Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unaona Lazima ya Kuzoeza Wengine?

Unaona Lazima ya Kuzoeza Wengine?

Nitawapa ninyi mafundisho mema.”METHALI 4:2.

NYIMBO: 93, 96

1, 2. Sababu gani tunapaswa kuzoeza wengine wafikie madaraka katika kutaniko?

YESU alitumika kwa bidii ili kuhubiri habari ya Ufalme. Pia, alitumia wakati mwingi ili kuzoeza wanafunzi wake. Aliwaonyesha namna ya kufundisha na namna ya kuhangaikia watu wa Mungu. Wanafunzi walijifunza namna ya kuwa kama vile wachungaji wenye kuhangaikia kondoo. (Mathayo 10:5-7) Filipo alihubiri pia kwa bidii, lakini alizoeza pia watoto wake wanamuke kufanya kazi hiyo. (Matendo 21:8, 9) Leo, sisi pia tunapaswa kuzoeza wengine. Sababu gani?

2 Katika makutaniko ya dunia yote, kuko wapya wengi wenye hawajabatizwa. Wapya hao wako na lazima ya mazoezi. Tunapaswa kuwasaidia waelewe sababu gani ni muzuri wasome na kujifunza Biblia kipekee. Na tena, tunapaswa kuwazoeza namna ya kuhubiri habari njema na kufundisha. Ndugu wenye wamebatizwa hivi karibuni wako na lazima ya mazoezi ili wafikie kuwa watumishi wa huduma na wazee wa kutaniko. Wote katika kutaniko wanaweza kujikaza ili kusaidia wahubiri wapya.—Methali 4:2.

FUNDISHA WAPYA NAMNA YA KUJIFUNZA BIBLIA

3, 4. (a) Namna gani mutume Paulo alionyesha kama kujifunza Maandiko kunatusaidia tupate matokeo ya muzuri katika kazi ya kuhubiri? (b) Mbele tutie moyo wanafunzi wetu wajifunze Biblia kipekee, sisi tunapaswa kuwa tunafanyaka nini?

3 Kila mutumishi wa Yehova anapaswa kusoma na kujifunza Biblia ili ajue mapenzi ya Mungu. Mutume Paulo alifasiria ndugu na dada wa kutaniko la Kolosai jambo hilo. Alisema hivi: ‘Hatujaacha kusali kwa ajili yenu na kuomba kwamba mujazwe ujuzi sahihi [wa kweli] wa mapenzi yake.’ Sababu gani lilikuwa jambo la maana sana wasome na kujifunza Maandiko? Kwa sababu hilo lingewapatia hekima na kuwasaidia waelewe namna ‘wangetembea kwa kumustahili Yehova.’ Pia, lingewasaidia kufanya “kila kazi njema” yenye Yehova alipenda wafanye, zaidi sana kazi ya kuhubiri habari njema. (Wakolosai 1:9, 10) Kwa hiyo, ikiwa tunajifunza na mutu fulani, tunapaswa kumusaidia aelewe kama kusoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida kunaweza kumusaidia amutumikie Yehova.

4 Hatuwezi kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia waone faida ya kujifunza Biblia kipekee ikiwa sisi wenyewe hatufanye hivyo. Kwa kweli, ikiwa tunasoma Biblia kwa ukawaida na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma, hilo litatusaidia katika maisha yetu na katika kazi ya kuhubiri. Kwa mufano, ikiwa mutu fulani anatuuliza ulizo lenye kuwa nguvu wakati tunahubiri, tutakuwa tayari kutumia Biblia ili kumujibia. Ao wakati tunasoma habari juu ya namna Yesu, Paulo, na wengine hawakuchoka katika kazi ya kuhubiri, tutatiwa moyo na tutaendelea kuhubiri hata wakati hali inakuwa ngumu. Na wakati tunaambia wengine mambo yenye tumejifunza katika funzo letu na namna yametusaidia, tunaweza kuwatia moyo wajifunze Biblia kwa uangalifu ili wao pia wapate faida hizo.

5. Namna gani unaweza kusaidia wapya wakuwe na programu ya kujifunza Biblia kipekee?

5 Unaweza kujiuliza hivi: ‘Namna gani ninaweza kusaidia mwanafunzi wangu ajifunze Biblia kwa ukawaida?’ Pengine unaweza kumuonyesha namna ya kutayarisha habari zenye kuwa katika kichapo chenye munajifunza naye. Unaweza kumuambia asome nyongeza ya habari yenye munazungumuzia katika kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? na asome pia maandiko ya Biblia yenye kuwa katika habari hiyo. Kisha, unaweza kumuonyesha namna ya kutayarisha mikutano ili aweze kutoa maelezo. Umutie moyo asome kila gazeti la Munara wa Mulinzi na Amuka! lenye linatokea. Na unaweza kumuonyesha namna ya kupata majibu ya maulizo ya Biblia, kwa mufano kwa kutumia Watchtower Library ao Watchtower—MAKTABA KWENYE INTERNETE. Ikiwa anajikaza kutumia njia hizo mbalimbali za kujifunza kipekee, pengine atafurahia funzo hilo na atapenda kujifunza mengi zaidi.

6. (a) Namna gani unaweza kusaidia mwanafunzi wako apende kabisa Biblia? (b) Mwanafunzi wa Biblia anaweza kufanya nini ikiwa anapenda kabisa Maandiko?

6 Wakati tunajifunza na mutu fulani, tunapenda atambue kama Biblia ni yenye faida kwa sababu itamusaidia afikie kumujua Yehova muzuri zaidi. Tusimukaze ajifunze, lakini tunaweza kumuonyesha namna anaweza kufurahia funzo hilo. Ikiwa anaendelea kujifunza mengi juu ya Biblia, atajisikia kabisa kama muandikaji mumoja wa zaburi mwenye aliimba hivi: ‘Kumukaribia Mungu ni kwema [muzuri] kwangu. Nimeweka kimbilio langu katika Bwana Mwenye Enzi Kuu [Mamlaka Makubwa Zaidi] Yehova.’ (Zaburi 73:28) Roho ya Yehova itasaidia kabisa mutu mwenye anapenda kumukaribia.

UWAZOEZE WAPYA KUHUBIRI NA KUFUNDISHA

7. Namna gani Yesu alizoeza wahubiri wa habari njema? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

7 Namna Yesu alizoeza mitume wake inaweza kutufundisha mambo mengi. Yesu alienda pamoja nao katika mahubiri, na waliona namna alifundisha watu. Pia, aliwapatia maagizo yenye kuwa wazi juu ya namna walipaswa kuhubiri. (Mathayo, sura ya 10) [1] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) Katika kipindi kifupi cha wakati, Yesu alifundisha mitume wake namna ya kufundisha wengine kweli. (Mathayo 11:1) Tuone mambo mbili yenye tunaweza kuzoeza wapya wafanye wakati wanahubiri.

8, 9. (a) Namna gani Yesu alizungumuza na watu katika mahubiri yake? (b) Namna gani tunaweza kusaidia wahubiri wapya wazungumuze na watu kama vile Yesu alifanya?

8 Zungumuza na watu. Yesu hakuzungumuza tu na vikundi vya watu. Mara nyingi alizungumuza na mutu mumoja-mumoja, na alizungumuza nao kwa njia ya urafiki. Kwa mufano, alikuwa na mazungumuzo yenye kupendeza pamoja na mwanamuke fulani mwenye alikuja kushota maji kwenye kisima karibu na muji wa Sikari. (Yohana 4:5-30) Pia, Yesu alizungumuza na Mathayo Lawi, mukusanya kodi (taxe), na alimualika akuwe mwanafunzi wake. Mathayo alikubali na kisha alialika Yesu na wengine wakuje nyumbani kwake ili wakule chakula. Katika nyumba hiyo, Yesu alizungumuza na watu wengi.—Mathayo 9:9; Luka 5:27-39.

Wakati tunazungumuza na watu kwa njia ya urafiki na kwa upole, pengine wanaweza kuwa tayari kabisa kusikiliza habari yenye tunawaletea

9 Pia, Yesu alizungumuza na Nathanaeli kwa njia ya urafiki, hata kama Nathanaeli alikuwa amesema mambo ya mubaya juu ya watu wa Nazareti. Kwa sababu Yesu alizungumuza naye kwa njia ya urafiki, Nathanaeli alibadilisha mawazo yake juu ya Yesu, mwenye alitoka Nazareti. Na alipenda kujifunza mengi juu ya Yesu. (Yohana 1:46-51) Mufano wa Yesu unatufundisha kama wakati tunazungumuza na watu kwa njia ya urafiki na kwa upole, pengine wanaweza kuwa tayari kabisa kusikiliza habari yenye tunawaletea. [2] [Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.] Wakati tunazoeza wapya kuzungumuza katika njia hiyo, watafurahia zaidi kazi ya kuhubiri.

10-12. (a) Namna gani Yesu alisaidia wale wenye walipendezwa na habari njema? (b) Namna gani tunaweza kusaidia wahubiri wapya wakomalishe ufundi wao wa kufundisha kweli za Biblia?

10 Fundisha wale wenye wako tayari kusikiliza. Yesu alikuwa na kazi nyingi ya kufanya. Lakini wakati watu walikuwa tayari kumusikiliza, alipitisha wakati pamoja nao na kuwafundisha mambo mengi. Kwa mufano, siku moja watu wengi walikusanyika pembeni ya bahari ili kumusikiliza Yesu. Kwa hiyo, Yesu alipanda katika mashua pamoja na Petro na kuanza kufundisha watu. Kisha hapo, alipenda pia kumufundisha jambo fulani. Yesu alifanya muujiza kwa kufanya Petro avue samaki wengi sana. Kisha alimuambia hivi: “Tangu sasa na kuendelea utakuwa ukiwavua watu wakiwa hai [wazima].” Mara moja Petro na wenzake ‘wakazirudisha mashua kwenye inchi kavu, wakaacha kila kitu’ na kumufuata Yesu.—Luka 5:1-11.

11 Nikodemo naye alipenda Yesu amufundishe mambo mengi. Lakini, kwa sababu Nikodemo alikuwa katika Sanhedrini, alikuwa anaogopa mambo yenye wengine wangesema ikiwa wangemuona anazungumuza na Yesu. Kwa hiyo, alimutembelea Yesu usiku. Yesu hakumufukuza, lakini alipitisha wakati pamoja naye na kumufasiria kweli za maana. (Yohana 3:1, 2) Sikuzote, Yesu alikuwa tayari kutumia wakati wake ili kufundisha watu kweli na kutia nguvu imani yao. Sisi pia, tunapaswa kuwa tayari kutembelea watu wakati wenye kufaa, na tunapaswa kupitisha wakati pamoja nao ili kuwasaidia waelewe mafundisho ya Biblia.

12 Wakati tunahubiri pamoja na wahubiri wapya, tunaweza kuwafundisha namna ya kurudilia kila mutu mwenye alionyesha kuwa anapendezwa. Tunaweza pia kualika wapya watusindikize kwenye marudio na mafunzo yetu ya Biblia. Ikiwa tunafanya hivyo, watajifunza namna ya kufundisha wengine na wataona kama ni jambo la muzuri sana kusaidia watu kama hao kujifunza kweli juu ya Yehova. Kisha, wahubiri hao wapya watafurahia sana kurudilia watu na kujifunza nao Biblia. Pia, watajifunza kuonyesha uvumilivu na kuepuka kuvunjika moyo haraka ikiwa hawapate tena watu nyumbani kwao.—Wagalatia 5:22; soma kisanduku “ Hakuchoka.”

ZOEZA WAPYA WAJIFUNZE KUTUMIKIA NDUGU ZAO

13, 14. (a) Biblia inazungumuzia watu wenye walijitoa sana ili kusaidia wengine, mifano hiyo inatufundisha nini? (b) Unaweza kutumia njia gani zenye kufaa ili kuzoeza wahubiri wapya na vijana waonyeshe ndugu na dada zao upendo?

13 Yehova anapenda watumishi wake wapendane kama vile ndugu na dada na watumikiane. (Soma Luka 22:24-27; 1 Petro 1:22.) Biblia inasema kama Yesu alitoa kila kitu, na hata uzima wake ili kusaidia wengine. (Mathayo 20:28) Dorkasi“alizidi katika matendo mema na zawadi za rehema.” (Matendo 9:36, 39) Maria ‘alifanya kazi’ kwa ajili ya ndugu na dada wa muji wa Roma. (Waroma 16:6) Namna gani tunaweza kusaidia wapya waelewe kama ni jambo la maana sana kufanya mambo ya muzuri kwa ajili ya ndugu na dada zao?

Zoeza wapya wapende na watumikie ndugu na dada zao

(Picha hii inapatana na fungu la 13 na 14)

14 Tunaweza kuomba wapya watusindikize wakati tunaenda kutembelea ndugu na dada wenye kuzeeka ao wagonjwa. Na wakati wazazi wanatembelea watu kama hao, wanaweza kuenda pamoja na watoto wao ikiwa inawezekana. Wazee wanaweza kuomba vijana ao wahubiri wapya watumike pamoja nao wakati wanapaswa kutolea ndugu na dada wenye kuzeeka chakula ao kutengeneza vitu fulani katika nyumba zao. Wakati vijana na wapya wanaona namna ndugu na dada wanahangaikiana, nao watajifunza kufanya hivyo. Kwa mufano, wakati alikuwa anahubiri katika eneo la mashamba, muzee mumoja alizoea kutembelea ndugu na dada wenye walikuwa wanaishi katika eneo hilo ili kujua hali yao. Mufano muzuri wa muzee huyo ulisaidia ndugu kijana mwenye alikuwa anaenda naye afikirie mambo yenye anaweza kufanya ili kusaidia ndugu na dada.—Waroma 12:10.

15. Sababu gani ni jambo la maana wazee wahangaikie maendeleo ya wanaume katika kutaniko?

15 Yehova amepatia wanaume daraka la kufundisha Neno la Mungu katika kutaniko. Kwa hiyo, ni jambo la maana ndugu wajifunze namna ya kufundisha muzuri wakati wanatoa hotuba. Ikiwa uko muzee, pengine unaweza kusikiliza mutumishi wa huduma wakati anarudilia hotuba fulani na kumusaidia afanye maendeleo. (Nehemia 8:8) [3]—Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.

16, 17. (a) Namna gani mutume Paulo alisaidia Timotheo afanye maendeleo? (b) Namna gani wazee wanaweza kuzoeza muzuri wale wenye watafikia kuwa wachungaji wa kesho wa kutaniko?

16 Kuko lazima ya kuzoeza ndugu wengi ili wakuwe wachungaji katika kutaniko. Mutume Paulo alizoeza Timotheo na alimutia moyo azoeze wengine. Alimuambia hivi: ‘Endelea kujipatia nguvu katika fazili zisizostahiliwa ambazo ni kuhusiana na Kristo Yesu; na mambo uliyoyasikia kutoka kwangu kwa usibitisho [uhakikisho] wa mashahidi wengi, mambo hayo uwakabizi [uwatolee] watu waaminifu, ambao nao watakuwa na sifa za kustahili vya kutosha kufundisha wengine.’ (2 Timotheo 2:1, 2) Paulo, alikuwa muzee na mutume; alifundisha Timotheo mambo mengi, kama vile namna ya kukomalisha ufundi wa kuhubiri na namna ya kusaidia wengine katika kutaniko.—2 Timotheo 3:10-12.

17 Mutume Paulo alipitisha wakati mwingi pamoja na Timotheo kwa sababu alipenda kuhakikisha kama Timotheo amepata mazoezi ya muzuri. (Matendo 16:1-5) Wazee wanaweza kuiga mufano wa mutume Paulo wakati wanaenda pamoja na watumishi wa huduma wenye kustahili ili kutembelea ndugu na dada fulani na kuwatia moyo. Kwa kufanya hivyo, wazee watafundisha watumishi wa huduma namna ya kufundisha wengine, namna ya kuonyesha uvumilivu na upendo, na namna ya kumutegemea Yehova wakati wanahangaikia kundi.—1 Petro 5:2.

KUZOEZA WENGINE NI JAMBO LA MAANA

18. Sababu gani ni jambo la maana tuzoeze wengine katika kazi ya Yehova?

18 Katika siku hizi za mwisho, wapya wengi wako na lazima ya mazoezi ili wakomalishe ufundi wao katika kazi ya kuhubiri. Pia, ndugu wako na lazima ya kujifunza namna ya kuhangaikia kutaniko. Yehova anapenda watumishi wake wote wapate mazoezi ya muzuri, na ametupatia pendeleo la kusaidia wapya. Kwa hiyo, ni jambo la maana kujikaza sana ili kuzoeza wengine, kama vile tu Yesu na mutume Paulo walifanya. Tunapaswa kuzoeza wengi zaidi kwa sababu kungali mengi ya kufanya katika kazi ya kuhubiri mbele mwisho ufike.

19. Sababu gani unapaswa kuwa hakika kama utapata matokeo ya muzuri ikiwa unajikaza sana ili kuzoeza wengine katika kazi ya Yehova?

19 Inaomba wakati na kujikaza ili kuzoeza wapya. Lakini tunaweza kuwa hakika kama Yehova na Yesu watatusaidia tujue namna ya kuzoeza wengine muzuri zaidi. Tutafurahi sana wakati tunaona wale wenye tulizoeza ‘wanafanya kazi kwa bidii na kujikaza wenyewe’ katika kutaniko ao katika kazi ya kuhubiri. (1 Timotheo 4:10) Na tunapaswa kuendelea kufanya nguvu yetu yote ili kufanya maendeleo ya kiroho, kukomalisha sifa zetu za Kikristo, na kumukaribia Yehova zaidi.

^ [1] (fungu la 7) Kwa mufano, Yesu aliambia wanafunzi wake (1) wahubiri habari ya Ufalme; (2) wategemee Mungu kuwa atawapatia chakula na manguo yenye wako nayo lazima; (3) waepuke kubishana na watu; (4) wamutumainie Mungu wakati watu wanawatesa; na (5) wasiogope mambo yenye watu wanaweza kuwafanyia.

^ [2] (fungu la 9) Mashauri ya muzuri sana juu ya namna tunaweza kuzungumuza na watu katika mahubiri yanapatikana katika kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ukurasa wa 62-64.

^ [3] (fungu la 15) Mashauri ya muzuri sana juu ya namna ndugu wanaweza kukomalisha ufundi wao wa kutoa hotuba katika kutaniko yanapatikana katika kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ukurasa wa 52-61.