Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kushinda Vita kwa Ajili ya Akili Yako

Namna ya Kushinda Vita kwa Ajili ya Akili Yako

UNASHAMBULIWA! Na adui yako mukubwa, Shetani, anatumia silaha hatari ili kukushambulia. Ni silaha gani? Ni propaganda! Kusudi la silaha hiyo ni kushambulia akili yako, hapana mwili wako.

Mutume Paulo alikuwa muangalifu juu ya hatari yenye propaganda ya shetani inaleta, lakini haiko Wakristo wenzake wote ndio walikuwa waangalifu. Kwa mufano, inawezekana wamoja katika Korintho, walianza kujitumainia kupita kiasi kwa kufikiri kuwa walikuwa na nguvu kiroho hivi kwamba hawangeweza kuanguka hata kidogo. (1 Kor. 10:12) Ndiyo sababu Paulo aliwatolea onyo hili: ‘Ninaogopa kwamba kwa njia fulani, kama nyoka alivyomushawishi Hawa [Eva] kwa ujanja wake, huenda akili zenu zikaharibiwa kutoka kwenye unyoofu wa moyo na usafi wa kiadili ambao unamufaa Kristo.’​—2 Kor. 11:3.

Onyo hilo la Paulo linaonyesha kuwa hatupaswe kujitumainia kupita kiasi. Ili kushinda vita kwa ajili ya akili yako, unapaswa kujua hatari yenye kuletwa na propaganda na kujilinda.

PROPAGANDA NI HATARI KADIRI GANI?

Propaganda ni nini? Katika habari hii, propaganda ni kutumia habari za uongo ili kuchochea namna ya watu ya kufikiri na kutenda. Watu fulani wanalinganisha propaganda na “uongo, kupotosha, kudanganya, kuchochea, kuongoza akili, [na] vita katika akili,” na wanaihusianisha na “ujanja mubaya, wenye kuharibu, na wenye haufae.”​—Propaganda and Persuasion.

Propaganda ni hatari kwa kadiri gani? Iko hatari kama gaze yenye kuwa na sumu yenye haionekane na yenye haina harufu, na inaingia polepole katika akili yetu. Kwa sababu tunaweza kukosa kujua ikiwa habari fulani ni za uongo, Vance Packard, mutu mwenye kujifunza tabia za watu, alisema hivi: Wengi kati yetu wanachochewa ao kuongozwa kwa ujanja kuliko namna tunaweza kuwazia.” Mutu mumoja mwenye elimu alisema kuwa propaganda imefanya wanaume na wanawake “wachochewe kwa vyepesi na tabia za mubaya sana zenye kuwa hatari” kama vile ‘kufanya mauaji makubwa, ubaguzi wa rangi ya ngozi, kuchukia sana dini fulani, na aina zingine za matendo ya mubaya.’​—Easily Led​—A History of Propaganda.

Ikiwa wanadamu wanaweza kutudanganya kupitia propaganda yao, Shetani iko na uwezo wa kutudanganya hata zaidi. Amejifunza tabia za wanadamu tangu wakati waliumbwa. Leo ‘ulimwengu muzima’ uko katika nguvu zake. Anaweza kutumia sehemu yoyote ya ulimwengu ili kueneza uongo wake. (1 Yoh. 5:19; Yoh. 8:44) Shetani amepata matokeo ya muzuri katika ‘kuzipofusha akili’ za watu hivi kwamba sasa ‘anaipotosha dunia nzima inayokaliwa.’ (2 Kor. 4:4; Ufu. 12:9) Namna gani unaweza kupinga propaganda yake?

TIA NGUVU UWEZO WAKO WA KUJILINDA

Yesu alitoa kanuni hii ya mwepesi ya kutusaidia kupiganisha propaganda: ‘Mutaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.’ (Yoh. 8:31, 32) Wakati wa vita, askari anapaswa kujua ni wapi kwenye anaweza kupata habari za kweli kwa sababu adui anaweza kueneza habari za uongo ili kumudanganya. Kwa hiyo, ni wapi unaweza kupata habari za kweli? Yehova ametoa habari hizo. Unaweza kupata katika Biblia habari zote zenye uko nazo lazima ili kupiganisha propaganda ya Shetani.​—2 Tim. 3:16, 17.

Kwa kweli, mutu mukubwa zaidi mwenye kueneza propaganda, ni kusema, Shetani, anajua jambo hilo. Kwa hiyo, anatumia ulimwengu wake ili kuchochea watu wasisome na kujifunza Biblia. Usianguke katika mitego yake yenye ujanja! (Efe. 6:11) Ukuwe na uwezo wa “kufahamu kabisa” mafundisho mbalimbali ya kweli. (Efe. 3:18) Kwa kweli, unapaswa kujikaza sana ili kufanya hivyo. Lakini kumbuka kweli hii ya musingi yenye muandikaji Noam Chomsky alisema: “Hakuna mutu mwenye anaweza kutia kweli katika akili yako. Ni kitu chenye unapaswa kutafuta wewe mwenyewe.” Kwa hiyo, ‘tafuta wewe mwenyewe’ kwa kuwa mwenye bidii katika ‘kuchunguza Maandiko kwa uangalifu kila siku.’​—Mdo. 17:11.

Ili kushinda vita kwa ajili ya akili yako, unapaswa kujua hatari yenye kuletwa na propaganda na kujilinda

Kumbuka kuwa Shetani hapendi ufikiri muzuri juu ya mambo mbalimbali. Sababu gani? Kwa sababu kitabu kimoja kinasema kuwa propaganda “inaweza kuwa na matokeo zaidi ikiwa watu . . . wameacha kufikiri ili kuchunguza ikiwa jambo fulani ni kweli ao ni uongo.” (Media and Society in the Twentieth Century) Kwa hiyo, usikubali ao kuamini tu bila kufikiri kila jambo lenye unasikia. (Met. 14:15) Utumikishe uwezo na nguvu zako za kufikiri zenye Mungu alikupatia ili kujihakikishia kwamba uko katika kweli.​—Met. 2:10-15; Rom. 12:1, 2.

UKUWE MWANGALIFU JUU YA NJIA ZA SHETANI ZA KUGAWANYA ILI KUTUSHINDA

Maaskari wanaweza kutumia kwa ufundi propaganda ili kuvunja maadui wao moyo na kuwafanya wakose nguvu za kupigana vita. Wanaweza kuchochea maadui wapigane wao kwa wao ao kuwadanganya ili wajitenge na maaskari wenzao wenye kupigana vita. Inasemekana kuwa Jenerali mumoja Mujerumani alisema kuwa sababu moja yenye iliwafanya washindwe katika Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ni kwamba watu “walipumbazwa akili na habari za uongo kutoka kwa adui kama vile nyoka anapumbaza sungura.” Shetani anatumia uongo kama huo ili kujaribu kutugawanya ili kutushinda. Kwa mufano anajikaza kuamusha mabishano kati ya ndugu na dada katika kutaniko ao kuwachochea wajitenge na tengenezo la Yehova kwa sababu ya mambo fulani yenye kuonekana kuwa ukosefu wa haki ao malalamiko.

Usidanganywe! Acha Neno la Mungu likuongoze. Kwa mufano, juu ya kuendeleza umoja kati ya ndugu na dada zako, Biblia inakutia moyo uendelee “kusameheana kwa hiari” na kufanya haraka ili kumaliza kukosa kuelewana. (Kol. 3:13, 14; Mt. 5:23, 24) Pia inatuonya sana juu ya kujitenga na kutaniko. (Met. 18:1) Ili kujua ikiwa unadanganywa ao hapana na propaganda ya Shetani, ujiulize hivi: ‘Ni nini iliongoza mawazo yangu wakati nilipambana na hali kama hiyo? Roho ya ulimwengu ao roho ya Mungu?’​—Gal. 5:16-26; Efe. 2:2, 3.

UENDELEE KUTUMAINIA WALE WENYE KUONGOZA

Askari mwenye ushikamanifu wake kwa kiongozi wake umeregezwa, hatapigana vita muzuri. Kwa hiyo, wale wenye kufanya propaganda wanajikaza kuvunja ushikamanifu na kufanya askari asitumainie kiongozi wake. Wanaweza kutumia propaganda kama hii: “Musitumainie viongozi wenu!” na “Musikubali wawaongoze kwenye musiba!” Ili kukazia mashambulizi yao, wanaweza kutumia kwa ujanja makosa yoyote yenye viongozi hao wanaweza kufanya. Shetani pia anafanya hivyo. Hachoke hata kidogo kujaribu kutuchochea tuache kutumainia uongozi wenye Yehova ametoa.

Utajilinda namna gani? Uazimie kushikamana ya tengeneza la Yehova na kutegemeza uongozi wenye anatoa hata kutokee hali gani za kukosa kukamilika. (1 Tes. 5:12, 13) ‘Usitikiswe upesi kutoka kwenye kufikiri kwako’ wakati unapambana na hali zenye kuwa kama mashambulizi hatari kutoka kwa waasi-imani ao watu wengine wenye kudanganya akili, hata kama mawazo yao yanaweza kuonekana kuwa ni ya kweli. (2 Tes. 2:2; Tito 1:10) Ufuate shauri lenye kijana Timotheo alipewa. Shikamana na kweli yenye ulijifunza na ukumbuke ulijifunza kweli hiyo kutoka kwa nani. (2 Tim. 3:14, 15) Kwa kweli kuna mambo mengi yenye kuhakikisha kuwa tunaweza kutumainia njia yenye Yehova ametumia kwa miaka mia moja hivi ili kutuongoza katika njia ya kweli.​—Mt. 24:45-47; Ebr. 13:7, 17.

USIACHE MAMBO YA KUOGOPESHA YA KUFANYE UKUWE ZAIFU

Ukumbuke kwamba wakati fulani propaganda ya Shetani inaweza kuonekana wazi-wazi. Wakati fulani, anatumia njia zenye kuogopesha; “aina moja ya zamani zaidi kati ya aina zote za propaganda.” (Easily Led​—A History of Propaganda) Kwa mufano, Profesa Mwingereza Philip Taylor aliandika kwamba Waashuru walitawala maadui wao kwa “kuwaogopesha kwa kutumia propaganda.” Shetani atatumia kuogopa mwanadamu, kuogopa mateso, kuogopa kifo, na woga mwengine wowote wenye haufae ili kujaribu kukutawala na kukufanya uache kumutumikia Yehova.​—Isa. 8:12; Yer. 42:11; Ebr. 2:15.

Usiruhusu Shetani atumie woga ili kukuvunja moyo ao kuvunja ushikamanifu wako. Yesu alisema hivi: ‘Musiwaogope wale wanaoua mwili na baada ya hilo hawawezi kufanya jambo lolote zaidi.’ (Lu. 12:4) Utumainie kabisa ahadi ya Yehova ya kukulinda, ya kukupatia “nguvu zinazopita zile za kawaida,” na kukusaidia upambane na mashambulizi ya Shetani yenye kuleta woga.​—2 Kor. 4:7-9; 1 Pet. 3:14.

Kwa kweli, unaweza kukutana na hali zenye kuogopesha na zenye kuvunja moyo. Lakini ukumbuke maneno haya yenye Yehova alimuambia Yoshua ili kumutia moyo: ‘Ukuwe hodari na mwenye nguvu. Usitetemeke wala usikuwe na hofu [woga], kwa maana Yehova Mungu wako yupo pamoja nawe kila mahali unapoenda.’ (Yos. 1:9) Wakati unakuwa na mahangaiko, bila kukawia umuelezee Yehova mahangaiko yako yote katika sala. Unaweza kuwa hakika kuwa ‘amani ya Mungu. . . italinda moyo wako na nguvu zako za akili’ ili ukuwe na nguvu za kupinga propaganda zote za Shetani.​—Flp. 4:6, 7, 13.

Unakumbuka propaganda yenye Rabshake mujumbe wa Waashuru alitumia juu ya watu wa Mungu? Ni kama vile alikuwa anasema kuwa, ‘Hakuna kitu chenye kinaweza kuwalinda juu ya Waashuru. Hata Yehova Mungu wenu, hawezi kuwasaidia.’ Aliongezea hivi bila kuogopa: ‘Yehova mwenyewe alituambia tuharibu inchi hii.’ Yehova naye alisema nini? ‘Usiogope kwa sababu ya maneno uliyosikia, ambayo watumishi wa mufalme wa Ashuru wamesema vibaya kunihusu.’ (2 Fal. 18:22-25; 19:6) Kisha alituma malaika mumoja mwenye aliua Waashuru 185 000 katika usiku moja!​—2 Fal. 19:35.

UKUWE NA HEKIMA​—UMUSIKILIZE YEHOVA SIKUZOTE

Umekwisha kuangalia filme fulani, na katika filme hiyo unaona namna mutu fulani anadanganywa? Inawezekana ulisema hivi katika moyo wako: ‘Usiamini jambo hilo! Wanakudanganya!’ Kwa hiyo, wazia malaika wanafanya hivyo pia kwa kukuambia hivi: “Usidanganywe na uongo wa Shetani!”

Kwa hiyo, ufunge masikio yako ili usisikilize propaganda ya Shetani. (Met. 26:24, 25) Umusikilize Yehova na umutumainie katika mambo yote yenye unafanya. (Met. 3:5-7) Ukubali mualiko wake huu wenye upendo: ‘Ukuwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie.’ (Met. 27:11) Kisha, utashinda vita kwa ajili ya akili yako!