuko lazima ya musaada katika kazi ya ujenzi, nilijaza ombi na nikaalikwa kuenda huko. Hapa katika Afrika, kisha majuma fulani, ninaenda kujenga Majumba ya Ufalme mahali mbalimbali. Wajenzi wenzangu wako kama familia yangu. Tunaishi pamoja, tunajifunza Biblia pamoja, na kufanya kazi pamoja. Ninafurahia pia kuhubiri kila juma pamoja na ndugu na dada wa eneo. Mipango yenye nilifanya wakati nilikuwa kijana mudogo imeniletea furaha kuliko namna niliwazia.”

13. Namna gani kazi ya Beteli inaletea vijana furaha?

13 Ndugu na dada fulani wenye walitimiza mipango yao ya kumutumikia Yehova kwa wakati wote, sasa wako kwenye Beteli. Utumishi wa Beteli ni kazi yenye kuleta furaha kwa sababu kila jambo lenye unafanya huko ni kwa ajili ya Yehova. Familia ya Beteli inasaidia kutoa chakula cha kiroho. Mwanabeteli mumoja mwenye kuitwa Dustin anasema hivi: “Nilifanya utumishi wa wakati wote kuwa muradi wangu wakati nilikuwa na miaka kenda, na nilianza kufanya kazi ya upainia wakati nilimaliza masomo. Kisha mwaka moja na nusu, nilialikwa kwenye Beteli, huko nilijifunza namna ya kutumia mashini ya kuchapisha na kisha nilijifunza namna ya kuweka programu mbalimbali katika ordinatere. Kwenye Beteli, ninafurahia kusikia moja kwa moja ripoti juu ya maendeleo ya kazi ya kufanya wanafunzi katika dunia yote. Ninafurahia kutumika hapa kwa sababu mambo yenye tunafanya yanasaidia watu wamukaribie Yehova.”

UTAFANYA MIPANGO GANI JUU YA WAKATI WAKO UNAOKUJA?

14. Namna gani unaweza kufanya mipango ya kuanza utumishi wa wakati wote?

14 Namna gani unaweza kufanya mipango ili kufanya utumishi wa wakati wote? Kuwa na sifa za kiroho ndilo jambo la maana zaidi lenye litakusaidia kupata matokeo ya muzuri katika utumishi wa wakati wote kwa Yehova. Kwa hiyo, ujifunze Neno la Mungu kwa bidii, ufikiri sana juu ya maana yake, na utafute namna ya kutangaza imani yako kwenye mikutano ya kutaniko. Wakati ungali kwenye masomo, unaweza kufikia kuwa muhubiri wa habari njema mwenye uzoefu na ufundi. Ujifunze kupendezwa na watu kwa kuwauliza maulizo kwa ufundi na kusikiliza majibu yao. Pia, unaweza kuomba kufanya mambo fulani katika kutaniko, kama vile kusaidia kusafisha na kutunza Jumba la Ufalme. Yehova anapenda kutumia watu wenye kuwa na roho ya upole na wenye kuwa na roho ya kujitoa. (Soma Zaburi 110:3; Mdo. 6:1-3) Mutume Paulo alimualika Timotheo aende pamoja naye katika kazi ya umisionere kwa sababu “alishuhudiwa vema na akina ndugu.”​—Mdo. 16:1-5.

15. Namna gani unaweza kufanya mipango ili kujitimizia mahitaji yako?

15 Kwa kawaida, watumishi wa wakati wote wako na lazima ya kujitimizia mahitaji yao ya kimwili. (Mdo. 18:2, 3) Pengine kusoma masomo kidogo kutakusaidia kupata kazi yenye inaweza kupatikana katika eneo lenu. Wakati unafanya mipango, uzungumuze na mwangalizi wa muzunguko na mapainia wenye kuwa katika muzunguko wenu. Uwaulize ni kazi gani yenye kufaa kwa ajili ya mapainia. Na kama vile Biblia inasema, ‘umukabizi Yehova mwenyewe kazi zako nayo mipango yako itafanywa imara.’​—Met. 16:3; 20:18.

16. Namna gani kumutumikia Yehova wakati wote wakati ungali kijana kunakutayarisha kwa ajili ya madaraka mengine ya wakati unaokuja?

16 Unaweza kuwa hakika kuwa Yehova anapenda ‘uushike imara’ wakati unaokuja wenye furaha. (Soma 1 Timotheo 6:18, 19.) Utumishi wa wakati wote unakusaidia kujiunga na watumishi wengine wa wakati wote na kukusaidia ukuwe Mukristo mwenye kukomaa kiroho. Wengi wametambua kuwa kumutumikia Yehova wakati wote wakati walikuwa wangali vijana, kumewasaidia pia wakuwe na ndoa zenye furaha zaidi. Mara nyingi, wale wenye walifanya kazi ya upainia mbele wafunge ndoa wameweza kuendelea kufanya kazi hiyo pamoja hata kisha kuoana.​—Rom. 16:3, 4.

17, 18. Namna gani moyo wako unachangia katika kufanya mipango?

17 Moyo wako unachangia katika kufanya mipango. Zaburi 20:4 inasema hivi juu ya Yehova: “Na akupe kulingana na moyo wako, naye na alitimize kusudi lako lote.” Kwa hiyo, ufikirie namna unapenda kutumia maisha yako. Fikiria mambo yenye Yehova anafanya wakati wetu na uone namna gani unaweza kusaidia katika utumishi wake. Kisha upange kufanya mambo yenye kumupendeza.

18 Kumutumikia Yehova kwa wakati wote kutakuletea furaha kubwa zaidi kwa sababu hiyo ndiyo njia ya maisha yenye kumutukuza Mungu. Ndiyo, “upate furaha tele [nyingi] katika Yehova, naye atakupa maombi ya moyo wako.”​—Zab. 37:4.

^ fu. 7 Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme yamechukua nafasi ya masomo hayo.